< 4 Mosebok 29 >

1 Och den förste dagen i sjunde månadenom skall ibland eder kallas helig, att I sammankommen; intet tjenstearbete skolen I göra deruppå; det är eder trummetandes dag.
Katika siku ya kwanza, ya mwezi wa saba, mtakuwa na kusanyiko takatifu la kumwabudu BWANA. Katika siku hiyo hamtafanya kazi zenu za kila siku. Itakuwa siku ya kupiga matarumbeta.
2 Och I skolen göra bränneoffer till en söt lukt Herranom, en ungan stut, en vädur, sju årsgamla lamb utan vank.
Mtatoa sadaka ya kuteketezwa ya kufanya harufu nzuri kwa BWANA. Mtatoa sadaka ya fahari mchanga, kondoo dume mmoja na wanakondoo dume saba wa mwaka mmoja, kila mmoja mkamilifu.
3 Dertill deras spisoffer, tre tiungar semlomjöl, blandadt med oljo, till stuten, två tiungar till väduren;
Pamoja na hao mtatoa sadaka ya unga, unga mwembamba uliochanganywa na mafuta, sehemu tatu za kumi za efa kwa ajili ya huyo fahari, sehemu mbili za kumi kwa ajili ya huyo kondoo mume,
4 En tiung på hvart och ett af de sju lamben;
na sehemu ya kumi ya kila hao wanakondoo waume saba.
5 Och en getabock till syndoffer, till att försona eder;
Na mtatoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi ili kufanya upatanisho kwa ajili yenu.
6 Förutan månadens bränneoffer, och dess spisoffer, och förutan det dagliga bränneoffret med dess spisoffer, och med deras drickoffer, efter deras sätt, till en söt lukt; det är ett offer Herranom.
Toeni hizo sadaka katika mwezi wa saba kama nyongeza ya sadaka mtakazotoa kila mwanzo wa kila mwezi: pamoja na sadaka maalumu za kuteketezwa na sadaka za unga. Hizi zitakuwa nyongeza za sadaka za kuteketezwa za kila siku, na sadaka zake za unga, na sadaka zake za vinywaji. Utakapokuwa ukiendelea na sadaka hizi, utakuwa ukitii kile kilichoamriwa kutoa harufu nzuri, sadaka iliyotengenezwa kwa moto kwa BWANA.
7 Den tionde dagen i denna sjunde månadenom skall ock när eder kallas helig, att I sammankommen; och I skolen späka edra kroppar, och intet arbete deruppå göra;
Siku ya kumi ya mwezi wa saba, mtakuwa na kusanyiko takatifu la kumwabudu BWANA. Mtajinyeneyekeza na hamtafanya kazi.
8 Utan offra bränneoffer Herranom till en söt lukt, en ungan stut, en vädur, sju årsgamla lamb utan vank;
Mtatoa sadaka ya kuteketezwa ili kutoa harufu nzuri kwa BWANA. Mtatoa fahari mmoja mchanga ili kutoa harufu nzuri, kondoo mmoja mume, na wanakondoo saba waume wa mwaka mmoja. Wote wakamilifu.
9 Med deras spisoffer, tre tiungar semlomjöl, blandade med oljo, till stuten, två tiungar till väduren;
Pamoja na sadaka hizo utatoa sadaka ya unga, unga mwembamba uliochanganywa na mafuta, sehemu tatu za kumi za efa kwa ajili ya fahari, sehemu mbili za kumi za kondoo dume mmoja,
10 Och en tiung på hvart och ett af de sju lamben.
na sehemu ya kumi ya efa moja kwa kila mwanakondoo wale saba.
11 Dertill en getabock till syndoffer, förutan försoningens syndoffer, och det dagliga bränneoffret med sitt spisoffer, och med deras drickoffer.
Mtatatoa beberu mmoja kuwa sadaka ya upatanisho. Hii itakuwa sadaka ya nyongeza ya upatanisho, ya sadaka ya kila siku ya kuteketezwa, pamoja na sadaka za unga, na sadaka zake za vinywaji.
12 Den femtonde dagen i den sjunde månaden skall kallas helig när eder, att I sammankommen; intet tjenstearbete skolen I göra deruppå, och I skolen hålla Herranom helg i sju dagar;
Siku ya kumi na tano ya mwezi wa saba, mtakuwa na kusanyiko takatifu lakumwabudu BWANA. Siku hiyo hamtafanya kazi za kila siku, na mtazitunza hizo sikukuu kwa muda wa siku saba kwa ajili ya BWANA.
