< 4 Mosebok 8 >

1 Och Herren talade med Mose, och sade:
BWANA akanena na Musa, akamwambia,
2 Tala med Aaron, och säg till honom: När du uppsätter lamporna, skall du så sätta dem, att de alla sju lysa framföre ljusastakan.
“Sema na Haruni umwambie, 'zile taa saba lazima zimulike mbele ya kinara utakapoziwasha,”
3 Och Aaron gjorde så, och satte lamporna upp till att lysa framföre ljusastakan; såsom Herren hade budit Mose.
Haruni alifanya haya. Aliziwasha zile taa juu ya kinara ili ziangaze mbele yake kama BWANA alivyomwagiza Musa.
4 Men ljusastaken var af tätt guld, både hans lägg och hans blommor; efter den eftersyn, som Herren hade vist Mose, så gjorde han ljusastakan.
Kinara kilitengenezwa kwa njia hii kama BWANA alivyomwelekeza Musa muundo wake. Kiitakaiwa kutengenezwa kwa dhahabu kuanzia kwenye kitako chake hadi juu, ndivyo kilivyotakiwa kutengenezwa kwa dhahabu kwa maua hadi juu.
5 Och Herren talade med Mose, och sade:
Tena, BWANA akanena na Musa, akasema,
6 Tag Leviterna utur Israels barn, och rena dem.
'“Uwatwae Walawi kati ya wana wa Israeli na uwatakase.”
7 Och alltså skall du göra med dem, att du dem renar: Du skall stänka skärvatten på dem, och allt slätt afraka allt deras hår, och två deras kläder, så äro de rene.
Uwafanyie hivi ili kuwatakasa: Uwanyunyizie maji ya utakaso juu yao. Hakikisha wamenyoa miili yao yote, wafue nguo zao, na kwa njia hii wajitakase wenyewe.
8 Sedan skola de taga en ung stut, och hans spisoffer, semlomjöl, blandadt med oljo; och en annan ung stut skall du taga till syndoffer;
Kisha wachukue fahari mchanga na sadaka ya unga mwembamba uliochanganywa na mafuta. Halafu wachukue fahari mchanga kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
9 Och skall hafva Leviterna in för dörrena af vittnesbördsens tabernakel, och församla hela menighetena af Israels barn;
Uwalete Walawi mbele ya hema ya kukutania, na uwakusanye jamii yote ya wana wa Israeli.
10 Och hafva Leviterna fram för Herran; och Israels barn skola lägga sina händer på Leviterna.
Uwalete Walawi mbele yangu, BWANA. Wana wa Israeli wataweka mikono yao juu ya Walawi.
11 Och Aaron skall veftoffra Leviterna för Herranom utaf Israels barn, att de tjena skola i Herrans ämbete.
Haruni atawatoa Walawi mbele yangu, kuwa sadaka ya kutikiswa. Atafanya hivi ili kwamba Walawi wanitumikie.
12 Och Leviterna skola lägga sina händer på stutarnas hufvud; och den ene skall Herranom till ett syndoffer, och den andre till ett bränneoffer gjord varda, till att försona Leviterna.
Walawi wataweka mikono yao juu ya hao fahari. Mtatoa fahari mmoja kuwa sadaka ya dhambi na fahari mwingine kuwa sadaka ya kuteketezwa kwangu, ili kuwa upatanisho kwa Walawi.
13 Och du skall ställa Leviterna inför Aaron och hans söner, och veftoffra dem Herranom;
Walete Walawi mbele ya Haruni na mbele ya wana wake, uwainue kuwa sadaka ya kutikiswa kwa ajili yangu.
14 Och skall således afskilja dem ifrån Israels barn, att de skola vara mine.
Kwa njia hii utawatenganisha Walawi toka wana wa Israeli. Walawi watakuwa wangu.
15 Sedan skola de ingå till att tjena ut i vittnesbördsens tabernakel. Alltså skall du rena och veftoffra dem;
Baadaye Walawi wataingia ndani ya hema ya kukutania. Utawatakasa. utawatoa kuwa sadaka ya kutikiswa
16 Ty de äro min gåfva utaf Israels barn; och jag hafver tagit dem till mig för allt det som öppnar moderlif, nämliga för förstfödingen i all Israels barn.
