< 3 Mosebok 16 >

1 Och Herren talade med Mose, sedan de två Aarons söner döde voro, då de offrade för Herranom.
Yahwe alizungumza na Musa - hii ni baada vifo vya wana wawili wa Haruni, walipomkaribia Yahwe na ndipo wakafa.
2 Och Herren sade: Säg dinom broder Aaron, att han icke i alla tider ingår uti den innersta helgedomen, inom förlåten inför nådastolen, som på arkenom är, att han icke dör; ty jag vill låta se mig uti ett moln på nådastolenom;
Yahwe alimwambia Musa, “Ongea na Haruni kaka yako na umwambie hapana kuja tu wakati wowote katika patakatifu pa patakatifu ndani ya pazia, mbele ya kifuniko cha upatanisho kilicho juu ya sanduku. Akifanya hivyo, anakufa, kwasababu naonekana katika wingu juu ya kifuniko cha upatanisho.
3 Utan härmed skall han gå in: Med en ung stut till syndoffer, och med en vädur till bränneoffer;
Hivi ndivyo jinsi Haruni lazima aje katika patakatifu pa patakatifu. Yeye lazima aingie pamoja na ndama kama sadaka ya dhambi, na kondoo dume kama sadaka ya dhambi.
4 Och skall kläda den helga linna kjortelen uppå, och hafva det linna nederklädet uppå sitt kött, och gjorda sig med ett linnet bälte, och hafva den linna hatten uppå; förty det äro de helga kläden; och skall bada sitt kött med vatten, och lägga dem uppå;
Ni lazima avae kanzu ya kitatani, na lazima avae ndani yake nguo ya kitani, na lazima avae mshipi wa kitani na kilemba cha kitani. Haya ni mavazi matakatifu. Lazima aoge mwili wake katika maji na avae mavazi haya.
5 Och skall taga utaf menighetene af Israels barnom två getabockar till syndoffer, och en vädur till bränneoffer.
Lazima achukue kwenye umati wa watu wa Israeli mbuzi wawili waume kama sadaka ya dhambi na kondoo dume moja ikiwa ni sadaka ya kuteketezwa.
6 Och Aaron skall hafva fram stuten, sitt syndoffer, och försona sig och sitt hus;
Ndipo Haruni lazima alete ng'ombe kama sadaka ya dhambi, ambayo itakuwa kwaajili yake mwenyewe, kufanya upatanisho kwaajili yake mwenyewe na familia yake.
7 Och sedan taga de två bockarna, och ställa dem fram för Herran, inför dörrena af vittnesbördsens tabernakel;
Ndipo lazima achukue mbuzi wawili na kuwaweka mbele ya Yahwe katika mlango wa kuingilia kwenye hema ya mkutano.
8 Och skall kasta lott öfver de två bockarna; den ena lotten Herranom, den andra fribockenom;
Ndipo Haruni lazima apige kura kwaajili ya mbuzi hao wawili, kura moja kwaajili ya Yahwe, na kura nyingine kwaajili ya msingiziwa.
9 Och skall offra den bocken till ett syndoffer, på hvilken Herrans lott föll.
Ndipo Haruni lazima awasilishe mbuzi ambaye kura imeangukia kwa Yahwe, na kumtoa mbuzi huyo kama sadaka ya dhambi.
10 Men den bocken, öfver hvilken dess frias lott föll, skall han ställa lefvande fram för Herran, att han skall försona honom, och släppa den fribocken i öknena.
Lakini mbuzi ambaye kura ya usingiziwa imemwangukia lazima aletwe kwa Yahwe akiwa hai, kufanya upatanisho kwa kumwachia aende porini kama, mbuzimsingiziwa.
11 Och så skall han då hafva fram sins syndoffers stut, och försona sig och sitt hus, och skall slagta honom;
Pia Haruni lazima alete ng'ombe kwaajili ya sadaka ya dhambi, ambayo itakuwa kwaajili yake mwenyewe, lazima afanye upatanisho kwaajili yake mwenyewe na familia yake, hivyo lazima yeye amuue huyo ng'ombe kama sadaka ya dhambi kwaajili yake mwenyewe.
12 Och skall taga ena panno, full med glöd af altaret, som står för Herranom, och handena fulla med stött rökverk, och bära det inom förlåten;
Haruni lazima achukue chetezo iliyojaa mkaa wa moto kutoka kwenye madhabahu mbele ya Yahwe, na mikono imejaa ubani mzuri, na kuleta vitu hivi ndani ya pazia.
