< 4 Mosebok 18 >
1 Och Herren sade till Aaron: Du och dine söner, och dins faders hus med dig, skolen bära helgedomens missgerning; och du och dine söner med dig skolen bära edars Presterskaps missgerning.
Bwana akamwambia Aroni, “Wewe, wanao na jamaa ya baba yako mtawajibika kwa makosa dhidi ya mahali patakatifu, na wewe na wanao peke yenu ndio mtakaowajibika kwa makosa dhidi ya ukuhani.
2 Men dine bröder af Levi dins faders slägte skall du taga till dig, att de äro när dig, och tjena dig; men du och dine söner med dig skolen tjena inför vittnesbördsens tabernakel.
Walete Walawi wenzako kutoka kabila la baba zako ili waungane nanyi na kuwasaidia wakati wewe na wanao mnapohudumu mbele ya Hema la Ushuhuda.
3 Och de skola taga vara på din tjenst, och hela tabernaklets tjenst; dock skola de intet nalkas intill helgedomens tyg, och till altaret, att både de och I icke skolen dö;
Watawajibika kwenu na watafanya kazi zote za Hema, lakini kamwe wasisogelee vifaa vya patakatifu au madhabahu, la sivyo wao na ninyi mtakufa.
4 Utan de skola vara när dig, att de taga vara uppå vittnesbördsens tabernakels tjenst, uti all tabernaklets ämbete; och ingen främmande skall nalkas eder.
Watajiunga nanyi na watawajibika kwa utunzaji wa Hema la Kukutania, yaani kazi zote kwenye Hema, wala hakuna mtu mwingine yeyote atakayeweza kusogea karibu hapo mlipo.
5 Så akter nu uppå helgedomens tjenste, och uppå altarens tjenste, att icke mer en vrede kommer öfver Israels barn.
“Mtawajibika katika utunzaji wa mahali patakatifu na madhabahu, ili kwamba ghadhabu isiwaangukie Waisraeli tena.
6 Ty si, jag hafver tagit edra bröder Leviterna ut ifrån Israels barn, och gifvit eder Herranom till en skänk, att de skola taga vara på ämbetet vid vittnesbördsens tabernakel.
Mimi mwenyewe nimewachagua Walawi wenzenu kutoka miongoni mwa Waisraeli kama zawadi kwenu, waliowekwa wakfu kwa Bwana ili kufanya kazi katika Hema la Kukutania.
7 Men du och dine söner med dig skolen akta på edart Presterskap, att I tjenen uti all altarens handel, och innanför förlåten; ty edart Presterskap gifver jag eder till ett ämbete för en gåfvo; om någor främmande går härtill, han skall dö.
Lakini ni wewe tu na wanao mtakaoweza kutumika kama makuhani kuhusiana na kila kitu kwenye madhabahu na ndani ya pazia. Ninawapa utumishi wa ukuhani kama zawadi. Mtu mwingine yeyote atakayekaribia mahali patakatifu ni lazima auawe.”
8 Och Herren sade till Aaron: Si, jag hafver gifvit dig mitt häfoffer, af allt det som Israels barn helga, för ditt Prestaämbete, och dinom sönom till en evig rätt.
Kisha Bwana akamwambia Aroni, “Mimi mwenyewe nimekuweka kuwa mwangalizi wa sadaka zote zitakazotolewa kwangu; matoleo yote matakatifu Waisraeli wanayonipa ninakupa wewe na wanao kama sehemu yenu na fungu lenu la kawaida.
9 Detta skall du hafva af det aldrahelgasta, som de offra: Alla deras gåfvor med allt deras spisoffer, och med allt deras syndoffer, och med allt deras skuldoffer, som de mig gifva, det skall vara dig och dinom sönom det aldrahelgasta.
Mtachukua sehemu ya yale matoleo matakatifu sana ambayo hayateketezwi kwa moto. Kutoka kwa matoleo yote wanayoniletea kama sadaka takatifu sana, ziwe za nafaka, au za dhambi, au za makosa, sehemu ile itakuwa yako na wanao.
10 På aldrahelgasta rum skall du äta det; hvad mankön är, skall deraf äta; ty det skall vara dig heligt.
Mtaila kama kitu kilicho kitakatifu sana; kila mwanaume ataila. Ni lazima mtaiheshimu kama takatifu.
