< 1 Mosebok 40 >
1 Och det begaf sig derefter, att Konungens i Egypten höfvitsman öfver skänkerna, och höfvitsmannen öfver bakarena, bröto deras herra Konungenom i Egypten emot.
Baada ya muda, mnyweshaji na mwokaji wa mfalme wa Misri, wakamkosea bwana wao, mfalme wa Misri.
2 Och Pharao vardt vred uppå dem,
Farao akawakasirikia hawa maafisa wake wawili, mnyweshaji mkuu na mwokaji mkuu,
3 Och lät sätta dem i hofmästarens hus i fängelse, der Joseph låg fången.
akawaweka chini ya ulinzi katika nyumba ya mkuu wa kikosi cha ulinzi katika gereza lile lile alimofungwa Yosefu.
4 Och hofmästaren satte Joseph öfver dem, att han skulle tjena dem; och de såto några dagar.
Mkuu wa kikosi cha ulinzi akawakabidhi kwa Yosefu, naye akawahudumia. Walipokuwa wamekaa chini ya ulinzi kwa muda,
5 Och både skänken och bakaren drömde om ena natt hvar sin dröm, och hvars deras dröm hade sin uttydelse.
kila mmoja wa hao wawili waliokuwa wamewekwa gerezani, yaani mnyweshaji na mwokaji wa mfalme wa Misri, waliota ndoto usiku mmoja, na kila ndoto ilikuwa na maana yake tofauti.
6 Då nu Joseph kom om morgonen in till dem, och såg dem ångse,
Yosefu alipowajia asubuhi yake, akawaona kwamba walikuwa na huzuni.
7 Frågade han dem, och sade: Hvi ären I så ångse i dag?
Ndipo Yosefu akawauliza maafisa hao wa Farao waliokuwa chini ya ulinzi pamoja naye nyumbani mwa bwana wake, akasema, “Mbona nyuso zenu zimejaa huzuni leo?”
8 De svarade: Oss hafver drömt, och vi hafvom ingen, som oss det utlägger. Joseph sade: Utläggningen hörer Gudi till; dock förtäljer mig det.
Wakamjibu, “Sisi sote tuliota ndoto, lakini hapakuwa na mtu yeyote wa kuzifasiri.” Ndipo Yosefu akawaambia, “Je, kufasiri ndoto si kazi ya Mungu? Niambieni ndoto zenu.”
9 Då förtäljde skänken sin dröm för Joseph, och sade till honom: Mig drömde, att ett vinträ var för mig:
Basi mkuu wa wanyweshaji akamweleza Yosefu ndoto yake. Akamwambia, “Katika ndoto yangu niliona mzabibu mbele yangu,
10 Det hade tre grenar; det grönskades, växte och blomstrades, och dess drufvor vordo mogna:
nao mzabibu ulikuwa na matawi matatu. Mara tu ulipoanza kuchipua, maua yalichanua na vishada vyake vikawa zabibu zilizoiva.
11 Och jag hade Pharaos skänkekar i mine hand, och tog och kryste dem i skänkekaret, och fick Pharao skänkekaret i handena.
Kikombe cha Farao kilikuwa mkononi mwangu, nikazitwaa zabibu, nikazikamua katika kikombe cha Farao, na nikaweka kikombe mkononi mwake.”
12 Joseph sade: Detta är uttydningen: Tre grenar äro tre dagar.
Yosefu akamwambia, “Hii ndiyo maana yake: Matawi matatu ni siku tatu.
13 Efter tre dagar skall Pharao upphäfva ditt hufvud, och sätta dig åter till dit ämbete, att du får honom skänkekaret i hans hand, såsom tillförene, då du var hans skänk.
Katika siku hizi tatu, Farao atakutoa gerezani na kukuweka tena kwenye nafasi yako, nawe utaweka kikombe cha Farao mikononi mwake, kama vile ulivyokuwa unafanya ulipokuwa mnyweshaji wake.
14 Men tänk uppå mig, då dig går väl, och gör barmhertighet med mig, att du Pharao ingifver, att han tager mig utaf detta huset;
Lakini wakati mambo yatakapokuwia mazuri, unikumbuke, unifanyie wema, useme mema juu yangu kwa Farao ili niondoke huku gerezani.
15 Ty jag är hemliga bortstulen utaf de Ebreers lande: Så hafver jag ock här intet gjort, att de mig insatt hafva.
Kwa maana nilichukuliwa kwa nguvu kutoka nchi ya Waebrania, na hata hapa nilipo sikufanya lolote linalostahili niwekwe gerezani.”
16 Då bakaren såg, att uttydningen var god, sade han till Joseph: Mig hafver ock drömt, att jag bar tre flätade korgar på mitt hufvud;
Yule mwokaji mkuu alipoona kuwa Yosefu amefasiri ikiwa na maana nzuri, akamwambia Yosefu, “Mimi pia niliota ndoto: Kichwani mwangu kulikuwepo vikapu vitatu vya mikate.
17 Och i öfversta korgenom allahanda bakad mat till Pharaos behof; och foglarne åto af korgenom på mitt hufvud.
Katika kikapu cha juu kulikuwa na aina zote za vyakula vilivyookwa kwa ajili ya Farao, lakini ndege walikuwa wakivila kutoka kwenye kikapu nilichokuwa nimebeba kichwani.”
18 Joseph svarade, och sade: Detta är uttydningen: Tre korgar äro tre dagar.
Yosefu akamwambia, “Hii ndiyo maana yake: Vikapu vitatu ni siku tatu.
19 Och efter tre dagar skall Pharao upphäfva ditt hufvud, och hänga dig i en galga; och foglarne skola äta ditt kött på dig.
Katika siku hizi tatu, Farao atakata kichwa chako na kukutundika juu ya mti. Nao ndege watakula nyama ya mwili wako.”
20 Och det hände tredje dagen, då begick Pharao sin årsdag, och han gjorde alla sina tjenare ena måltid: Och upphof den öfversta skänkens hufvud, och den öfversta bakarens, ibland sina tjenare;
Mnamo siku ya tatu, ilikuwa kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Farao, naye akawaandalia maafisa wake wote karamu. Akawatoa gerezani mnyweshaji mkuu na mwokaji mkuu, akawaweka mbele ya maafisa wake:
21 Och satte den öfversta skänken åter till sitt skänkeämbete, att han skulle få Pharao skänkekaret i handena;
Ndipo akamrudisha mnyweshaji mkuu kwenye nafasi yake, ili aweke kikombe mikononi mwa Farao tena,
22 Men den öfversta bakaren lät han hänga; som Joseph hade uttydt honom.
lakini akamwangika yule mwokaji mkuu, sawasawa na jinsi Yosefu alivyowaambia katika tafsiri yake.
23 Men den öfverste skänken tänkte intet på Joseph, utan förgat honom.
Pamoja na hayo, mnyweshaji mkuu hakumkumbuka Yosefu, bali alimsahau.