13 Och lägga rökverket på elden inför Herranom, så att dambet af rökverket skyler nådastolen, som är på vittnesbördet, att han icke dör;
Hapo lazima aweke ubani juu ya moto mbele za Yahwe ili kwamba wingu kutoka kwenye ubani liweze kufunika kifuniko cha agano la imani ya upatanisho. Yeye afanye hivyo ili kwamba asife.
14 Och skall taga blodet af stutenom, och stänka med sitt finger upp åt nådastolen, frammantill. Sju resor skall han så stänka af blodet för nådastolenom med hans finger.
Ndipo lazima achukue kiasi cha damu ya ng'ombe na kuinyunyiza kwa kidole chake mbele ya kifuniko cha upatanisho. Lazima anyunyize kiasi cha damu kwa kidole chake mara saba mbele ya kifuniko cha upatanisho.
15 Sedan skall han slagta bocken, folkens syndoffer, och bära af hans blod derinom förlåten, och skall göra med hans blod såsom han gjorde med stutens blod, och stänka desslikes dermed frammantill, upp åt nådastolen;
Ndipo lazima aue mbuzi kwaajili ya sadaka ya dhambi ambayo ni kwaajili ya watu na kuileta damu yake ndani kwenye pazi. Hapo lazima aifanyie damu kama alivyofanya kwenye damu ya fahali: lazima ainyunyize juu ya kifuniko cha upatanisho na mbele ya kifunuko cha upatanisho.
16 Och skall alltså försona helgedomen af Israels barnas orenhet, och ifrå deras öfverträdelse i alla deras synder. Sammalunda skall han göra vittnesbördsens tabernakel; ty de äro orene, som omkring ligga.
Yeye lazima afanye upatanisho kwaajili ya mahali patakatifu kwa sababu ya matendo ya unajisi ya watu wa Israeli, na kwa sababu ya uasi na dhambi zao zote. Yeye pia lazima afanye haya kwaajili ya hema ya mkutano, ambapo Yahwe anaishi kati yao, katika uwepo wa matendo yao ya unajisi.
17 Ingen menniska skall vara inuti vittnesbördsens tabernakel, när han går derin till att försona i helgedomenom, tilldess han går ut igen; och skall alltså försona sig och sitt hus, och hela Israels menighet.
Hakuna mtu anayetakiwa kuwepo katika hema ya mkutano wakati Haruni anaingia kufanya upatanisho katika mahali patakatifu pa patakatifu, na mpaka atoke nje na amemaliza kufanya upatanisho kwaajili yake mwenyewe na kwaajili ya familia yake, na kwaajili umati wa Israeli.
18 Och när han utgår till altaret, som står för Herranom, skall han försona det; och skall taga af stutens blod, och af bockens blod, och stryka på altarens horn allt omkring;
Yeye lazima aende nje kwenye madhabahu hapo mbele za Yahwe na kufanya upatanisho kwaajili ya hiyo, na lazima achukue kiasi cha damu ya mbuzi na kuiweka juu ya pembe za madhabahu yote kuzunguka.
19 Och skall stänka af blodet med sitt finger sju resor deruppå, och rensa, och helga det af Israels barnas orenhet.
Anatakiwa anyunyize kiasi cha damu juu yake kwa kidole chake mara saba kuitakasa na kuitenga maalumu kwa Yahwe, mbali kutoka matendo ya unajisi wa watu wa Israeli.
20 Och när han fullkomnat hafver helgedomens och vittnesbördsens tabernakels och altarens försoning, skall han hafva fram den lefvande bocken;
Atakapo maliza kupatanisha kwaajili ya mahali patakatifu sana, hema la mkutano, na madhabahu, lazima amlete mbuzi aliyehai.
21 Och skall då Aaron lägga båda sina händer på hans hufvud, och bekänna öfver honom alla Israels barnas missgerningar, och all deras öfverträdelse i alla deras synder, och skall lägga dem på bockens hufvud, och låta honom löpa genom någon mans hjelp, som förhanden är, i öknena;
Haruni lazima aweke mikono yake yote juu ya kichwa cha mbuzi huyu aliyehai na akiri juu yake maovu yote ya watu wa Israeli, uasi wao wote, dhambi zao zote. Ndipo lazima aweke dhambi hizo juu ya kichwa cha mbuzi na amwachie katika uangalizi wa mtu aliyetari kumwongoza mbuzi huyo porini.
22 Att bocken skall bortbära alla deras missgerningar på sig uti vildmarkena; och låta honom i öknene.
Mbuzi lazima abebe juu yake mwenyewe uovu wote kwenda mahali pakiwa. Kule msituni, huyo mtu amwache mbuzi aende huru.
