< Job 38 >

1 Och Herren svarade Job uti ett väder, och sade:
Kisha Bwana akamjibu Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli. Akasema:
2 Hvilken är den som i sina tankar så fela vill, och talar så med oförnuft?
“Nani huyu atiaye mashauri yangu giza kwa maneno yasiyo na maarifa?
3 Gjorda dina länder såsom en man; jag vill fråga dig: Säg, äst du så klok?
Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza swali, nawe unijibu.
4 Hvar vast du, då jag grundade jordena? Säg mig:
“Ulikuwa wapi nilipoweka misingi ya dunia? Niambie, kama unafahamu.
5 Vetst du, ho henne hafver satt sitt mått; eller ho hafver dragit något snöre öfver henne?
Ni nani aliyeweka alama vipimo vyake? Hakika wewe unajua! Ni nani aliyenyoosha kamba ya kupimia juu yake?
6 Eller hvaruppå står hennes fotafäste; eller ho hafver henne en hörnsten lagt;
Je, misingi yake iliwekwa juu ya nini, au ni nani aliyeweka jiwe la pembeni,
7 Då morgonstjernorna tillsammans lofvade mig, och all Guds barn fröjdade sig?
wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja, na malaika wote walipokuwa wakipiga kelele kwa furaha?
8 Ho hafver tillslutit hafvet med sina dörrar, då det utbrast såsom utu moderlifve;
“Ni nani aliyeifungia bahari milango ilipopasuka kutoka tumbo,
9 Då jag klädde det med skyar, och invefvade det i töckno, såsom i lindakläde;
nilipoyafanya mawingu kuwa vazi lake, na kuyafungia katika giza nene,
10 Då jag förtog thy dess flod med minom dam, och satte thy bom och dörrar före;
nilipoamuru mipaka yake, na kuiweka milango yake na makomeo mahali pake,
11 Och sade: Allt härintill skall du komma, och icke vidare; här skola dina stolta böljor sätta sig?
niliposema, ‘Unaweza kufika mpaka hapa wala si zaidi; hapa ndipo mawimbi yako yenye kiburi yatakapokomea’?
12 Hafver du i dinom tid budit morgonen, och vist morgonrodnanom sitt rum;
“Umepata kuiamrisha asubuhi ipambazuke, au kuyaonyesha mapambazuko mahali pake,
13 Att jordenes ändar måga fattade varda, och de ogudaktige der utskuddade blifva?
yapate kushika miisho ya dunia, na kuwakungʼuta waovu waliomo?
14 Inseglet skall sig förvandla såsom ler, så att de skola blifva såsom ett kläde;
Dunia hubadilika kama udongo wa mfinyanzi chini ya lakiri; sura yake hukaa kama ile ya vazi.
15 Och dem ogudaktigom skall deras ljus förtaget varda, och de högfärdigas arm skall sönderbruten varda.
Waovu huzuiliwa nuru yao, nao mkono wao ulioinuliwa huvunjwa.
16 Hafver du kommit uti hafsens grund, och vandrat uti djupsens fjät?
“Je, umepata kufika kwenye chemchemi za bahari? Au kutembea mahali pa ndani pa vilindi?
17 Hafva dödsens dörrar någon tid upplåtit sig för dig; eller hafver du sett dörrarna åt mörkret?
Umewahi kuonyeshwa malango ya mauti? Umewahi kuiona milango ya uvuli wa mauti?
18 Hafver du förnummit huru bred jorden är? Låt höra, vetst du allt detta?
Je, wewe unafahamu ukubwa wa dunia? Niambie kama unajua haya yote.
19 Hvilken är vägen dit, der ljuset bor, och hvilket är mörkrens rum;
“Njia ya kufika kwenye makao ya nuru ni ipi? Nako maskani mwa giza ni wapi?
20 Att du måtte aftaga dess gränso, och märka stigen till dess hus?
Je, unaweza kuvirudisha kwenye makao yake? Unajua njia za kufika maskani mwake?
21 Visste du, att du skulle på den tiden född varda, och huru många dina dagar blifva skulle?
Hakika unajua, kwa kuwa ulikuwa umeshazaliwa! Kwani umeishi miaka mingi!
