< Psaltaren 84 >

1 En Psalm Korah barnas, på Gittith, till att föresjunga. Huru lustige äro dina boningar, Herre Zebaoth!
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya wana wa Kora. Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, makao yako yapendeza kama nini!
2 Min själ längtar och trängtar efter Herrans gårdar. Min kropp och själ fröjda sig uti lefvandes Gudi.
Nafsi yangu inatamani sana, naam, hata kuona shauku, kwa ajili ya nyua za Bwana; moyo wangu na mwili wangu vinamlilia Mungu Aliye Hai.
3 Ty foglen hafver funnit ett hus, och svalan sitt bo, der de sina ungar lägga; nämliga ditt altare, Herre Zebaoth, min Konung och min Gud.
Hata shomoro amejipatia makao, mbayuwayu amejipatia kiota mahali awezapo kuweka makinda yake: mahali karibu na madhabahu yako, Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mfalme wangu na Mungu wangu.
4 Salige äro de som i dino huse bo, de lofva dig till evig tid. (Sela)
Heri wale wanaokaa nyumbani mwako, wanaokusifu wewe daima.
5 Salige äro de menniskor, som dig för sin starkhet hålla, och af hjertat efter dig vandra;
Heri wale ambao nguvu zao ziko kwako, na njia ziendazo Sayuni zimo mioyoni mwao.
6 De der gå genom jämmerdalen, och göra der källor; och lärarena varda med mycken välsignelse prydde.
Wanapopita katika Bonde la Baka, hulifanya mahali pa chemchemi, pia mvua za vuli hulijaza kwa madimbwi.
7 De vinna den ena segren efter den andra, att man se må, att den rätte Guden är i Zion.
Huendelea toka nguvu hadi nguvu, hadi kila mmoja afikapo mbele za Mungu huko Sayuni.
8 Herre Gud Zebaoth, hör min bön; akta härtill, Jacobs Gud. (Sela)
Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, sikia maombi yangu; nisikilize, Ee Mungu wa Yakobo.
9 Gud, vår sköld, skåda dock; se uppå din smordas rike.
Ee Mungu, uitazame ngao yetu, mtazame kwa wema mpakwa mafuta wako.
10 Ty en dag uti dina gårdar är bättre, än eljest tusende. Jag vill heldre vakta dörrena uti mins Guds huse, än länge bo uti de ogudaktigas hyddom.
Siku moja katika nyua zako ni bora kuliko siku elfu mahali pengine; afadhali ningekuwa bawabu katika nyumba ya Mungu wangu kuliko kukaa katika mahema ya waovu.
11 Ty Herren Gud är sol och sköld. Herren gifver nåd och äro; dem frommom skall intet godt fattas.
Kwa kuwa Bwana ni jua na ngao, Bwana hutoa wema na heshima; hakuna kitu chema anachowanyima wale ambao hawana hatia.
12 Herre Zebaoth, säll är den menniska, som sig förlåter uppå dig.
Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, heri ni mtu yule anayekutumaini wewe.

< Psaltaren 84 >