< Romarbrevet 16 >
1 Jag befaller eder våra syster Phebe, hvilken är i församlingenes tjenst i Kenchrea.
Napenda kumtambulisha kwenu dada yetu Foibe, mtumishi katika kanisa la Kenkrea.
2 Att I henne undfången i Herranom, såsom helgon höfves; och görer henne bistånd i all ärende, der hon eder behöfver; ty hon hafver mångom, och jemväl mig sjelfvom, varit till godo.
Naomba mpokeeni katika Bwana ipasavyo watakatifu na kumpa msaada wowote atakaohitaji kutoka kwenu, kwa maana yeye amekuwa msaada kwa watu wengi, mimi nikiwa miongoni mwao.
3 Helser Priscilla, och Aqvila, mina hjelpare i Christo Jesu;
Wasalimuni Prisila na Akila, watumishi wenzangu katika Kristo Yesu.
4 Hvilke för mitt lif hafva vågat sin hals; dem tackar icke allenast jag, utan ock alla Hedningars församlingar.
Wao walihatarisha maisha yao kwa ajili yangu; wala si mimi tu ninayewashukuru bali pia makanisa yote ya watu wa Mataifa.
5 Helser ock församlingena i deras hus; helser Epenetus, min älskeliga, hvilken var den första frukt i Achajen, i Christo.
Lisalimuni pia kanisa linalokutana nyumbani mwao. Msalimuni rafiki yangu mpendwa Epaineto, aliyekuwa mtu wa kwanza kumwamini Kristo huko Asia.
6 Helser Maria, den der mycket arbete för oss haft hafver.
Msalimuni Maria, aliyefanya kazi kwa bidii kwa ajili yenu.
7 Helser Andronicus, och Junia, mina fränder och medfångar, de der märkelige äro ibland Apostlarna; de der ock för mig voro i Christo.
Wasalimuni Androniko na Yunia, jamaa zangu ambao wamekuwa gerezani pamoja nami. Wao ni maarufu miongoni mwa mitume, nao walikuwa katika Kristo kabla yangu.
8 Helser Amplia, min älskeliga i Herranom.
Msalimuni Ampliato, yeye nimpendaye katika Bwana.
9 Helser Urbanus, vår hjelpare i Christo, och Stachis, min älskeliga.
Msalimuni Urbano, mtendakazi mwenzetu katika Kristo, pamoja na rafiki yangu mpendwa Stakisi.
10 Helser Apellen, den der bepröfvad är i Christo; helser dem som äro af Aristobuli hus.
Msalimuni Apele aliyejaribiwa na akaithibitisha imani yake katika Kristo. Wasalimuni wote walio nyumbani mwa Aristobulo.
11 Helser Herodion, min frända; helser dem som äro af Narcissi hus, i Herranom.
Msalimuni ndugu yangu Herodioni. Wasalimuni wote walio nyumbani mwa Narkisi walio katika Bwana.
12 Helser Tryphena och Tryphosa, de der arbeta i Herranom; helser Persiden, mina älskeliga, som mycket arbetat hafver i Herranom.
Wasalimuni Trifaina na Trifosa, wale wanawake wanaofanya kazi kwa bidii katika Bwana. Msalimuni rafiki yangu mpendwa Persisi, mwanamke mwingine aliyefanya kazi kwa bidii katika Bwana.
13 Helser Rufum, den utkorada i Herranom; och hans moder, och mina.
Msalimuni Rufo, mteule katika Bwana, pamoja na mama yake, ambaye amekuwa mama kwangu pia.
14 Helser Asyncritum, Phlegontem, Herman, Patroban, Hermen, och de bröder som med dem äro.
Wasalimuni Asinkrito, Flegoni, Herme, Patroba, Herma na ndugu wote walio pamoja nao.
