< Josua 11 >
1 Då Jabin, Konungen i Hazor, detta hörde, sände han till Jobab, Konungen i Madon, och till Konungen i Achsaph,
Ikawa Yabini mfalme wa Hazori aliposikia habari za mambo haya, akatuma ujumbe kwa Yobabu mfalme wa Madoni, na kwa mfalme wa Shimroni, na kwa mfalme wa Akishafu,
2 Och till de Konungar, som bodde norrut uppå bergen, och uppå slättmarkene, söderut Cinneroth; och i dalarna, och i NaphotDor, utmed hafvet;
na pia kwa wafalme wa upande wa kaskazini wale waliokuwa milimani, katika Araba upande wa kusini mwa Kinerethi, kwenye shefela, upande wa magharibi na katika miinuko ya Nafoth-Dori upande wa magharibi;
3 Till de Cananeer österut och vesterut, till de Amoreer, Hetheer, Phereseer, och Jebuseer uppå bergen; så ock till de Heveer nedanför Hermons berg i Mizpa land.
kwa Wakanaani upande wa mashariki na magharibi; kwa Waamori, Wahiti, Waperizi na Wayebusi katika nchi ya vilima; na kwa Wahivi chini ya Hermoni katika eneo ya Mispa.
4 Desse drogo ut med alla deras härar, dråpeliga mycket folk, såsom sanden i hafsstrandene; och ganska många hästar och vagnar.
Wakaja na vikosi vyao vyote na hesabu kubwa ya farasi na magari ya kuvutwa na farasi, jeshi kubwa, kama wingi wa mchanga ulio pwani ya bahari.
5 Alle desse Konungar församlade sig, och kommo, och lägrade sig ihop vid det vattnet Merom, till att strida med Israel.
Wafalme hawa wote wakaunganisha majeshi yao na kupiga kambi pamoja kwenye Maji ya Meromu, ili kupigana dhidi ya Israeli.
6 Och Herren sade till Josua: Frukta dig intet för dem; ty i morgon på denna tiden skall jag gifva dem alla slagna för Israels barn; deras hästar skall du hasa, och bränna deras vagnar i eld.
Bwana akamwambia Yoshua, “Usiwaogope, kwa sababu kesho saa kama hii nitawatia wote mikononi mwa Israeli, wakiwa wameuawa. Utakata mishipa ya nyuma ya miguu ya farasi wao na kuyachoma moto magari yao ya vita.”
7 Och Josua kom hasteliga på dem, och allt krigsfolket med honom, vid vattnet Merom, och öfverföll dem.
Hivyo Yoshua pamoja na jeshi lake lote wakaja dhidi yao ghafula kwenye Maji ya Meromu kuwashambulia,
8 Och Herren gaf dem i Israels händer; och de slogo dem, och jagade dem allt intill det stora Zidon, och intill det varma vattnet; och intill slätten i Mizpe österut, och slogo dem tilldess icke en igenblef.
naye Bwana akawatia mikononi mwa Israeli. Wakawashinda na kuwafukuza hadi Sidoni Kuu na kuwafikisha Misrefoth-Maimu, hadi Bonde la Mispa upande wa mashariki, hadi pakawa hakuna yeyote aliyebaki.
9 Då gjorde Josua dem såsom Herren honom budit hade, och hasade deras hästar, och brände upp deras vagnar;
Yoshua akawatendea kama Bwana alivyoamuru. Akakata mishipa ya nyuma ya miguu ya farasi wao na kuchoma moto magari yao ya vita.
10 Och vände om på samma tiden, och vann Hazor, och slog dess Konung med svärd; ty Hazor var tillförene hufvudstaden för alla dessa Konungariken;
Wakati huo Yoshua akarudi na kuuteka mji wa Hazori na kumuua mfalme wake kwa upanga. (Hazori ulikuwa mji mkuu wa falme hizo zote.)
11 Och slog alla de själar, som derinne voro, med svärdsegg, och gaf dem tillspillo; och lät intet igenblifva, som anda hade; och brände upp Hazor med eld.
Kila aliyekuwa ndani yake wakamuua kwa upanga. Wakawaangamiza kabisa, wala hawakusaza chochote chenye pumzi na akauchoma Hazori kwenyewe kwa moto.
12 Dertill alla dessa Konungarnas städer vann Josua, med deras Konungar; och slog dem med svärdsegg, och gaf dem tillspillo, såsom Mose Herrans tjenare budit hade.