13 Och skolen göra bränneoffer till en söt lukts offer Herranom, tretton unga stutar, två vädrar, fjorton årsgamla lamb utan vank;
Mtatoa sadaka ya kuteketezwa, sadaka iliyotengenezwa kwa moto ilikutoa harufu nzuri kwa BWANA. Mtatoa mafahari wachanga kumi na tatu, kondoo waume wawili, na wanakondoo waume kumi na nne wa mwaka mmoja. Wote wakamilifu.
14 Med deras spisoffer, tre tiungar semlomjöl, blandadt med oljo, till hvar och en af de tretton stutar, två tiungar uppå hvar väduren af de två;
Pamoja na hao mtatoa sadaka ya unga, unga mwembaba uliochanganywa na mafuta, sehemu tatu za kumi za efa kwa kila fahari katika hao kumi na tatu, sehemu mbili za kumi kwa kila hao kondoo dume wawili,
15 Och en tiung uppå hvart och ett af de fjorton lamben.
na sehemu ya kumi ya efa ya hao wanakondoo kumi na nne.
16 Dertill en getabock till syndoffer, förutan det dagliga bränneoffret med sitt spisoffer och sitt drickoffer.
Mtatoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi katika nyongeza ya sadaka ya kuteketezwa, sadaka yake ya unga, pamoja na sadaka za vinywaji.
17 På den andra dagen, tolf unga stutar, två vädrar, fjorton årsgamla lamb utan vank;
Siku ya pili ya kusanyiko, mtatoa mafahari kumi na mbili, kondoo dume wawili na wanakondoo dume kumi na mbili wa umri wa mwaka mmoja, wote wakamilifu.
18 Med deras spisoffer och drickoffer, till stutarna, till vädrarna och till lamben, i deras tal efter sättet.
Pamoja nao mtatoa sadaka ya unga, na sadaka ya vinywaji kwa ajili ya wale mafahari, kondoo dume, na kwa ajili ya wale wanakondoo, mkitoa sadaka nyingi kama ilvyoamriwa.
19 Dertill en getabock till syndoffer, förutan det dagliga bränneoffret med sitt spisoffer, och med deras drickoffer.
Mtatoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi kuwa nyongeza ya sadaka za kila siku, sadaka yake ya unga, na sadaka zake za vinywaji.
20 På tredje dagen, ellofva stutar, två vädrar, fjorton årsgamla lamb utan vank;
Siku ya tatu ya kusanyiko, mtatoa sadaka mafahari kumi na moja, kondoo dume wawili, na wanakondoo dume kumi na nne wa umri wa mwaka mmoja, wakamilifu.
21 Med deras spisoffer och drickoffer, till stutarna, till vädrarna, och till lamben, i deras tal efter sättet.
Pamoja na hizo sadaka mtatoa sadaka ya unga na sdaka ya vinywaji kwa wale mafahari, kwa wale kondoo dume, na kwa wale wanakondoo, utoe sadaka nyingi kama ilivyoamriwa.
22 Dertill en getabock till syndoffer, förutan det dagliga bränneoffret, med sitt spisoffer och sitt drickoffer.
Mtatoa sadaka beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi kama nyongeza ya zile sadaka za kila siku, na sadaka zake za unga, na sadaka zake za vinywaji.
23 På fjerde dagen, tio stutar, två vädrar, fjorton årsgamla lamb utan vank;
Siku ya nne ya kusanyiko, mtatoa mafahari kumi, kondoo dume wawili, na wanakondoo dume kumi na nne wa mwaka mmoja, wakamilifu.
24 Med deras spisoffer och drickoffer, till stutarna, till vädrarna, och till lamben, i deras tal efter sättet.
Pamoja na sadaka hizo mtatoa sadaka za unga na sdaka za vinywaji kwa wale mafahari, na kwa wale kondoo dume na kwa wale wanakodoo, mtatoa sadaka nyingi kama ilivyoamriwa.
25 Dertill en getabock till syndoffer, förutan det dagliga bränneoffret med sitt spisoffer, och sitt drickoffer.
Mtatoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi kuwa nyongeza ya sadaka za kuteketezwa za kila siku, sadaka zake za unga, na sadaka zake za vinywaji
26 På femte dagen, nio stutar, två vädrar, fjorton årsgamla lamb utan vank;
Siku ya tano ya kusanyiko, mtatoa mafahari tisa, kondoo dume wawili, na wanakondoo dume kumi na nne wa mwaka mmoja, wakamilifu.
