< 4 Mosebok 26 >
1 Och skedde efter denna plågona, att Herren talade med Mose och Eleazar, Prestens Aarons son, och sade:
Baada ya hiyo tauni, Bwana akamwambia Mose na Eleazari mwana wa kuhani Aroni,
2 Tag summona af hela menighetene af Israels barn, ifrå tjugu år och derutöfver, efter deras fäders hus, alla de som förmå draga i här i Israel.
“Hesabu jumuiya yote ya Kiisraeli kwa jamaa zao, wale wote wenye umri wa miaka ishirini na zaidi, ambao wanaweza kutumika katika jeshi la Israeli.”
3 Och Mose, samt med Eleazar Prestenom, talade på de Moabiters mark, vid Jordan in mot Jericho,
Hivyo Mose na kuhani Eleazari wakazungumza na watu kwenye nchi tambarare ya Moabu, ngʼambo ya Yordani kutokea Yeriko, wakasema,
4 Med dem, som tjugu åra gamle voro, och derutöfver, såsom Herren hade budit Mose och Israels barnom, som utur Egypti land dragne voro.
“Hesabuni wanaume wenye umri wa miaka ishirini na zaidi, kama Bwana alivyomwagiza Mose.” Hawa ndio Waisraeli waliotoka Misri:
5 Ruben, den förstfödde Israels son. Rubens barn voro: Hanoch, af hvilkom de Hanochiters slägt kommer: Pallu, af hvilkom de Palliters slägt kommer:
Wazao wa Reubeni, mwana mzaliwa wa kwanza wa Israeli, walikuwa: kutoka kwa Hanoki, ukoo wa Wahanoki; kutoka kwa Palu, ukoo wa Wapalu;
6 Hezron, af hvilkom de Hezroniters slägt kommer: Charmi, af hvilkom de Charmiters slägt kommer.
kutoka kwa Hesroni, ukoo wa Wahesroni; kutoka kwa Karmi, ukoo wa Wakarmi.
7 Dessa äro Rubens slägter; och deras tal var tre och fyratio tusend, sjuhundrad och tretio.
Hizi zilikuwa ndizo koo za Reubeni; wale waliohesabiwa walikuwa 43,730.
8 Men Pallu barn voro: Eliab.
Mwana wa Palu alikuwa Eliabu,
9 Och Eliabs barn voro: Remuel; och Dathan, och Abiram. Desse äro Dathan och Abiram, myndige män i den menighetene, som satte sig upp emot Mose och Aaron uti Korahs parti, då de satte sig upp emot Herran;
nao wana wa Eliabu walikuwa Nemueli, Dathani na Abiramu. Hawa wawili Dathani na Abiramu ndio walikuwa maafisa wa jumuiya ambao walimwasi Mose na Aroni, na walikuwa miongoni mwa wafuasi wa Kora wakati walimwasi Bwana.
10 Och jorden öppnade sin mun, och uppsvalg dem med Korah, då det partiet blefvo döde, och elden förtärde tuhundrad och femtio män; och voro till ett tecken.
Ardhi ilifunua kinywa chake na kuwameza pamoja na Kora, ambaye wafuasi wake walikufa wakati moto ulipowateketeza wanaume 250. Nao walikuwa kama alama ya onyo.
11 Men Korahs barn blefvo icke döde.
Pamoja na hayo, hao ukoo wa Kora hawakufa.
12 Simeons barn uti deras slägter voro: Nemuel, af honom kommer de Nemueliters slägt: Jamin, af honom kommer de Jaminiters slägt: Jachin, af honom kommer de Jachiniters slägt:
Wazao wa Simeoni kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Nemueli, ukoo wa Wanemueli; kutoka kwa Yamini, ukoo wa Wayamini; kutoka wa Yakini, ukoo wa Wayakini;
13 Serah, af honom kommer de Serahiters slägt: Saul, af honom kommer de Sauliters slägt.
kutoka kwa Zera, ukoo wa Wazera; kutoka kwa Shauli, ukoo wa Washauli.
14 Dessa äro Simeons slägter, tu och tjugu tusend, och tuhundrad.
Hizi ndizo koo za Simeoni; walikuwa 22,200.
15 Gads barn uti deras slägter voro: Zephon, af honom kommer de Zephoniters slägt: Haggi, af honom kommer de Haggiters slägt: Suni, af honom kommer de Suniters slägt:
Wazao wa Gadi kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Sifoni, ukoo wa Wasifoni; kutoka kwa Hagi, ukoo wa Wahagi; kutoka kwa Shuni, ukoo wa Washuni;
16 Osni, af honom kommer de Osniters slägt: Eri, af honom kommer de Eriters slägt:
kutoka kwa Ozni, ukoo wa Waozni; kutoka kwa Eri, ukoo wa Waeri;
17 Arod, af honom kommer de Aroditers slägt: Areli, af honom kommer de Areliters slägt.
kutoka kwa Arodi, ukoo wa Waarodi; kutoka kwa Areli, ukoo wa Waareli.