22 Hafver du der varit, dädan snön kommer; eller hafver du sett, hvadan haglet kommer;
“Je, umeshawahi kuingia katika ghala za theluji, au kuona ghala za mvua ya mawe,
23 Hvilka jag bevarat hafver intill bedröfvelsens dag, intill stridenes och örligets dag?
ambazo nimeziweka akiba kwa ajili ya wakati wa taabu, na kwa ajili ya wakati wa vita na mapigano?
24 Genom hvilken vägen delar sig ljuset, och östanväder uppkommer på jordena?
Ni ipi njia iendayo mahali umeme wa radi unapotawanyiwa, au mahali upepo wa mashariki unaposambaziwa juu ya dunia?
25 Ho hafver utskift regnskurene sitt lopp, och ljungeldenom och dundrena vägen;
Ni nani aliyepasua mifereji kwa ajili ya maji mengi ya mvua yaendayo kasi na njia ya umeme wa radi,
26 Så att det regnar uppå jordena, der ingen är, i öknene, der ingen menniska är;
ili kusababisha mvua kunyeshea mahali pasipokaliwa na mtu, jangwa lisilo na yeyote ndani yake,
27 Att det skall uppfylla ödemarken och öknen, och kommer gräset till att växa?
ili kuitosheleza nchi ya ukiwa na jangwa, na majani yaanze kumea ndani yake?
28 Ho är regnets fader? Ho hafver födt daggenes droppar?
Je, mvua ina baba? Ni nani baba azaaye matone ya umande?
29 Utu hvars lif är isen utgången; och ho hafver födt rimfrostet under himmelen;
Barafu inatoka tumbo la nani? Ni nani azaaye ukungu kutoka mbinguni,
30 Att vattnet skulle fördoldt varda såsom under stenar, och djupet blifver ofvanuppå ståndandes?
wakati maji yawapo magumu kama jiwe, wakati uso wa vilindi vya maji unapoganda?
31 Kan du binda tillsammans sjustjärnornas band, eller upplösa Orions band?
“Je, waweza kuufunga mnyororo wa Kilimia? Waweza kulegeza kamba za Orioni?
32 Kan du hemta morgonstjernorna fram i sin tid, eller föra vagnen på himmelen öfver sin barn?
Waweza kuyaongoza makundi ya nyota kwa majira yake, au kuongoza Dubu na watoto wake?
33 Vetst du, huru himmelen skall regeras; eller kan du sätta ett herradöme öfver honom på jordene?
Je, unajua sheria zinazotawala mbingu? Waweza kuweka utawala wa Mungu duniani?
34 Kan du föra dina dunder högt uppe i skynom, att vattnens myckenhet dig öfvertäcker?
“Waweza kuiinua sauti yako mpaka mawinguni, na kujifunika mwenyewe na gharika ya maji?
35 Kan du utsläppa ljungeldar, att de fara åstad, och säga: Här äre vi?
Je, wewe hutuma umeme wa radi kwenye njia zake? Je, hutoa taarifa kwako kukuambia, ‘Sisi tuko hapa’?
36 Ho hafver satt visdomen uti det fördolda? Ho hafver gifvit tankomen förstånd?
Ni nani aliyeujalia moyo hekima au kuzipa akili ufahamu?
37 Ho är så vis, att han skyarna räkna kan? Ho kan förstoppa vattuläglarna i himmelen,
Nani mwenye hekima ya kuyahesabu mawingu? Ni nani awezaye kuinamisha magudulia ya mbinguni
38 När stoftet är vått vordet, så att det tillhopalöper, och klimparne låda tillsammans?
wakati mavumbi yawapo magumu, na mabonge ya udongo kushikamana pamoja?
39 Kan du gifva lejinnone hennes rof i jagtene; och mätta de unga lejonen;
“Je, utamwindia simba jike mawindo, na kuwashibisha simba wenye njaa
40 Så att de lägga sig uti sitt rum, och stilla ligga i kulone på vakt?
wakati wao wamejikunyata mapangoni mwao, au wakivizia kichakani?
41 Ho reder korpenom mat, när hans ungar ropa till Gud, och veta icke hvar deras mat är?
Ni nani ampaye kunguru chakula wakati makinda yake yanamlilia Mungu, yakizungukazunguka kwa ajili ya kukosa chakula?

< Job 38 >