11 Jag hafver ock gifvit dig och dinom sönom, och dinom döttrom med dig, deras gåfvors häfoffer, i allo Israels barnas veftoffre till en evig rätt: Den som ren är i dino huse, han skall äta deraf.
“Hiki pia ni chako: chochote kilichotengwa kutoka kwenye matoleo yote ya sadaka za kuinuliwa za Waisraeli. Ninakupa wewe haya, wana na binti zako kama sehemu yenu ya kawaida. Kila mmoja wa nyumba yako ambaye ni safi kwa taratibu za ibada anaweza kuyala.
12 Alla bästa oljo, och all bästa vinmust, och deras förstlingskorn, det som de gifva Herranom, hafver jag gifvit dig.
“Ninawapa mafuta ya zeituni yaliyo bora kuliko yote, na divai mpya iliyo bora kuliko zote na nafaka wanazompa Bwana kama malimbuko katika mavuno yao.
13 Den första frukten af allt det i deras lande är, det som de bära Herranom, skall vara ditt; den som ren är i dino huse, han skall äta deraf.
Malimbuko yote ya nchi ambayo wanamletea Bwana yatakuwa yenu. Kila mmoja nyumbani kwako ambaye ni safi kwa taratibu za Ibada anaweza kula.
14 Allt det spillgifvet är i Israel, skall vara ditt.
“Kila kitu katika Israeli ambacho kimetolewa kwa Bwana ni chenu.
15 Allt det som moderlif öppnar ibland allt kött, det som de bära Herranom, vare sig menniska eller fänad, skall vara ditt; dock så, att du den första fruktena af mennisko låter lösa, och den första frukten af en oren fänad också lösa låter;
Kila mzaliwa wa kwanza wa mwanadamu na wa mnyama, ambaye ametolewa kwa Bwana ni wenu. Lakini ni lazima mtamkomboa kila mwana mzaliwa wa kwanza na kila mzaliwa wa kwanza wa kiume wa wanyama wasio safi.
16 Och skola de lösa det, när det är en månad gammalt; och skall gifvat till lösen för penningar, för fem siklar efter helgedomens sikel, hvilken tjugu gera gäller.
Watakapokuwa na umri wa mwezi mmoja, ni lazima mtawakomboa kwa bei ya ukombozi iliyowekwa, kwa shekeli tano za fedha, kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, yenye uzito wa gera ishirini.
17 Men den första frukten af fä eller får, eller get, skall du icke till lösen gifva; ty de äro helig. Deras blod skall du stänka på altaret, och deras feta skall du uppbränna till en söt lukts offer Herranom.
“Lakini kamwe usimkomboe mzaliwa wa kwanza wa maksai, kondoo au mbuzi; hawa ni watakatifu. Nyunyizia damu yao juu ya madhabahu na uchome mafuta yao kama sadaka itolewayo kwa moto, harufu nzuri inayompendeza Bwana.
18 Deras kött skall vara ditt, såsom ock veftebröstet, och högre bogen din är.
Nyama zao zitakuwa chakula chenu, kama ilivyokuwa kidari cha kuinuliwa na paja la mguu wa kulia.
19 Allt häfoffer, som Israels barn helga Herranom, hafver jag gifvit dig och dinom sönom, och dinom döttrom med dig till en evig rätt; det skall vara ett oförgängeligit och evigt förbund för Herranom, dig och dine säd med dig.
Chochote kitakachotengwa kutoka sadaka takatifu ambazo Waisraeli wanamtolea Bwana, ninakupa wewe, wanao na binti zako kama fungu lenu la kawaida. Ni Agano la milele la chumvi mbele za Bwana kwako na watoto wako.”
20 Och Herren sade till Aaron: Du skall ingen besittning hafva i deras land, och ingen lott hafva med dem; ty jag är din lott, och ditt arfvegods ibland Israels barn.
Bwana akamwambia Aroni, “Hutakuwa na urithi wowote katika nchi yao, wala hutakuwa na sehemu miongoni mwao; Mimi ni fungu lako na urithi wako miongoni mwa Waisraeli.