18 Dessa äro Gads barnas slägter: deras tal fyratiotusend och femhundrad.
Hizi ndizo zilizokuwa koo za Gadi; wale waliohesabiwa walikuwa 40,500.
19 Juda barn: Er och Onan, hvilke både blefvo döde i Canaans lande.
Eri na Onani walikuwa wana wa Yuda, lakini walifia huko Kanaani.
20 Och voro Juda barn i deras slägter: Sela, af honom kommer de Selaniters slägt: Perez, af honom kommer de Pereziters slägt: Serah, af honom kommer de Serahiters slägt.
Wazao wa Yuda kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Shela, ukoo wa Washela; kutoka kwa Peresi, ukoo wa Waperesi; kutoka kwa Zera, ukoo wa Wazera.
21 Men Perez barn voro: Hezron, af honom kommer de Hezroniters slägt: Hamul, af honom kommer de Hamuliters slägt.
Wazao wa Peresi walikuwa: kutoka kwa Hesroni, ukoo wa Wahesroni; kutoka kwa Hamuli, ukoo wa Wahamuli.
22 Dessa äro Juda slägter; deras tal sex och sjutio tusend, och femhundrad.
Hizi ndizo zilizokuwa koo za Yuda; wale waliohesabiwa walikuwa 76,500.
23 Isaschars barn i deras slägter voro: Thola, af honom kommer de Tholaiters slägt: Phuva, af honom kommer de Phuvaiters slägt:
Wazao wa Isakari kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Tola, ukoo wa Watola; kutoka kwa Puva, ukoo wa Wapuva;
24 Jasub, af honom kommer de Jasubiters slägt: Simron, af honom kommer de Simroniters slägt.
kutoka kwa Yashubu, ukoo wa Wayashubu; kutoka kwa Shimroni, ukoo wa Washimroni.
25 Dessa äro Isaschars slägter; deras tal fyra och sextio tusend, trehundrad.
Hizi ndizo zilizokuwa koo za Isakari; wale waliohesabiwa walikuwa 64,300.
26 Sebulons barn i deras slägter voro: Sered, af honom kommer de Sarditers slägt: Elon, af honom kommer de Eloniters slägt: Jahleel, af honom kommer de Jahleeliters slägt.
Wazao wa Zabuloni kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Seredi, ukoo wa Waseredi; kutoka kwa Eloni, ukoo wa Waeloni; kutoka kwa Yaleeli, ukoo wa Wayaleeli.
27 Dessa äro Sebulons slägter; deras tal sextiotusend, och femhundrad.
Hizi ndizo zilizokuwa koo za Zabuloni, wale waliohesabiwa walikuwa 60,500.
28 Josephs barn i deras slägter voro: Manasse och Ephraim.
Wazao wa Yosefu kwa koo zao kutoka kwa Manase na kwa Efraimu walikuwa:
29 Manasse barn voro: Machir, af honom kommer de Machiriters slägt: Machir födde Gilead, af honom kommer de Gileaditers slägt.
Wazao wa Manase: kutoka kwa Makiri, ukoo wa Wamakiri (Makiri alikuwa baba wa Gileadi); kutoka kwa Gileadi, ukoo wa Wagileadi.
30 Gileads barn äro: Jeser, af honom kommer de Jeseriters slägt: Helek, af honom kommer de Helekiters slägt:
Hawa ndio waliokuwa wazao wa Gileadi: kutoka kwa Iezeri, ukoo wa Waiezeri; kutoka kwa Heleki, ukoo wa Waheleki;
31 Asriel, af honom kommer de Asrieliters slägt: Sichem, af honom kommer de Sichemiters slägt.
kutoka kwa Asirieli, ukoo wa Waasirieli; kutoka kwa Shekemu, ukoo wa Washekemu;
32 Semida, af honom kommer de Semiditers slägt: Hepher, af honom kommer de Hepheriters slägt.
kutoka kwa Shemida, ukoo wa Washemida; kutoka kwa Heferi, ukoo wa Waheferi.
33 Men Zelaphehad var Hephers son, och hade inga söner, utan döttrar; de heto: Mahela, Noa, Hogla, Milca och Thirza.
(Selofehadi mwana wa Heferi hakuzaa wana, bali alikuwa na watoto wa kike tu, ambao majina yao yalikuwa Mahla, Noa, Hogla, Milka na Tirsa.)