15 Helser Philologum, och Julian, Nereum, och hans syster, och Olympan, och all helgon när dem.
Wasalimuni Filologo, Yulia, Nerea na dada yake, na Olimpa na watakatifu wote walio pamoja nao.
16 Helser eder inbördes med en helig kyss; helsa eder Christi församlingar.
Salimianeni ninyi kwa ninyi kwa busu takatifu. Makanisa yote ya Kristo yanawasalimu.
17 Käre bröder, jag förmanar eder, att I hafven uppseende på dem, som tvist och förargelse åstadkomma, emot den lärdom som I hafven lärt; och viker ifrå dem.
Ndugu zangu, nawasihi mjihadhari na kujiepusha na wale watu waletao matengano na kuweka vikwazo mbele yenu dhidi ya mafundisho mliyojifunza.
18 Ty sådane tjena icke Herranom Jesu Christo, utan sinom buk; och igenom söt ord och smekande tal förföra deras hjerta, som menlöse äro.
Kwa maana watu kama hao hawamtumikii Bwana Kristo, bali wanatumikia tamaa zao wenyewe. Kwa kutumia maneno laini na ya kubembeleza, hupotosha mioyo ya watu wajinga.
19 Ty edar lydaktighet är utkommen till hvar man. Derföre fröjdar jag mig öfver eder; men jag vill, att I ären vise på det goda, och enfaldige på det onda.
Kila mtu amesikia juu ya utii wenu, nami nimejawa na furaha tele kwa ajili yenu. Lakini nataka mwe na hekima katika mambo mema na bila hatia katika mambo maovu.
20 Men fridsens Gud förträde Satanam under edra fötter snarliga. Vårs Herras Jesu Christi nåd vare med eder. Amen.
Mungu wa amani atamponda Shetani chini ya miguu yenu upesi. Neema ya Bwana wetu Yesu iwe nanyi. Amen.
21 Helsar eder Timotheus, min medhjelpare, och Lucius, och Jason, och Sosipater, mine fränder;
Timotheo, mtendakazi mwenzangu anawasalimu. Vivyo hivyo Lukio, Yasoni, na Sosipatro, ndugu zangu.
22 Helsar jag Tertius eder, som brefvet skrifvit hafver, i Herranom.
Mimi, Tertio, niliye mwandishi wa waraka huu, nawasalimu katika Bwana.
23 Helsar eder Gajus, min och hela församlingenes värd; helsar eder Erastus, stadsens räntomästare, och Qvartus, brodren.
Gayo, ambaye ni mwenyeji wangu na wa kanisa lote, anawasalimu. Erasto, mweka hazina wa mji huu, pamoja na Kwarto ndugu yetu pia wanawasalimu. [
24 Vårs Herras Jesu Christi nåd vare med eder allom. Amen.
Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe pamoja nanyi nyote. Amen.]
25 Men honom, som magt hafver att stadfästa eder, efter mitt Evangelium, och predikan af Jesu Christo, efter hemlighetenes uppenbarelse, den af evig tid härtill hafver förtegad varit; (aiōnios )
Sasa atukuzwe yeye awezaye kuwafanya ninyi imara kwa Injili yangu na kuhubiriwa kwa Yesu Kristo, kutokana na kufunuliwa siri zilizofichika tangu zamani za kale. (aiōnios )
26 Men nu uppenbarad och kungjord, igenom Propheternas skrifter, af eviga Guds befallning; på det tron skall få lydaktighet ibland alla Hedningar; (aiōnios )
Lakini sasa siri hiyo imefunuliwa na kujulikana kupitia maandiko ya kinabii kutokana na amri ya Mungu wa milele, ili mataifa yote yaweze kumwamini na kumtii (aiōnios )
27 Gudi, som är allena vis, vare pris och ära, genom Jesum Christum, i evighet. Amen. (aiōn )
Mungu aliye pekee, mwenye hekima, ambaye kwa njia ya Yesu Kristo utukufu ni wake milele na milele! Amen. (aiōn )