21 Men Levi barn hafver jag gifvit all tionde i Israel till ett arfvegods, för deras ämbete, som de göra mig vid vittnesbördsens tabernakel;
“Ninawapa Walawi zaka yote katika Israeli kama urithi wao kuwa kama malipo kwa kazi wanayoifanya wakati wanapohudumu katika Hema la Kukutania.
22 Så att härefter Israels barn intet skola nalkas intill vittnesbördsens tabernakel, till att komma sig i synd och dö;
Kuanzia sasa, kamwe Waisraeli wasisogelee karibu na Hema la Kukutania, la sivyo watabeba matokeo ya dhambi zao, nao watakufa.
23 Utan Leviterna skola akta på ämbetet vid vittnesbördsens tabernakel, och de skola bära deras synder till en evig rätt till edra efterkommande; och de skola intet arfvegods besitta ibland Israels barn.
Ni Walawi watakaofanya kazi katika Hema la Kukutania na kubeba wajibu wa makosa dhidi yake. Hili ni agizo la kudumu kwa vizazi vijavyo. Hawatapokea urithi wowote miongoni mwa Waisraeli.
24 Ty Israels barnas tiond, som de häfoffra Herranom, hafver jag gifvit Leviterna till arfvegods; derföre hafver jag sagt till dem, att de ibland Israels barn intet arfvegods besitta skola.
Badala yake, ninawapa Walawi zaka zote zinazotolewa na Waisraeli kama sadaka kwa Bwana kuwa urithi wao. Hiyo ndiyo sababu nimesema hivi kuhusu wao: ‘Hawatakuwa na urithi miongoni mwa Waisraeli.’”
25 Och Herren talade med Mose, och sade:
Bwana akamwambia Mose,
26 Tala till de Leviter, och säg till dem: När I tagen tionden af Israels barn, den jag eder af dem gifvit hafver till edart arfvegods, så skolen I göra Herranom deraf ett häfoffer, ju tiond af tiond;
“Sema na Walawi na uwaambie: ‘Mtakapopokea zaka kutoka kwa Waisraeli ambayo ninawapa kama urithi wenu kutoka kwao, ni lazima mtoe sehemu ya kumi ya hiyo zaka kama sadaka kwa Bwana, iwe zaka ya hiyo zaka.
27 Och skolen sådana edart häfoffer hålla såsom I gåfven korn af ladone, och fyllo af pressen.
Sadaka yenu itahesabiwa kwenu kama nafaka kutoka sakafu ya kupuria, au divai kutoka kwenye shinikizo la kukamulia zabibu.
28 Alltså skolen I ock gifva Herranom häfoffer af allo edro tiond, som I tagen af Israels barnom; så att I sådant Herrans häfoffer gifven Prestenom Aaron.
Kwa njia hii, ninyi pia mtatoa sadaka kwa Bwana kutoka zaka zote mtakazopokea kutoka kwa Waisraeli. Kutoka kwenye zaka hizi, ni lazima mtoe sehemu ya Bwana kwa Aroni, kuhani.
29 Utaf allt, det eder gifvet varder, skolen I gifva Herranom allahanda häfoffer, af allt det bästa, som deraf helgadt varder.
Ni lazima mtoe kama sehemu ya Bwana iliyo nzuri sana tena ile sehemu iliyo takatifu sana kuliko zote ya kile kitu mlichopewa.’
30 Och säg till dem: När I alltså det bästa deraf häfoffren, så skall det Levitomen räknadt varda, lika som det af ladone, och såsom det af pressen gåfves.
“Waambie Walawi: ‘Mtakapotoa sehemu zilizo bora sana, itahesabiwa kwenu kama mazao ya sakafu ya kupuria nafaka, au ya shinikizo la kukamulia zabibu.
31 Och I mågen det äta allestäds, I och edor barn; ty det är edor lön för edart ämbete uti vittnesbördsens tabernakel.
Ninyi na watu wa nyumbani mwenu mnaweza kula sehemu iliyobaki mahali popote, kwani ndio ujira wenu kwa ajili ya kazi yenu katika Hema la Kukutania.
32 Så synden I icke deröfver, när I häfoffren det feta deraf, och icke ohelgen det Israels barn helgat hafva, att I icke dön.
Kwa kutoa sehemu zake zilizo bora sana, hamtakuwa na hatia katika jambo hili; ndipo hamtatia unajisi sadaka takatifu za Waisraeli, nanyi hamtakufa.’”