< Hesekiel 46 >
1 Detta säger Herren Herren: Den porten på inra gården, som österut ligger, skall i de sex söknadagar tillsluten vara; men om Sabbathsdagen, och i nymånadenom, skall man upplåta honom.
“‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Lango la ukumbi wa ndani linaloelekea upande wa mashariki litakuwa linafungwa kwa siku sita za juma, ila siku ya Sabato na siku ya Mwezi Mwandamo litafunguliwa.
2 Och Försten skall träda utantill under portens förhus, och blifva ståndandes utantill vid porten afsides; och Presterna skola offra hans bränneoffer och tackoffer; men han skall tillbedja vid portens tröskel, och sedan gå ut igen; men porten skall öppen blifva, allt intill aftonen.
Mkuu anayetawala ataingia kupitia baraza ya njia ya lango la ukumbi na kusimama karibu na nguzo ya lango. Makuhani watatoa sadaka za mkuu anayetawala za kuteketezwa na sadaka za amani. Mkuu anayetawala atasujudu kwenye kizingiti cha njia ya lango, kisha atatoka nje, lakini lango halitafungwa mpaka jioni.
3 Sammalunda ock folket i landena skola tillbedja för Herranom, i dörrene åt samma port, på Sabbatherna och nymånaderna.
Siku za Sabato na za Mwezi mwandamo watu wote wa nchi wataabudu mbele za Bwana penye lile ingilio la ile njia.
4 Men bränneoffret, som Försten för Herranom offra skall, på Sabbathsdagenom, skall vara sex lamb, de utan vank äro, och en vädur utan vank;
Sadaka ya kuteketezwa aletazo mkuu anayetawala kwa Bwana siku ya Sabato itakuwa ni wana-kondoo sita na kondoo dume mmoja, wote wasiwe na dosari.
5 Och ju ett epha till väduren, till spisoffer men till lamben, så myckt som han förmår, till spisoffer, och ju ett hin oljo till ett epha.
Sadaka ya nafaka inayotolewa pamoja na huyo kondoo dume itakuwa efa moja na sadaka ya nafaka inayotolewa na hao wana-kondoo itakuwa kiasi apendacho mtu pamoja na hini ya mafuta kwa kila efa.
6 Men i nymånadenom skall man offra en ung oxa, den utan vank är, och sex lamb, och en vädur utan vank;
Siku ya mwezi mwandamo atatoa fahali mchanga, wana-kondoo sita na kondoo dume, wote wasiwe na dosari.
7 Och ju ett epha till oxan, och ett epha till väduren, till spisoffer; men till lamben så mång epha som han förmår, och ju ett hin oljo till ett epha.
Atatoa kuwa sadaka ya nafaka efa moja pamoja na fahali mmoja, efa moja na kondoo dume mmoja na pamoja na wana-kondoo kama atakavyo kutoa, pamoja na hini ya mafuta kwa kila efa.
8 Och när Försten går derin, så skall han gå in genom portens förhus, och åter gå der ut igen.
Wakati mkuu anayetawala aingiapo, atapitia kwenye baraza ya njia ya lango, naye atatoka nje kwa njia hiyo hiyo.
9 Men folket i landena, som för Herran kommer på de stora högtider, och ingår genom den porten norrut till att tillbedja, det skall åter utgå genom den porten sunnantill; och de som ingå genom den porten sunnantill, de skola utgå genom den porten nordantill; och skola icke gå ut igen genom porten, der de igenom ingångne äro, utan gå rätt framåt ut.
“‘Wakati watu wa nchi wanapokuja mbele za Bwana katika sikukuu zilizoamriwa, yeyote aingiaye kwa lango la kaskazini kuabudu atatoka nje kwa lango la kusini na yeyote aingiaye kwa lango la kusini atatoka nje kwa lango la kaskazini. Hakuna mtu yeyote atakayerudi kwa kupitia lango lile aliloingilia, lakini kila mmoja atatoka nje kwa lango linalokabili lile aliloingilia.
10 Men Försten skall både ingå och utgå med dem.
Mkuu anayetawala atakuwa miongoni mwao, akiingia nao ndani wanapoingia, naye atatoka nao nje wanapotoka.
11 Och på helgadagomen, och högtidomen, skall man offra till spisoffer, ju till en stut ett epha, och ju till en vädur ett epha, och till lamben så mycket en förmår, och ju ett hin oljo till ett epha.
“‘Kwenye sikukuu na kwenye sikukuu zilizoamriwa, sadaka ya nafaka itakuwa efa moja pamoja na fahali mmoja, efa moja pamoja na kondoo dume mmoja, pamoja na idadi ya wana-kondoo kama mtu apendavyo kutoa, pamoja na hini ya mafuta kwa kila efa.
12 Men då Försten vill göra ett friviljogt bränneoffer eller tackoffer Herranom, så skall man upplåta honom den porten östantill, att han må offra sitt bränneoffer och tackoffer, lika som han det eljest på Sabbathen offra plägar; och när han går åter ut, så skall man sluta porten igen efter honom.
Mkuu anayetawala anapotoa sadaka ya hiari kwa Bwana, ikiwa ni sadaka ya kuteketezwa au sadaka ya amani, lango linaloelekea mashariki litafunguliwa kwa ajili yake. Atatoa sadaka yake ya kuteketezwa au sadaka yake ya amani kama afanyavyo katika siku ya Sabato. Kisha atatoka nje, naye akiisha kutoka nje, lango litafungwa.
