< 3 Mosebok 4 >

1 Och Herren talade med Mose, och sade:
Bwana akamwambia Mose,
2 Tala med Israels barn, och säg: Om en själ syndar af ovetenhet emot något Herrans bud, som hon icke göra skulle;
“Waambie Waisraeli: ‘Mtu yeyote afanyapo dhambi bila kukusudia na akatenda lile lililokatazwa katika amri yoyote ya Bwana:
3 Nämliga, om en Prest, som smord är, syndar, så att han förargar folket, han skall för sina synd, som han gjort hafver, bära fram en ung stut, den utan vank är, Herranom till ett syndoffer;
“‘Ikiwa kuhani aliyetiwa mafuta amefanya dhambi na kuwaletea watu hatia, lazima alete kwa Bwana fahali mchanga asiye na dosari, kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili ya dhambi aliyotenda.
4 Och skall hafva stuten fram för Herran inför dörrena af vittnesbördsens tabernakel, och lägga sina hand på hans hufvud, och slagta honom för Herranom.
Atamkabidhi huyo fahali kwenye ingilio la Hema la Kukutania mbele za Bwana. Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha huyo fahali na kumchinja mbele za Bwana.
5 Och Presten, som smord är, skall taga af hans blod, och bära in uti vittnesbördsens tabernakel;
Kisha kuhani huyo aliyetiwa mafuta atachukua sehemu ya damu ya huyo fahali na kuileta katika Hema la Kukutania.
6 Och skall doppa sitt finger uti blodet, och stänka dermed sju resor för Herranom inför förlåten i det helga;
Atachovya kidole chake katika hiyo damu na kuinyunyiza sehemu yake mara saba mbele za Bwana mbele ya pazia la mahali patakatifu.
7 Och skall af samma blod stryka på hornen af rökaltaret, som står för Herranom inuti vittnesbördsens tabernakel, och gjuta allt blodet på bottnen af bränneoffrens altare, som står för dörrene till vittnesbördsens tabernakel.
Kisha kuhani atatia sehemu ya hiyo damu juu ya pembe za madhabahu ya kufukizia uvumba wenye harufu nzuri iliyoko mbele za Bwana katika Hema la Kukutania. Damu iliyobaki ya huyo fahali ataimwaga chini ya hayo madhabahu ya kuteketezea sadaka kwenye ingilio la Hema la Kukutania.
8 Och allt det feta af syndoffret skall han häfoffra, nämliga det feta, som är öfver inelfverna, och allt det feta, som invärtes är;
Atayaondoa mafuta yote ya fahali huyo wa sadaka ya dhambi, mafuta yale yanayofunika sehemu za ndani au zile zinazounganika nazo,
9 Båda njurarna med det feta, som derpå är vid länderna, och det nätet öfver lefrena med njurarna;
figo zote mbili na mafuta yaliyo juu yake karibu na kiuno na yale yanayofunika ini ambayo atayaondoa pamoja na figo zote,
10 Såsom man häfoffrar i tackoffret af oxanom; och skall uppbrännat på bränneoffrens altare.
kama vile mafuta yanayoondolewa kutoka kwenye maksai aliyetolewa sadaka ya amani. Kisha kuhani ataviteketeza juu ya madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa.
11 Men hudena af stuten med allt köttet, samt med hufvudet, och fötterna, och inelfverna, och gåret,
Lakini ngozi ya huyo fahali na nyama zake zote, pamoja na kichwa na miguu yake, sehemu za ndani na matumbo,
12 Det skall han allt utföra utu lägret, på ett rent rum, dit man slår askona, och skall uppbrännat på ved i elde.
yaani sehemu nyingine zote zilizobaki za huyo fahali, lazima azitoe nje ya kambi mpaka mahali palipo safi kiibada, ambapo majivu hutupwa, naye atamchoma kwa moto juu ya kuni zilizoko juu ya lundo la majivu.