34 Dessa äro Manasse slägter; deras tal tu och femtio tusend, och sjuhundrad.
Hizi ndizo zilizokuwa koo za Manase; wale waliohesabiwa walikuwa 52,700.
35 Ephraims barn i deras slägter voro: Suthelah, af honom kommer de Suthelahiters slägt: Becher, af honom kommer de Becheriters slägt: Thahan, af honom kommer de Thahaniters slägt.
Hawa walikuwa wazao wa Efraimu kwa koo zao: kutoka kwa Shuthela, ukoo wa Washuthela; kutoka kwa Bekeri, ukoo wa Wabekeri; kutoka kwa Tahani, ukoo wa Watahani;
36 Men Suthelahs barn voro: Eran, af honom kommer de Eraniters slägt.
Hawa ndio walikuwa wazao wa Shuthela: kutoka kwa Erani, ukoo wa Waerani.
37 Dessa äro Ephraims barnas slägter, deras tal tu och tretio tusend, och femhundrad. Dessa äro Josephs barn i deras slägter.
Hizi ndizo zilizokuwa koo za Efraimu; wale waliohesabiwa walikuwa 32,500. Hawa ndio waliokuwa wazao wa Yosefu kwa koo zao.
38 BenJamins barn i deras slägter voro: Bela, af honom kommer de Belaiters slägt: Asbel, af honom kommer de Asbeliters slägt: Ahiram, af honom kommer de Ahiramiters slägt:
Wazao wa Benyamini kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Bela, ukoo wa Wabela; kutoka kwa Ashbeli, ukoo wa Waashbeli; kutoka kwa Ahiramu, ukoo wa Waahiramu;
39 Supham, af honom kommer de Suphamiters slägt: Hupham, af honom kommer de Huphamiters slägt.
kutoka kwa Shufamu, ukoo wa Washufamu; kutoka kwa Hufamu, ukoo wa Wahufamu.
40 Men Bela barn voro: Ard och Naaman, af dem kommer de Arditers och Naamiters slägt.
Wazao wa Bela kutoka kwa Ardi na Naamani walikuwa: kutoka kwa Ardi, ukoo wa Waardi; kutoka kwa Naamani, ukoo wa Wanaamani.
41 Dessa äro BenJamins barn i deras slägter; deras tal fem och fyratio tusend, och sexhundrad.
Hizi ndizo zilizokuwa koo za Benyamini; wale waliohesabiwa walikuwa 45,600.
42 Dans barn i deras slägter voro: Suham, af honom kommer de Suhamiters slägt. Dessa äro Dans slägter i deras slägter.
Hawa ndio waliokuwa wazao wa Dani kwa koo zao: kutoka kwa Shuhamu, ukoo wa Washuhamu. Hizi ndizo zilizokuwa koo za Dani:
43 Och alle de Suhamiters slägte i deras tal voro fyra och sextio tusend, och fyrahundrad.
Wote walikuwa koo za Washuhamu; wale waliohesabiwa walikuwa 64,400.
44 Assers barn i deras slägter voro: Jimna, af honom kommer de Jimniters slägt: Jisvi, af honom kommer de Jisviters slägt: Beria, af honom kommer de Beriiters slägt.
Wazao wa Asheri kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Imna, ukoo wa Waimna; kutoka kwa Ishvi, ukoo wa Waishvi; kutoka kwa Beria, ukoo wa Waberia;
45 Men Beria barn voro: Heber, af honom kommer de Heberiters slägt: Malchiel, af honom kommer de Malchieliters slägt.
kutoka kwa wazao wa Beria: kutoka kwa Heberi, ukoo wa Waheberi; kutoka kwa Malkieli, ukoo wa Wamalkieli.
46 Och Assers dotter het Sarah.
(Asheri alikuwa na binti aliyeitwa Sera.)
47 Dessa äro Assers barnas slägter; deras tal tre och femtio tusend, och fyrahundrad.
Hizi ndizo zilizokuwa koo za Asheri; wale waliohesabiwa walikuwa 53,400.
48 Naphthali barn i deras slägter voro: Jahzeel, af honom kommer de Jahzeeliters slägt: Guni, af honom kommer de Guniters slägt:
Wazao wa Naftali kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Yaseeli, ukoo wa Wayaseeli; kutoka kwa Guni, ukoo wa Waguni;
49 Jezer, af honom kommer de Jezeriters slägt: Sillem, af honom kommer de Sillemiters slägt.
kutoka kwa Yeseri, ukoo wa Wayeseri; kutoka kwa Shilemu, ukoo wa Washilemu.
