< Jona 2 >
1 Och Jona bad till Herran sin Gud, i fiskens buk;
Akiwa ndani ya tumbo la nyangumi, Yona alimwomba Bwana Mungu wake.
2 Och han sade: Jag ropade till Herran i mine ångest, och han svarade mig; jag ropade utu helvetes buk, och du hörde mina röst. (Sheol )
Akasema: “Katika shida yangu nalimwita Bwana, naye akanijibu. Kutoka kina cha kaburi niliomba msaada, nawe ukasikiliza kilio changu. (Sheol )
3 Du kastade mig uti djupet, midt i hafvet, så att floderna kommo omkring mig; alle dine våger och böljor gingo öfver mig.
Ulinitupa kwenye kilindi, ndani kabisa ya moyo wa bahari, mikondo ya maji ilinizunguka, mawimbi yako yote na viwimbi vilipita juu yangu.
4 Jag tänkte, att jag bortkastad var ifrå din ögon; men jag skall ännu få se ditt helga tempel.
Nikasema, ‘Nimefukuziwa mbali na uso wako, hata hivyo nitatazama tena kuelekea Hekalu lako takatifu.’
5 Vattnen omhvärfde mig allt intill mitt lif; djupet omgrep mig, sjövassen öfvertäckte mitt hufvud.
Maji yaliyonimeza yalinitisha, kilindi kilinizunguka; mwani ulijisokota kichwani pangu.
6 Jag sönk neder till bergsgrunden, jorden hade beslutit mig med sina bommar evinnerliga; men du hafver fört mitt lif utu förderfvet, Herre min Gud.
Nilizama chini sana mpaka pande za mwisho za milima, makomeo ya hiyo nchi yalinifungia hata milele. Lakini uliuleta uhai wangu kutoka shimoni, Ee Bwana Mungu wangu.
7 Då min själ öfvergaf sig, tänkte jag uppå Herran, och min bön kom till dig, uti ditt helga tempel.
“Wakati uhai wangu ulipokuwa unatoka, nilikukumbuka wewe, Bwana, nayo maombi yangu yalikufikia wewe, katika Hekalu lako takatifu.
8 Men de som förlåta sig uppå sina gerningar, hvilka dock intet äro, de akta intet om nådena.
“Wale watu wanaongʼangʼana na sanamu zisizofaa hupoteza neema ile ambayo ingekuwa yao.
9 Men jag vill offra med tacksägelse. Min löfte vill jag betala Herranom, att han mig hulpit hafver.
Lakini mimi, kwa wimbo wa shukrani, nitakutolea dhabihu. Lile nililowekea nadhiri nitalitimiza. Wokovu watoka kwa Bwana.”
10 Och Herren sade till fisken, och han utsputade Jona in uppå landet.
Basi Bwana akamwamuru yule nyangumi, naye akamtapika Yona katika nchi kavu.