23 Och Aaron skall gå in uti vittnesbördsens tabernakel, och afkläda sig de linna kläden, som han på sig klädt hade, då han gick in uti helgedomen, och skall der låta blifva dem;
Ndipo Haruni anapaswa kwenda tena humo kwenye hema ya mkutano na kuvua mavazi ya kitani ambayo amayavaa kabla hajaenda mahali patakatifu sana, na anatakiwa kuyaacha mavazi hayo pale.
24 Och skall bada sitt kött med vatten på heligt rum, och kläda sin egen kläder uppå, och gå derut, och göra sitt bränneoffer och folkens bränneoffer, och försona både sig och folket;
Anapaswa aoshe mwili wake kwa maji mahali patakatifu, na avae nguo zake za kawaida; pia lazima atoke nje kutoa sadaka ya kuteketezwa na sadaka ya kuteketezwa na sadaka ya kuteketezwa kwaajili ya wale watu, na kwa njia hii anafanya upatanisho kwaajili yake mwenyewe na kwaajili ya watu.
25 Och bränna upp det feta af syndoffret på altarena.
Lazima yeye achome mafuta ya sadaka ya dhambi juu ya madhabahu.
26 Men den, som förde fribocken ut, skall två sin kläder, och bada sitt kött med vatten, och sedan komma igen i lägret.
Huyu mtu anayemwacha mbuzi msingiziwa aende huru anafua nguo zake na kuosha mwili wake katika maji; baada ya hayo, anaweza kurudi tena kambini.
27 Syndoffrens stut och syndoffrens bock, hvilkas blod till försoning buret vardt in i helgedomen, skall man föra utom lägret, och uppbränna i elde, både deras hud, kött och träck.
Yule fahali kwaajili ya sadaka ya dhambi na mbuzi kwaajili ya sadaka za dhambi, ambaye damu yake ililetwa kufanya upatanisho katika mahali patakatifu, lazima ipelekwe nje ya kambi. kule lazima wachome, ngozi zao, nyama yao na kinyesi chao.
28 Och den som bränner det upp, han skall två sin kläder, och bada sitt kött med vatten, och sedan komma i lägret.
Huyu anayechoma sehemu hizo lazima afue nguo zake na aoge mwili wake katika maji; baada ya hapo, anaweza kurudi tena kwenye kambi.
29 Och skall detta vara eder en evig rätt: På tionde dagenom i sjunde månadenom skolen I späka edra kroppar, och ingen gerning göra, vare sig inländsk eller utländsk ibland eder;
Hii itakuwa sharti kwaajili yenu kwamba katika mwezi wa saba, kwenye siku ya kumi ya mwezi, mtanyenyekea wenyewe na msifanye kazi, iwe mwenyeji wa kuzaliwa au mgeni anayeishi kati yenu.
30 Förty på den dagen sker eder försoning, så att I varden rengjorde; ifrån alla edra synder varden I rengjorde för Herranom.
Hii ni kwasababu katika siku hii ya upatanisho utafanywa kwaajili yenu, kuwatakasa ninyi kutoka dhambi zenu zote ili mwe safi mbele za Yahwe.
31 Derföre skall det vara eder den störste Sabbath, och I skolen späka edra kroppar; en evig rätt vare det.
Hii ni maalumu kwa Sabato ya kupumzika kwaajili yenu, na lazima mnyenyekee wenyewe na msifanye kazi. Hili litakuwa sharti kati yenu.
32 Men den försoningen skall en Prest göra, den man vigt hafver, och hvilkens hand man fyllt hafver till en Prest i hans faders stad; och skall kläda på sig de linna kläder, som äro de helga kläden;
Kuhani mkuu, ambaye atapakwa mafuta na kuwekwa wakfu kuwa kuhani mkuu katika nafasi ya baba yake, lazima afanye upatanisho huu na kuvaa mavazi ya kitani, hayo ni mavazi matakatifu.
33 Och skall alltså försona den helga helgedomen, och vittnesbördsens tabernakel, och altaret, och Presterna, och allt folket af menighetene.
Lazima afanye upatanisho kwaajili ya mahali patakatifu sana; lazima afanye upatanisho kwaajili ya hema ya mkutano na madhabahu, na lazima afanye upatanisho kwaajili ya makuhani na kwaajili ya kusanyiko la watu.
34 Det skall vara eder en evig rätt, att I försonen Israels barn af alla deras synder, ena reso om året. Och Mose gjorde såsom Herren honom budit hade.
Hii daima itakuwa sharti kwaajili yako, kufanya upatanisho kwaajili ya watu wa Israeli kwasababu ya dhambi zao zote, mara moja kwa kila mwaka.” Na ilikuwa ikifanika kama Yahwe alivyomwamuru Musa.

< 3 Mosebok 16 >