13 Och han skall göra Herranom dagliga ett bränneoffer, nämlige ett årsgammalt lamb utan vank; det samma skall han offra hvar morgon;
“‘Kila siku utamtoa mwana-kondoo wa mwaka mmoja asiyekuwa na dosari kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana, utaitoa kila siku asubuhi.
14 Och skall hvar morgon lägga deruppå sjettedelen af ett epha till spisoffer, och tredjedelen af ett hin oljo, beblandadt med semlomjöl, till spisoffer Herranom. Det skall vara en evig rätt om det dagliga offret.
Pia kila siku asubuhi pamoja na hiyo sadaka utatoa sadaka ya nafaka, ikiwa na sehemu ya sita ya efa pamoja na theluthi moja ya hini ya mafuta ya kuchanganya na ule unga. Utoaji wa sadaka hii ya nafaka kwa Bwana ni amri ya daima.
15 Och alltså skola de offra lambet, samt med spisoffrena och oljone, hvar morgon till ett dagligit bränneoffer.
Kwa hiyo mwana-kondoo na sadaka ya nafaka na mafuta vitatolewa kila siku asubuhi kwa ajili ya sadaka ya daima ya kuteketezwa.
16 Detta säger Herren Herren: När Försten gifver enom sinom son en skänk af sitt arf, det samma skall höra hans sönom till, och de skola besitta det för ett arf.
“‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ikiwa mkuu atawalaye atatoa zawadi kutoka kwenye urithi wake na kumpa mmoja wa wanawe, hiyo zawadi itakuwa pia kwa wazao wake, itakuwa mali yao kwa urithi.
17 Men om han något skänker enom af sina tjenare af sitt arf, det skola de besitta allt intill friåret, och sedan skall det falla intill Förstan igen; ty hans del skall allena komma hans söner till.
Hata hivyo, kama atatoa zawadi kutoka urithi wake na kumpa mmoja wa watumishi wake, mtumishi anaweza kuiweka mpaka mwaka wa uhuru, kisha itarudishwa kwa mkuu anayetawala. Urithi wake ni wa wanawe peke yao, ni mali yao.
18 Och skall Försten intet taga ifrå sino folke af deras arfvedel, eller drifva dem ifrå deras ägor; utan skall låta sinom barnom sina egna ägor; på det att hvar slägten må vid sig blifva åtskiljeliga, och hvar behålla det honom tillhörer.
Mkuu anayetawala hana ruhusa kuchukua urithi wowote wa watu na kuwaondoa kwenye mali zao. Mkuu atawalaye atawapa wanawe urithi wao, kutoka kwenye mali zake mwenyewe, ili kwamba pasiwe na mtu wangu yeyote atakayetengwa na urithi wake.’”
19 Och han hade mig in i ingången vid sidon åt porten nordantill, till helgedomens kamrar, hvilke Prestomen tillhörde; och si, der var ett rum uti ett hörn vesterut.
Kisha mtu yule akanileta kwa kupitia kwenye ingilio lililokuwa kando ya lango mpaka kwenye vyumba vitakatifu vinavyoelekea kaskazini, ambavyo ni vya makuhani, naye akanionyesha mahali fulani upande wa mwisho wa magharibi.
20 Och han sade till mig: Detta är det rummet, der Presterna skuldoffer och syndoffer koka skola, och baka spisoffer, att de icke skola behöfva bära det ut i yttra gården; på det folket icke skall synda på det helga.
Akaniambia, “Mahali hapa ndipo makuhani watakapotokosea sadaka ya hatia na sadaka ya dhambi na kuoka sadaka ya nafaka, kuepuka kuzileta katika ukumbi wa nje na kushirikisha utakatifu kwa watu.”
21 Sedan hade han mig ut i den yttra gården, och befallde mig gå uti gårdsens fyra hörn; och si, der var ett rum uti hvart gårdsens hörn.
Baada ya hapo akanileta kwenye ukumbi wa nje na kunizungusha kwenye pembe zake nne, nami nikaona katika kila pembe ya huo ukumbi kulikuwa na ukumbi mwingine.
22 Och i de fyra gårdsens hörn voro rum till att röka, fyratio alnar långa och tretio alnar breda, ju den ene så vid som den andre.
Katika pembe nne za huo ukumbi wa nje kulikuwa na kumbi nyingine, zenye urefu wa dhiraa arobaini na upana wake dhiraa thelathini, ambapo hizo kumbi kwenye hizo pembe nne zilikuwa na vipimo vilivyo sawa.
23 Och der gick en liten mur om dem alla fyra; der voro eldstäder gjorde nedre utmed muren allt omkring.
Mzunguko wa ndani wa hizo kumbi nne ulikuwa na ukingo wa jiwe, zikiwa na sehemu zilizojengwa kwa ajili ya moto kuzunguka chini ya huo ukingo.
24 Och han sade till mig: Detta år kokorummet, der tjenarena i husens uti koka skola det som folket offrar.
Akaniambia, “Hizi ndizo sehemu za kupikia ambazo wale wanaohudumu kwenye Hekalu watatokosea dhabihu za watu.”