< 4 Mosebok 34 >
1 Och Herren talade med Mose, och sade:
BWANA akanena na Musa akasema,
2 Bjud Israels barnom, och säg till dem: När I uti Canaans land kommen, så skall det landet, som eder till arfvedel faller i Canaans lande, hafva sin landamär.
“Waamuru watu wa Israeli na uwaambie, 'Mtakapoingia katika nchi ya Kanaani, nchi ambayo itakuwa mali yenu, nchi ya Kanaani na mipaka yake, mpaka wenu wa kusini utaendelea kutoka nyika ya Sini hadi mpaka wa Edomu.
3 Den sidan söderut skall begynna af den öknene Zin vid Edom, så att edart landamäre söderut skall vara ifrån ändanom af salthafvet, det österut ligger;
Mwisho wa mpaka wa kusini utakuwa mwisho wa bahari ya chumvi kuelekea mashariki.
4 Och att det landamäret skall sträcka sig ifrå sunnan uppåt intill Akrabbim, och gå igenom Zinna; och dess ända ifrå sunnan intill KadesBarnea, och räcka intill den byn Addar, och gå igenom Azmon;
Mpaka wenu utageukia kusini kutoka mlima kuelekea Akrabimu na kupitia nyika ya Sini. na kutokea huko utaelelkea kusini mwa Kadeshi Barinea na kuelekea Hazari Adari mpaka Azimoni.
5 Och skall sträcka sig ifrån Azmon allt intill Egypti bäck; och dess ände vare i hafvena.
Kutoka huko, mpaka utageuka kutoka Azimoni kuelekea kijito cha Misri na kukifuata mpaka baharini.
6 Men det landamäret vesterut skall vara detta, nämliga det stora hafvet; det skall vara edart landamäre vesterut.
Mpaka wa Magharibi utakuwa pwani ya bahari kuu. Huu ndio utakuwa mpaka wenuwa Magharibi.
7 Det landamäret norrut skall vara detta: I skolen mäta ifrå stora hafvet allt intill berget Hor;
Mpaka wenu wa kaskazini utaanzia kwenye bahari kuu hadi Mlima Hori,
8 Och ifrå berget Hor mäta intilldess man kommer till Hamath; så att dess utgång skall vara det landamäret Zedada;
kisha kutoka Mlima Hori hadi Lebo Hamathi, kisha Zedadi.
9 Och samma landamärens ände inåt Ziphron, och dess ände vare vid den byn Enan; det skall vara edart landamäre norrut;
Mpaka utaendelea hadi Zifroni na kuishia Hazari Enani. Huu ndio utakuwa mpaka wenu wa kaskazini.
10 Och skolen mäta eder landamäret österut, ifrå den byn Enan intill Sepham.
Kisha mtaweka alama za mpaka wenu wa mashariki ambao utaanzia Hazari Enani kuelekea kusini Shefamu.
11 Och det landamäret gånge nederåt ifrå Sepham intill Ribla, till Ain östanefter; sedan gånge nederåt, och drage sig uppmed sidone af hafvet Cinnereth österut;
Kisha mpaka wa kusini utaendelea kutoka Shefamu hadi Ribla, upande wa masharikia mwa Aini. Mpaka utaedelea upande huo wa mashariki hadi upande wa mashariki wa bahari ya Kinerethi.
12 Och komme neder åt Jordan, så att dess ände blifver salthafvet; det skall vara edart land med sin landamäre allt omkring.
Kisha mpaka utaendelea kuelekea kusini hadi mto Yorodani na hadi bahari ya chumvi. Hii ndiyo itakuwa nchi yenu, kwa kuifuata mipaka yake yote inayozunguka.'”
13 Och Mose böd Israels barnom, och sade: Detta är landet, som I skolen skifta emellan eder med lott, hvilket Herren budit hafver att gifva de nio slägter, och den halfva slägtene.
Kisha Musa akawaamuru watu wa Israeli akasema, “Hii ndiyo nchi ambayo mtaipokes kwa kura, ambayo BWANA ameamuru kuwapa wale makabila tisa na nusu.
14 Ty Rubens barnas slägte efter deras fäders hus, och Gads barnas slägte efter deras fäders hus, och den halfva slägten Manasse, hafva allaredo tagit sin del.
Kabila ya uzao wa Reubeni, kwa kufuata jinsi walivyopewa urithi kwa jamaa ya kabila yao, na uzao wa kabila la Gadi, kwa kufuata jinsi walivyopewa urithi kwa jamaa ya kabila yao, na nusu ya Manase wamepata ardhi yao.
15 Så hafva de två slägterna, och den halfva slägten, sin arfvedel på desso sidone Jordan in mot Jericho österut.
Wale makabila mawili na nusu wameshapata mgawo wao ng'ambo ya mto Yorodani upande wa mashariki, kuelekea kule linakotokea jua.”
16 Och Herren talade med Mose, och sade:
BWANA akanena na Musa akasema,
17 Desse äro namnen af männerna, som landet skola skifta emellan eder: Presten Eleazar, och Josua, Nuns son.
“Haya ndiyo majinaya watu watakaoigawa ardhi kwa ajili ya urithi wao: Eliazari kuhani na Joshua mwana wa Nuni.
18 Dertill skolen I taga Förstan af hvarjo slägtene, till att utskifta landet.
Mtachagua kiongozi mmoja toka kila kabila ili kuigawa ardhi kwa koo zao.
19 Och desse äro männernas namn: Caleb, Jephunne son, af Juda slägte.
Haya ndiyo majina ya wanaume: Kutoka kabila la Yuda, Kalebu mwana wa Yefune.
20 Semuel, Ammihuds son, af Simeons slägte.
Kutoka kwenye kabila la uzao wa Simeoni, Shemueli mwana wa Amihudi.
21 Elidad, Chislons son, af BenJamins slägte.
Kutoka kabila la Benjamini, Elidadi mwana wa Kisloni.
22 Bucki, Jogli son, Försten för Dans barnas slägte.
Kiongozi kutoka kabila la uzao wa Dani, Buki mwana wa Jogili.
23 Hanniel, Ephods son, Försten för Manasse barnas slägte, af Josephs barnom.
Kiongozi kutoka uzao wa Yusufu, kwenye kabila la Manase, Hannieli mwana wa Efodi.
24 Kemuel, Siphtans son, Försten för Ephraims barnas slägte.
Kiongozi kutoka kwenye kabila la uzao wa Efraimu, Kemueli mwana wa Shiftani.
25 Elizaphan, Parnachs son, Försten för Sebulons barnas slägte.
Kiongozi kutoka kabila la uzao wa Zabuloni, Elizafani mwana wa Parinaki.
26 Palthiel, Assans son, Försten för Isaschars barnas slägte.
Kiongozi kutoka kwenye kabila la uzao wa Isakari, Palitieli mwana wa Azzani.
27 Ahihud, Selomi son, Försten för Assers barnas slägte.
Kiongozi kutoka kabila la uzao wa Asheri, Ahihudi mwana wa Shelomi.
28 Pedahel, Ammihuds son, Försten för Naphthali barnas slägte.
Kiongozi kutoka kabila la uzao wa Naftali, Pedaheli mwana wa Amihudi.”
29 Desse äro de som Herren budit hafver, att de skulle utskifta Israels barnom arfvet i Canaans land.
BWANA aliwaamuru wanaume hawa kuigawa nchi ya Kanaani na kuwapa kila kabla sehemu yao.