< Psaltaren 17 >

1 En bön Davids. Herre, hör rätthetena; gif akt uppå mitt rop, förnim mina bön, den icke utaf en falsk mun går.
Maombi ya Daudi. Sikia ombi langu kwa ajili ya haki, Yawhe; uusikilize mwito wangu wa msaada. Uyasikilize maombi yangu yatokayo katika midomo isiyo na udanganyifu.
2 Tala du i mine sak, och se du uppå hvad rätt är.
Uthibitisho wangu na uje kutoka uweponi mwako; macho yako na yaone kile kilicho sahihi!
3 Du pröfvar mitt hjerta, och besöker det om nattena, och ransakar mig, och finner intet; jag hafver satt mig före, att min mun icke öfverträda skall.
Kama utaujaribu moyo wangu, kama utakuja kwangu wakati wa usiku, wewe utanitakasa na hautapata mipango yeyote ya uovu; mdomo wangu hautavunja sheria.
4 Jag förvarar mig i dina läppars orde, för menniskors gerningar, på mördarens väg.
Kama kwa matendo ya binadamu, ni katika neno la midomo yako ya kuwa nimejiepusha na njia za wahalifu.
5 Behåll min gång på dinom stigom, att min steg icke slinta.
Mwenendo wangu umeshikila kwa umakini mwenendo wako; miguu yangu haija teleza.
6 Jag ropar till dig, att du Gud ville höra, mig; böj din öron till mig, hör mitt tal.
Nakuita wewe, kwa kuwa unanijibu, Mungu; geizia sikio lako kwangu na usikilize ninapo ongea.
7 Bevisa, dina underliga godhet, du, deras Frälsare, som trösta uppå dig, emot dem som sig emot dina högra hand sätta.
Onyesha uaminifu wa agano lako katika namna ya ajabu, wewe uokoaye kwa mkono wa haki yako wale wanao kukimbilia wewe kutoka kwa adui zao.
8 Bevara mig såsom en ögnasten; beskärma mig under dina vingars skugga;
Unilinde kama mboni ya jicho lako; unifiche katika kivuli cha mbawa zako
9 För de ogudaktiga, som mig förhärja; för mina ovänner, som efter mina själ stå allt omkring.
kutoka katika uwepo wa waovu ambao wananitusi, adui zangu wanizungukao.
10 Deras fete hålla tillsamman; de tala med sin mun stor ord.
Wao hawana huruma kwa yeyote; midomo yao huongea kwa majivuno.
11 Hvar vi gå, så äro de kringom oss; sina ögon ställa de derefter, att de måga slå oss till jordena;
Wao wame zizunguka hatua zangu. Wamekaza macho yao wanishambulie mpaka ardhini.
12 Såsom ett lejon, som rof begärar; såsom ett ungt lejon, som i kulone sitter.
Wao ni kama mfano wa hasira ya simba mawindoni. Ni kama simba kijana anapotokea mafichoni.
13 Herre, statt upp, öfverfall honom, och nederslå honom; undsätt mina själ ifrå de ogudaktiga, med ditt svärd;
Inuka, Yahwe! Uwashambulie! Uwaangushe chini kwenye nyuso zao! Uyaokoe maisha yangu kutokana na waovu kwa upanga wako!
14 Ifrå dine hands menniskom, Herre, ifrå denne verldenes menniskom, hvilka sin del hafva medan de lefva; dem du buken fyller med dina håfvor; de der barn nog hafva, och låta sina återlefvor sinom barnom.
Uniokoe kutoka kwa watu hawa kwa mkono wako, Yahwe, kutoka kwa watu wa dunia hii ambao utajiri wao ni maisha haya pekee! Wewe utayajaza matumbo ya wale uwathaminio na utajiri; watakuwa na watoto wengi na wataacha utajiri wao kwa watoto wao.
15 Men jag vill skåda ditt ansigte i rättfärdighet; jag vill mätt varda, när jag uppvakar efter ditt beläte.
Bali mimi, nitauona uso wako katika haki; Nitashuhudiwa, pale nitakapo amka, na macho yako.

< Psaltaren 17 >