< Psaltaren 132 >
1 En visa i högre choren. Tänk, Herre, uppå David, och uppå allt hans lidande;
Wimbo wa kwenda juu. Ee Bwana, mkumbuke Daudi na taabu zote alizozistahimili.
2 Hvilken Herranom svor, och lofvade dem mägtiga i Jacob:
Aliapa kiapo kwa Bwana na akaweka nadhiri kwa Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo:
3 Jag vill icke gå i mins hus hyddo, eller lägga mig på mine sängs lägre;
“Sitaingia nyumbani mwangu au kwenda kitandani mwangu:
4 Jag vill icke låta mina ögon sofva, eller mina ögnalock sömnoga vara;
sitaruhusu usingizi katika macho yangu, wala kope zangu kusinzia,
5 Tilldess jag må finna ett rum för Herranom, till en boning dem mägtiga i Jacob.
mpaka nitakapompatia Bwana mahali, makao kwa ajili ya Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo.”
6 Si, vi höre derom i Ephrata; vi hafve funnit det på skogsmarkene.
Tulisikia habari hii huko Efrathi, tulikutana nayo katika mashamba ya Yaara:
7 Vi vilje gå in uti hans boningar, och tillbedja inför hans fotapall.
“Twendeni kwenye makao yake, na tuabudu kwenye kiti cha kuwekea miguu yake;
8 Herre, statt upp till dina ro, du och din magts ark.
inuka, Ee Bwana, uje mahali pako pa kupumzikia, wewe na Sanduku la nguvu zako.
9 Låt dina Prester kläda sig med rättfärdighet, och dina heliga glädja sig.
Makuhani wako na wavikwe haki, watakatifu wako na waimbe kwa furaha.”
10 Tag icke bort dins smordas regemente, for din tjenare Davids skull.
Kwa ajili ya Daudi mtumishi wako, usimkatae mpakwa mafuta wako.
11 Herren hafver svorit David en sannan ed, der skall han intet ifrå träda: Jag skall sätta dig dins lifs frukt uppå din stol.
Bwana alimwapia Daudi kiapo, kiapo cha uhakika ambacho hatakitangua: “Nitamweka mmoja wa wazao wako mwenyewe katika kiti chako cha enzi,
12 Om dina barn hålla mitt förbund, och min vittnesbörd, som jag dem lärandes varder, så skola ock deras barn sitta på dinom stol evinnerliga.
kama wanao watashika Agano langu na sheria ninazowafundisha, ndipo wana wao watarithi kiti chako cha enzi milele na milele.”
13 Ty Herren hafver utvalt Zion, och hafver lust till att bo der.
Kwa maana Bwana ameichagua Sayuni, amepaonea shauku pawe maskani yake:
14 Detta är min hvila evinnerliga, här vill jag bo; ty här behagar mig väl.
“Hapa ni mahali pangu pa kupumzika milele na milele; hapa ndipo nitakapoketi nikitawala, kwa sababu nimepaonea shauku:
15 Jag vill välsigna dess spis, och gifva dess fattigom bröd nog.
Nitambariki kwa kumpa mahitaji tele: nitashibisha maskini wake kwa chakula.
16 Dess Prester vill jag bekläda med salighet, och dess helige skola glädja sig.
Nitawavika makuhani wake wokovu, nao watakatifu wake watadumu wakiimba kwa furaha.
17 Dersammastäds skall uppgå Davids horn; jag hafver tillredt minom smorda ena lykto.
“Hapa nitamchipushia Daudi pembe, na kuweka taa kwa ajili ya masiya wangu.
18 Hans fiendar vill jag bekläda med skam; men öfver honom skall hans krona blomstras.
Adui zake nitawavika aibu, bali taji kichwani pake itangʼaa sana.”