27 Med deras spisoffer och drickoffer, till stutarna, till vädrarna, och till lamben, i deras tal efter sättet.
Pamoja na sadaka hizo mtatoa sadaka za unga na sadaka ya vinywaji kwa ajili ya wale mafahari, kondoo dume, na wale wanakondoo, mkitoa sdaka nyingi kama ilivyoamriwa.
28 Dertill en getabock till syndoffer, förutan det dagliga bränneoffret, med sitt spisoffer, och sitt drickoffer.
Mtatoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi kama nyongeza ya sadaka za kuteketezwa za kila siku, na sadaka zake za unga, na sadaka za vinywaji.
29 På sjette dagen, åtta stutar, två vädrar, fjorton årsgamla lamb utan vank;
Siku ya sita ya kusanyiko, mtatoa mafahari wanane, kondoo dume wawili, na wanakondoo kumi na nne wa mwaka mmoja, wakamilifu.
30 Med deras spisoffer och drickoffer, till stutarna, till vädrarna, och till lamben, i deras tal efter sättet.
Pamoja na sadaka hizo mtatoa sadaka za unga nasadaka za vinywaji kwa wale mafahari, kondoo wa dume na wale wanakondoo, mkitoa sadaka nyingi kama ilivyoamriwa.
31 Dertill en getabock till syndoffer, förutan det dagliga bränneoffret, med sitt spisoffer, och sitt drickoffer.
Mtatoa beberu kuwa sadaka ya dhambi kama nyongeza ya sadaka za kila siku za kuteketezwa, sadaka zadaka zake za unga, na sadaka zake za vinywaji.
32 På sjunde dagen sju stutar, två vädrar, fjorton årsgamla lamb utan vank;
Siku ya saba ya kusanyiko, mtatoa mafahari saba, kondoo dume saba, na wanakondoo dume kumi na nne wa mwaka mmoja, wakamilifu.
33 Med deras spisoffer och drickoffer, till stutarna, till vädrarna, och till lamben, i deras tal efter sättet.
Pamoja nao mtataengeneza sadaka ya unga na sadaka ya vinywaji kwa ajili ya wale mafahari, na kondoo dume, na kwa wale wanakondoo, mkitoa sadaka nyingi kama ilivyoamriwa.
34 Dertill en getabock till syndoffer, förutan det dagliga bränneoffret, med sitt spisoffer, och sitt drickoffer.
Mtatoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi kama nyongeza ya sadaka ya kuteketezwa ya kila siku, na sadaka yake ya unga, na sadaka yake ya vinywaji.
35 På den åttonde skall vara församlingenes dag; intet tjenstearbete skolen I göra deruppå;
Siku ya nane mtakuwa na kusanyiko lingine makini. Hamtafanya kazi zenu za kila siku.
36 Och skolen offra bränneoffer till en söt lukts offer Herranom; en stut, en vädur, sju årsgamla lamb, utan vank;
Mtafanya sadaka za kuteketezwa, sadaka iliyotengenezwa kwa moto ili kutoa harufu nzuri kwa BWANA. Mtatoa fahari mmoja, kondoo mmoja dume, na wanakondoo saba dume wa umri wa mwaka mmoja, wakamilifu.
37 Med deras spisoffer och drickoffer, till stuten, till väduren, och till lamben, i deras tal efter sättet.
Mtatoa sadaka zake za unga na sadaka zake za vinywaji kwa ajili ya yule fahari, kondoo dume, na kwa wale wanakondoo, mkifanya sadaka nyingi kadri ilivyoamriwa.
38 Dertill en bock till syndoffer, förutan det dagliga bränneoffret, med sitt spisoffer och sitt drickoffer.
Mtatoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi kama nyongeza ya sadaka za kila siku, na sadaka zake za unga, na sadaka zake za vinywaji.
39 Detta skolen I göra Herranom i edra högtider, undantagno det I lofven och friviljoge gifven till bränneoffer, spisoffer, drickoffer och tackoffer.
Hivi ndivyo utakavyotoa sadaka kwa BWANA katika sikukuu zenu za kila mwaka. Hivi vitakuwa nyongeza ya viapo vyenu na sadaka zenu za hiari. Mtavitoa hivi kama sadaka zenu za kuteketezwa, sadaka za unga, sadaka za vinywaji, na sadaka za amani.”
40 Och Mose sade Israels barnom allt det Herren honom budit hade.
Musa aliwaambia wana wa Israeli kila kitu ambacho BWANA alikuwa amemwamuru kusema.

< 4 Mosebok 29 >