13 Om en hel menighet i Israel försåge sig, och gerningen vore fördold för deras ögon, så att de gjort hade emot något Herrans bud, det de icke göra skulle, och vorde så brottslige;
“‘Ikiwa jumuiya yote ya Israeli watatenda dhambi pasipo kukusudia na kufanya lile lililokatazwa katika amri yoyote ya Bwana, hata kama jumuiya haifahamu juu ya jambo hilo, wana hatia.
14 Och förnumme så sedan sina synd, som de gjort hade; så skola de hafva en ung stut fram till syndoffer, och ställa honom för dörrena af vittnesbördsens tabernakel.
Wanapotambua kuhusu dhambi waliyoitenda, lazima kusanyiko lilete fahali mchanga kuwa sadaka ya dhambi na kuikabidhi mbele ya Hema la Kukutania.
15 Och de äldste af menighetene skola lägga deras händer på hans hufvud för Herranom, och slagta den stuten för Herranom.
Wazee wa jumuiya wataweka mikono yao juu ya kichwa cha huyo fahali aliye mbele za Bwana, naye fahali atachinjwa mbele za Bwana.
16 Och Presten, som smord är, skall bära bloden af stuten in uti vittnesbördsens tabernakel;
Kisha kuhani aliyetiwa mafuta ataiingiza sehemu ya damu ya huyo fahali ndani ya Hema la Kukutania.
17 Och doppa derin med sitt finger, och sju resor stänka för Herranom inför förlåten;
Atachovya kidole chake kwenye damu na kuinyunyiza mara saba mbele za Bwana mbele ya hilo pazia.
18 Och skall stryka af blodet på hornen af altaret, som står för Herranom uti vittnesbördsens tabernakel, och allt det andra blodet gjuta på bottnen af bränneoffersaltaret, som står för dörrene af vittnesbördsens tabernakel.
Atatia sehemu ya hiyo damu juu ya pembe za madhabahu yaliyo mbele za Bwana katika Hema la Kukutania. Damu iliyobaki ataimwaga chini ya madhabahu ya kuteketezea sadaka, penye ingilio la Hema la Kukutania.
19 Allt hans feta skall han häfoffra, och uppbränna på altaret;
Atayaondoa mafuta yote ya yule fahali na kuyateketeza juu ya madhabahu,
20 Och skall göra med denna stuten, såsom han gjorde med syndoffersstutenom. Och alltså skall Presten försona dem, och det varder dem förlåtet.
naye atamfanyia fahali huyu kama alivyomfanyia yule fahali mwingine wa sadaka ya dhambi. Kwa njia hii kuhani atawafanyia watu upatanisho, nao watasamehewa.
21 Och skall han föra stuten utu lägret och bränna honom upp, såsom han uppbrände den förra stuten. Det skall vara syndoffret för menighetene.
Kisha atamchukua yule fahali nje ya kambi na kumteketeza kama alivyomteketeza yule wa kwanza. Hii ni sadaka ya dhambi kwa ajili ya jumuiya.
22 Om en Förste syndar, och något gör emot Herrans sins Guds bud, det han icke göra skulle, och varder brottslig ovetandes;
“‘Wakati kiongozi ametenda dhambi bila kukusudia na kufanya yaliyokatazwa katika amri yoyote ya Bwana Mungu wake, ana hatia.
23 Och förnimmer sina synd, som han gjort hafver; han skall frambära till offers en getabock utan all vank;
Atakapofahamishwa dhambi aliyotenda, ni lazima alete mbuzi dume asiye na dosari kama sadaka yake.
24 Och lägga sina hand på bocksens hufvud, och slagta honom på det rum, der man slagtar bränneoffer för Herranom; det vare hans syndoffer.
Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha yule mbuzi na kumchinja mahali pale ambapo sadaka za kuteketezwa huchinjiwa mbele za Bwana. Hii ni sadaka ya dhambi.
