< Psaltaren 56 >

1 Ett gyldene klenodium Davids, till att föresjunga, om den dumba dufvona ibland de främmanda, då de Philisteer grepo honom i Gath. Gud, var mig nådelig, ty menniskor vilja nedersänka mig; dagliga strida de, och tränga mig.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Njiwa mkimya wa mbali.” Utenzi wa Daudi. Baada ya kukamatwa na Wafilisti huko Gathi. Ee Mungu unihurumie, maana watu wananifuatia vikali; mchana kutwa wanazidisha mashambulizi yao.
2 Mine fiender nedersänka mig dagliga ty månge strida emot mig högmodeliga.
Wasingiziaji wangu wananifuatia mchana kutwa, wengi wananishambulia kwa kiburi chao.
3 När jag fruktar mig, så hoppas jag uppå dig.
Wakati ninapoogopa, nitakutumaini wewe.
4 Jag vill prisa Guds ord; på Gud vill jag hoppas, och intet frukta mig. Hvad skulle något kött göra mig?
Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu, katika Mungu ninatumaini; sitaogopa. Mwanadamu apatikanaye na kufa, atanitenda nini?
5 Dagliga strida de emot min ord; alle deras tankar äro, att de må göra mig ondt.
Mchana kutwa wanayageuza maneno yangu, siku zote wanapanga shauri la kunidhuru.
6 De hålla tillhopa, och vakta, och taga vara uppå mina hälar, huru de mina själ gripa måga.
Wananifanyia hila, wanajificha, wanatazama hatua zangu, wakiwa na shauku ya kuutoa uhai wangu.
7 Hvad de ondt göra, det är allaredo tillgifvet ( säga de ). Gud störte sådana menniskor neder utan alla nåde.
Wasiepuke kwa vyovyote, Ee Mungu, katika hasira yako yaangushe mataifa.
8 Räkna min flykt; fatta mina tårar uti din lägel; utan tvifvel räknar du dem.
Andika maombolezo yangu, orodhesha machozi yangu katika gombo lako: je, haya hayapo katika kumbukumbu zako?
9 Då måste mina fiender tillbakavända. När jag ropar, förmärker jag, att du min Gud äst.
Ndipo adui zangu watarudi nyuma ninapoita msaada. Kwa hili nitajua kwamba Mungu yuko upande wangu.
10 Jag vill prisa Guds ord; Herrans ord vill jag prisa.
Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu, katika Bwana, ambaye neno lake ninalisifu,
11 Uppå Gud hoppas jag, och fruktar mig intet; hvad kunna menniskor göra mig?
katika Mungu ninatumaini, sitaogopa. Mwanadamu anaweza kunitenda nini?
12 Jag hafver gjort dig löfte, Gud, att jag dig tacka vill.
Ee Mungu, nina nadhiri kwako, nitakutolea wewe sadaka zangu za shukrani.
13 Ty du hafver frälst mina själ ifrå döden, mina fötter ifrå fall; att jag må vandra för Gudi uti de lefvandes ljuse.
Kwa kuwa umeniokoa toka kwenye mauti na miguu yangu kwenye kujikwaa, ili niweze kuenenda mbele za Mungu katika nuru ya uzima.

< Psaltaren 56 >