Yoshua akaiteka hii miji yote ya kifalme pamoja na wafalme wake na kuwapiga kwa upanga. Akawaangamiza kabisa wote, jinsi Mose mtumishi wa Bwana alivyowaagiza.
13 Dock uppbrände Israels barn inga städer med eld, som högt uppe lågo, förutan Hazor allena; det uppbrände Josua.
Lakini Israeli hawakuichoma moto hata mojawapo ya miji iliyojengwa katika vilima vyao vidogo isipokuwa mji wa Hazori ambao Yoshua aliuchoma moto.
14 Och allt rofvet af dessa städerna, och boskapen, bytte Israels barn emellan sig; men alla menniskor slogo de med svärdsegg, tilldess de förgjorde dem, och läto intet igenblifva, som anda hade.
Waisraeli wakajichukulia nyara zote na mifugo yote ya miji hii, bali waliwaua watu wote kwa upanga hadi walipowaangamiza kabisa, pasipo kumbakiza yeyote mwenye pumzi.
15 Såsom Herren sinom tjenare Mose, och Mose Josua budit hade, så gjorde Josua, att intet blef tillbaka af allt det Herren hade budit Mose.
Kama vile Bwana alivyomwagiza Mose mtumishi wake, vivyo hivyo Mose alimwagiza Yoshua, naye Yoshua akafanya kama vivyo, hakukosa kufanya lolote katika yale yote Bwana aliyomwagiza Mose.
16 Alltså intog Josua all denna landen på bergen, och allt det söderut ligger, och allt landet Gosen, och dalarna, och slättmarkena, och Israels berg med dess dalar;
Yoshua akaiteka nchi hii yote: nchi ya vilima, Negebu yote, eneo yote ya Gosheni, shefela ya upande wa magharibi, Araba na milima ya Israeli pamoja na shefela zao,
17 Allt ifrå berget, som åtskiljer landet uppåt emot Seir intill BaalGad, på bergsens Libanons slätt nedan vid Hermons berg; alla deras Konungar vann han, och slog dem, och drap dem.
kuanzia Mlima Halaki ambao umeinuka kuelekea Seiri hadi Baal-Gadi katika Bonde la Lebanoni chini ya Mlima Hermoni. Akawateka wafalme wake wote, akawapiga na kuwaua.
18 Men han förde örlig med dessa Konungarna i långan tid.
Yoshua akapigana vita dhidi ya wafalme hawa wote kwa muda mrefu.
19 Och var ingen stad, som sig gaf med frid under Israels barn, undantagna de Heveer, som bodde i Gibeon; utan de vunno dem alla med strid.
Hakuna mji wowote katika eneo hili uliofanya mkataba wa amani na Israeli, isipokuwa hao Wahivi wa Gibeoni. Wengine wote walishindwa katika vita.
20 Och det skedde så af Herranom, att deras hjerta vardt förstockadt, till att möta Israels barn med strid; på det de skulle tillspillo komma, och dem ingen nåd vederfaras, utan förgöras, såsom Herren hade budit Mose.
Kwa maana Bwana mwenyewe ndiye aliifanya mioyo yao iwe migumu, ili kupigana vita dhidi ya Israeli ili apate kuwafutilia mbali pasipo huruma, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
21 På den tiden kom Josua, och utrotade de Enakim utaf bergen af Hebron, af Debir, af Anab, af all Juda berg, och af all Israels berg, och gaf dem tillspillo med deras städer;
Wakati huo Yoshua akaenda kuwaangamiza Waanaki kutoka nchi ya vilima: kuanzia Hebroni, Debiri na Anabu, na kutoka nchi yote ya vilima ya Yuda na kutoka nchi yote ya vilima ya Israeli. Yoshua akawaangamiza kabisa pamoja na miji yao.
22 Och lät ingen Enakim igenblifva i Israels barnas land, förutan i Gasa, i Gath, och i Asdod; der blefvo de igen.
Hawakubaki Waanaki wowote katika nchi ya Israeli, ila tu katika nchi ya Gaza, Gathi na Ashdodi.
23 Alltså tog Josua allt landet in, alldeles såsom Herren hade sagt till Mose; och gaf det Israels barnom till arfs, hvarjo slägtene sin del. Och landet vände åter att strida.
Hivyo Yoshua akaiteka nchi hiyo yote kama vile Bwana alivyokuwa amemwagiza Mose, naye Yoshua akawapa Israeli kuwa urithi wao, kulingana na walivyogawanyika katika kabila zao. Ndipo nchi ikawa na amani bila vita.