< 3 Mosebok 12 >
1 Och Herren talade med Mose, och sade:
Bwana akamwambia Mose,
2 Tala med Israels barn, och säg: När en qvinna undfår säd, och föder piltabarn, då skall hon vara oren i sju dagar, så länge hon lider sina krankhet.
“Waambie Waisraeli: ‘Mwanamke ambaye atapata mimba na kuzaa mtoto wa kiume atakuwa najisi kwa kawaida ya ibada kwa siku saba, kama anavyokuwa najisi wakati wa siku zake za hedhi.
3 Och på åttonde dagen skall man omskära hans förhuds kött.
Mvulana atatahiriwa siku ya nane.
4 Och hon skall hemma blifva tre och trettio dagar uti hennes renselseblod. Intet heligt skall hon komma vid, och till helgedomen skall hon icke komma, till dess hennes renselsedagar äro ute.
Kisha ni lazima huyo mwanamke asubiri kwa siku thelathini na tatu, ndipo atakaswe kutoka damu kwake. Hataruhusiwa kugusa kitu chochote kilicho kitakatifu au kuingia mahali patakatifu, mpaka siku za kutakaswa kwake zimetimia.
5 Föder hon pigobarn, så skall hon vara oren i två veckor, så länge hon lider sina krankhet, och skall sex och sextio dagar hemma blifva i hennes renselseblod.
Kama akimzaa mtoto wa kike, mwanamke huyo atakuwa najisi kwa majuma mawili, kama wakati wake wa hedhi. Kisha atasubiri kwa siku sitini na sita, ndipo atatakaswa kutoka damu kwake.
6 Och när hennes renselsedagar äro ute, efter son eller dotter, skall hon bära fram ett årsgammalt lamb till bränneoffer, och en ung dufvo, eller turturdufvo, till syndoffer Prestenom, för dörrena af vittnesbördsens tabernakel.
“‘Siku zake za utakaso kwa ajili ya mwana au binti zitakapotimia, mwanamke huyo atamletea kuhani kwenye ingilio la Hema la Kukutania mwana-kondoo mwenye umri wa mwaka mmoja kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, na kinda la njiwa au hua kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
7 Der skall han offrat för Herranom, och försona henne, så varder hon ren af sinom blodgång. Detta är lagen för den som föder piltabarn eller pigobarn.
Atavitoa mbele za Bwana ili kufanya upatanisho kwa ajili yake, na kisha atakuwa safi kwa desturi ya ibada kutokana na kutokwa damu kwake. “‘Haya ndiyo masharti kwa ajili ya mwanamke atakayezaa mtoto wa kiume au wa kike.
8 Om hennes hand icke förmå ett får, så tage två turturdufvor, eller två unga dufvor, den ena till bränneoffer, den andra till syndoffer; så skall Presten försona henne, att hon skall varda ren.
Kama huyo mwanamke hana uwezo wa kumpata mwana-kondoo, ataleta hua wawili au makinda mawili ya njiwa, moja kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa na mwingine kwa ajili ya sadaka ya dhambi. Kwa njia hii, kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake, naye atakuwa safi.’”