Fanya hivi kwa sababu wao ni wangu wote kutoka kwa wana wa Israeli. Watachukua nafasi ya kila mzaliwa wa kwanza afunguaye tumbo, mzaliwa wa kwanza wa uzao wa Israeli. Nimewachukua Walawi kwa ajili yangu.
17 Förty all förstföding i Israels barn är min, både af menniskor och af fänad; den tid jag slog all förstföding i Egypti land, helgade jag dem mig;
Wazaliwa wa kwanza wote kutoka kwa wana wa Israeli ni wangu, watu wote pamoja na wanyama pia. Siku ile nilipowachukua wazaliwa wa kwanza katika nchi ya Misri, Niliwatenga kwa ajili yangu
18 Och tog Leviterna mig till för all förstföding ibland Israels barn;
Nimewachukua Walawi kutoka kwa wana wa Israeli badala ya wazaliwa wa kwanza.
19 Och gaf dem Aaron och hans söner för en gåfvo utur Israels barn, att de tjena skola i Israels barnas ämbete uti vittnesbördsens tabernakel, till att försona Israels barn; på det att ibland Israels barn icke skall komma en plåga, om de ville nalkas helgedomen.
Nimewatoa Walawi kuwa zawadi kwa Haruni na wana wake. Nimewachukua toka wana wa Isreali ili kuwatumikia wana wa Israeli katika hema ya kukutania. Nimewatoa ili kuwa upatanisho kwa watu ili kwamba wasipatwe na mapigo wakati wanapokaribia kwenye eneo takatifu.
20 Och Mose, med Aaron och hela menigheten af Israels barn, gjorde med Leviterna allt såsom Herren Mose budit hade.
Musa, Haruni na jamii ya Waisraeli wote waliwafanyia Walawi hivi. Walifanya kila kitu ambacho BWANA alikuwa amemwamuru Musa kuhusu Walawi. Wana wa Israeli wakafanya haya pamoja nao.
21 Och Leviterna renade sig, och tvådde sin kläder; och Aaron veftoffrade dem för Herranom, och försonade dem, att de vordo rene.
Walawi wakajitakasa wenyewe na kufua mavazi yao, Na Haruni akawatoa kama sadaka ya kutikiswa kwa BWANA na akafanya upatanisho kwao ili kuwatakasa.
22 Sedan gingo de in att göra sitt ämbete uti vittnesbördsens tabernakel, för Aaron och hans söner. Såsom Herren hade budit Mose om Leviterna, så gjorde de med dem.
Baada ya hayo, Walawi waliingia ndani kufanya utumishi wao katika hema ya kukutania mbele ya Haruni na mbele ya wanawe. Kama BWANA alivyokuwa amemwagiza Musa juu ya Walawi. Waliwahudumia Walawi wote kwa jinsi hii.
23 Och Herren talade med Mose, och sade:
BWANA akanena na Musa tena, Akasema,
24 Detta är det Leviterna bör: Ifrå fem och tjugu år, och derutöfver, doga de till ämbete och tjenst i vittnesbördsens tabernakel.
“Haya yote ni kwa ajili ya Walawi ambao wana umri wa miaka ishirini na mitano na zaidi. Wataungana na wale wanaohudumia hekaluni.
25 Men ifrå femtionde året skola de vara löse ifrå tjenstenes ämbete, och skola icke mera tjena;
Wataacha kutoa huduma hii watakapokuwa na umri wa miaka hamsini. Katika umri huu hawatakiwi kuendelea na huduma tena.
26 Utan taga vara på deras bröders tjenst uti vittnesbördsens tabernakel; men ämbetet skola de icke sköta. Alltså skall du göra med Leviterna, att hvar och en tager vara på sina vakt.
Wanaweza kuwasaidia ndugu zao wanaoendelea kufanya kazi ndani ya hema ya kukutania, lakini hawatakiwai kufanya kazi tena. Utawaelekeza Walawi kuyafahamu haya yote.”

< 4 Mosebok 8 >