25 Sedan skall då Presten taga af syndoffrens blod med sitt finger, och stryka det på hornen af bränneoffersaltaret, och det andra blodet gjuta på hornen af bränneoffrens altare.
Kisha kuhani atachukua sehemu ya damu ya sadaka ya dhambi kwa kidole chake na kuitia kwenye pembe za madhabahu ya sadaka ya kuteketeza, na kuimwaga damu iliyobaki chini ya madhabahu.
26 Men allt hans feta skall han uppbränna på altaret, lika såsom det feta af tackoffrena; och alltså skall Presten försona hans synd, och det varder honom förlåtet.
Atayateketeza mafuta yote juu ya madhabahu, kama alivyoteketeza mafuta ya sadaka ya amani. Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho wa dhambi kwa ajili ya yule mtu, naye atasamehewa.
27 Om en själ af meniga folket syndar ovetandes, så att hon ovetandes gör emot något Herrans bud, det hon icke göra skulle, och blifver så brottslig;
“‘Kama mtu katika jumuiya ametenda dhambi pasipo kukusudia na kufanya lile lililokatazwa katika amri yoyote ya Bwana, yeye ana hatia.
28 Eller förnimmer sina synd, som hon gjort hafver; hon skall bära fram för ett offer ena get utan vank, för syndena, som hon gjort hafver;
Atakapofahamishwa dhambi yake aliyoitenda, ni lazima alete mbuzi jike asiye na dosari kama sadaka yake kwa ajili ya dhambi aliyotenda.
29 Och skall lägga sina hand på syndoffrens hufvud, och slagta det på bränneoffrens rum.
Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha sadaka ya dhambi na kumchinjia mahali pa kuteketezea sadaka.
30 Och Presten skall taga af blodet med sitt finger, och stryka på hornen af bränneoffrens altare, och allt blodet gjuta på bottnen af altaret.
Kisha kuhani atachukua sehemu ya ile damu kwa kidole chake na kuitia kwenye pembe za madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa na kuimwaga damu iliyobaki chini ya madhabahu.
31 Allt hennes feta skall han aftaga, såsom han aftager det feta af tackoffrena, och skall uppbränna på altaret till en söt lukt Herranom. Och alltså skall Presten försona henne, och det varder henne förlåtet.
Atayaondoa mafuta yote, kama vile mafuta yaondolewavyo kwenye sadaka ya amani, naye kuhani atayateketeza juu ya madhabahu kama harufu nzuri ya kumpendeza Bwana. Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake, naye atasamehewa.
32 Men bär han fram ett får till syndoffer, så bäre en gymmer utan vank;
“‘Ikiwa ataleta mwana-kondoo kama sadaka yake ya dhambi, atamleta jike asiye na dosari.
33 Och lägge sina hand på syndoffrens hufvud, och slagte det till ett syndoffer, på det rummet, der man slagtar bränneoffret.
Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha huyo mwana-kondoo na kumchinja kwa ajili ya sadaka ya dhambi mahali sadaka ya kuteketezwa huchinjiwa.
34 Och Presten skall taga af blodet med sitt finger, och stryka på hornen af bränneoffrets altare, och gjuta allt blodet på bottnen af altaret.
Kisha kuhani atachukua sehemu ya damu ya sadaka ya dhambi kwa kidole chake na kuitia juu ya pembe za madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa, na ile damu iliyobaki ataimwaga chini ya madhabahu.
35 Men allt dess feta skall man aftaga, såsom han aftager det feta af tackoffrets fåre, och skall det uppbränna på altaret till ett Herrans offer. Och alltså skall Presten försona hans synd, den han gjort hafver, och honom varder det förlåtet.
Ataondoa mafuta yote, kama vile mafuta yaondolewavyo kutoka kwenye mwana-kondoo wa sadaka ya amani, naye kuhani atayateketeza juu ya madhabahu juu ya zile sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto. Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake kwa dhambi aliyoitenda, naye atasamehewa.

< 3 Mosebok 4 >