50 Dessa äro Naphthali slägter i deras slägter: deras tal fem och fyratio tusend, och fyrahundrad.
Hizi ndizo zilizokuwa koo za Naftali; wale waliohesabiwa walikuwa 45,400.
51 Detta är summan af Israels barn, sex gånger hundradetusend, ett tusend, sjuhundrad och tretio.
Jumla ya hesabu ya wanaume wa Israeli ilikuwa 601,730.
52 Och Herren talade med Mose, och sade:
Bwana akamwambia Mose,
53 Dessom skall du utskifta landet till arfs, efter namnens tal.
“Watagawiwa nchi kama urithi kwa kulingana na hesabu ya majina.
54 Mångom skall du gifva mycket till arfs, och fåm litet; hvarjom och enom skall man gifva efter deras tal.
Kundi kubwa zaidi lipe urithi mkubwa zaidi, na kundi dogo zaidi lipewe urithi mdogo zaidi; kila kundi litapokea urithi wake kulingana na hesabu ya wale walioorodheshwa.
55 Dock skall man skifta landet med lott; efter deras faders slägters namn skola de arf taga.
Hakikisha kuwa nchi inagawanywa kwa kura. Kile kitakachorithiwa na kila kikundi kitakuwa kwa kulingana na majina ya kabila la babu yao.
56 Ty efter lotten skall du utskifta dem arfvet, emellan de många och de få.
Kila urithi utagawanywa kwa kura miongoni mwa makundi makubwa na madogo.”
57 Och detta är summan af de Leviter uti deras slägter: Gerson, af hvilkom de Gersoniters slägt: Kehat, af hvilkom de Kehatiters slägt: Merari, af hvilkom de Merariters slägt.
Hawa walikuwa Walawi ambao walihesabiwa kwa koo zao: kutoka kwa Gershoni, ukoo wa Wagershoni; kutoka kwa Kohathi, ukoo wa Wakohathi; kutoka kwa Merari, ukoo wa Wamerari.
58 Dessa äro Levi slägter: De Libniters slägt, de Hebroniters slägt, de Maheliters slägt, de Musiters slägt, de Korahiters slägt; men Kehat födde Amram.
Hizi pia zilikuwa koo za Walawi: ukoo wa Walibni; ukoo wa Wahebroni; ukoo wa Wamahli; ukoo wa Wamushi; ukoo wa wana wa Kora. (Kohathi alikuwa baba aliyemzaa Amramu;
59 Och Amrams hustru het Jochebed, Levi dotter, den honom född var uti Egypten; och hon födde Amram, Aaron och Mose, och deras syster MirJam.
jina la mke wa Amramu ni Yokebedi, naye pia alikuwa mzao wa Lawi, ambaye alizaliwa kwa Walawi nchini Misri. Alimzalia Amramu: Aroni, Mose na dada yao Miriamu.
60 Men af Aaron vardt född Nadab, Abihu, Eleazar och Ithamar.
Aroni alikuwa baba yake Nadabu na Abihu, Eleazari na Ithamari.
61 Men Nadab och Abihu blefvo döde, då de offrade främmande eld för Herranom.
Lakini Nadabu na Abihu walikufa wakati walitoa sadaka mbele za Bwana kwa moto usioruhusiwa.)
62 Och deras tal var tre och tjugu tusend, allt mankön ifrå en månad och derutöfver; ty de vordo icke räknade ibland Israels barn; förty man gaf dem icke arf ibland Israels barn.
Wanaume wote wa Walawi wa umri wa mwezi mmoja na zaidi walikuwa 23,000. Wao hawakuhesabiwa pamoja na Waisraeli wengine kwa sababu hawakupokea urithi miongoni mwao.
63 Detta är summan af Israels barn, som Mose och Presten Eleazar talde på de Moabiters mark vid Jordan, in mot Jericho;
Hawa ndio walioorodheshwa na Mose na kuhani Eleazari wakati waliwahesabu Waisraeli kwenye nchi tambarare ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko.
64 Ibland hvilka var ingen utaf den summo, då Mose och Presten Aaron talde Israels barn uti Sinai öken.
Hakuna hata mmoja wao aliyekuwa miongoni mwa wale waliohesabiwa na Mose na kuhani Aroni wakati waliwahesabu Waisraeli katika Jangwa la Sinai.
65 Förty Herren hade sagt dem, att de skulle döden dö i öknene. Och ingen blef qvar, utan Caleb, Jephunne son, och Josua, Nuns son.
Kwa maana Bwana alikuwa amewaambia hao Waisraeli hakika wangekufa huko jangwani, wala hakuna mmoja wao aliyeachwa, isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune na Yoshua mwana wa Nuni.