< Ordspråksboken 25 >

1 Desse äro ock Salomos Ordspråk, hvilka här tillsatt hafva Hiskia män, Juda Konungs.
Hizi ni mithali zaidi za Solomoni, zilizonakiliwa na watu wa Hezekia mfalme wa Yuda:
2 Det är Guds ära ena sak fördölja; men Konungars ära är ena sak utransaka.
Ni Utukufu wa Mungu kuficha jambo, bali ni utukufu wa wafalme kuchunguza jambo.
3 Himmelen är hög, och jorden djup; men Konungars hjerta är oransakeligit.
Kama mbingu zilivyo juu na nchi ilivyo chini, ndivyo ambavyo mioyo ya wafalme haichunguziki.
4 Man kastar bort slagget ifrå silfret, så varder der ett rent käril utaf.
Ondoa takataka kwenye madini ya fedha, nako ndani yake kutatokea chombo cha mfua fedha.
5 Man kastar ett ogudaktigt väsende bort ifrå Konungenom, så varder hans säte med rättfärdighet befäst.
Ondoa waovu mbele ya mfalme, nacho kiti chake cha enzi kitaimarishwa kwa njia ya haki.
6 Pråla icke för Konungenom, och träd icke fram der de store stå.
Usijikweze mwenyewe mbele ya mfalme, wala usidai nafasi miongoni mwa watu wakuu;
7 Ty det är dig bättre, när man till dig säger: Gack hitupp; än att du skulle för Förstanom förnedrad varda, det din ögon se måste.
ni afadhali yeye akuambie, “Njoo huku juu,” kuliko yeye kukuaibisha mbele ya mkuu. Kile ulichokiona kwa macho yako
8 Var icke hastig till att träta: ty hvad vill du sedan göra, när din nästa dig skämt hafver?
usiharakishe kukipeleka mahakamani, maana utafanya nini mwishoni kama jirani yako atakuaibisha?
9 Handla dina sak med din nästa, och uppenbara icke ens annars hemlighet;
Kama ukifanya shauri na jirani yako, usisaliti siri ya mtu mwingine,
10 På det att den det hörer icke skall tala dig illa till, och ditt onda rykte icke återvänder.
ama yeye aisikiaye aweza kukuaibisha na kamwe sifa yako mbaya haitaondoka.
11 Ett ord i sinom tid taladt är såsom ett gyldene äple uti silfskålom.
Neno lisemwalo kwa wakati ufaao ni kama matunda ya mtofaa ya dhahabu yaliyowekwa kwenye vijalizo vya fedha.
12 Den som en visan straffar, och han lyder honom, det är såsom en gyldene örnaring, och ett gyldene halsband.
Kama vile kipuli cha dhahabu au pambo la dhahabu safi, ndivyo lilivyo karipio la mtu mwenye hekima kwa sikio lisikilizalo.
13 Lika som snököld i andstiden, så är ett troget bådskap honom, som det sändt hafver, och vederqvicker sins herras själ.
Kama vile ubaridi wa theluji wakati wa mavuno ndivyo alivyo mjumbe mwaminifu kwa wale wamtumao, huburudisha roho za bwana zake.
14 Den der mycket talar, och håller intet, är såsom ett moln och väder utan regn.
Kama vile mawingu na upepo pasipo mvua ndivyo alivyo mtu ajisifuye kwa zawadi ambazo hatoi.
15 Genom tålamod varder en Förste blidkad, och en len tunga stillar hårdhetena.
Kwa njia ya uvumilivu mtawala aweza kushawishiwa, nao ulimi laini waweza kuvunja mfupa.
16 Finner du hannog, så ät så mycket som behöfves af honom, att du icke för mätt varder, och spyr det ut.
Ukipata asali, kula kiasi tu cha kukutosha, ukila zaidi, utatapika.
17 Drag din fot tillbaka ifrå dins nästas hus; han måste ledas vid dig, och varda dig vred.
Ingiza mguu wako nyumbani kwa jirani yako mara chache, ukizidisha, atakukinai na atakuchukia.
18 Den som emot sin nästa falskt vittnesbörd talar, han är ett spjut, svärd och skarp pil.
Kama vile rungu au upanga au mshale mkali ndivyo alivyo mtu atoaye ushuhuda wa uongo dhidi ya jirani yake.
19 Föraktarens hopp i nödenes tid är såsom en rutten tand, och en oviss fot.
Kama vile jino bovu au mguu uliolemaa, ndivyo ilivyo kumtegemea mtu asiye mwaminifu wakati wa shida.
20 Den för ett bedröfvadt hjerta visor qväder, det är såsom en sönderrifven klädnad om vintren, och ättika på krito.
Kama vile avuaye mavazi siku ya baridi, au kama siki iliyomwagwa juu ya magadi, ndivyo alivyo yeye amuimbiaye nyimbo mtu mwenye moyo mzito.
21 Hungrar din ovän, så spisa honom med bröd; törstar han, så gif honom vatten dricka;
Kama adui yako ana njaa, mpe chakula ale; kama ana kiu, mpe maji anywe.
22 Ty du samkar kol tillhopa uppå hans hufvud, och Herren vedergäller dig det.
Kwa kufanya hivyo, unaweka makaa ya moto yanayowaka kichwani pake, naye Bwana atakupa thawabu.
23 Nordanväder gör storm, och en hemlig tunga gör ett oblidt ansigte.
Kama vile upepo wa kaskazini uletavyo mvua, ndivyo ulimi usingiziao uletavyo uso wa hasira.
24 Det är bättre att sitta uti en vrå på taket, än när en trätosamma qvinno i ett stort nus.
Ni afadhali kuishi pembeni mwa paa la nyumba, kuliko kuishi nyumba moja na mke mgomvi.
25 Ett godt rykte utaf fjerran land är lika som kallt vatten ene törstigo själ.
Kama vile maji baridi kwa nafsi iliyochoka ndivyo zilivyo habari njema kutoka nchi ya mbali.
26 En rättfärdig, som för enom ogudaktigom faller, är såsom en rörd brunn och en förderfvad källa.
Kama vile chemchemi iliyotibuliwa matope au kisima kilichotiwa taka ndivyo alivyo mtu mwenye haki akishiriki na waovu.
27 Den som för mycken hannog äter, det är icke godt; och den svår ting utransakar, det varder honom för svårt.
Si vyema kula asali nyingi sana, wala si heshima kujitafutia heshima yako mwenyewe.
28 En man, som sin anda icke hålla kan, han är såsom en öppen stad utan murar.
Kama vile mji ambao kuta zake zimebomoka ndivyo alivyo mtu ambaye hawezi kujitawala mwenyewe.

< Ordspråksboken 25 >