< 2 Mosebok 37 >
1 Och Bezaleel gjorde arken af furoträ, halftredje aln lång, halfannor aln bred och hög;
Bezaleli akatengeneza Sanduku la mbao za mshita: urefu wake ulikuwa dhiraa mbili na nusu, upana wake dhiraa moja na nusu, na kimo chake dhiraa moja na nusu.
2 Och öfverdrog honom med klart guld innan och utan; och gjorde honom en gyldene krans omkring;
Akalifunika kwa dhahabu safi ndani na nje, na kulizungushia ukingo wa dhahabu.
3 Och göt fyra gyldene ringar till hans fyra hörner; på hvarje sidone två;
Akasubu pete nne za dhahabu na kuzifungia kwenye miguu yake minne, pete mbili kwa upande mmoja na pete mbili kwa upande mwingine.
4 Och gjorde stänger af furoträ, och öfverdrog dem med guld;
Kisha akatengeneza mipiko ya mti wa mshita na kuzifunika kwa dhahabu.
5 Och satte dem uti ringarna på sidone af arken, så att man kunde bära honom.
Akaiingiza hiyo mipiko kwenye zile pete katika pande mbili za Sanduku ili kulibeba.
6 Och han gjorde nådastolen af klart guld, halftredje aln lång, och halfannor aln bred;
Akatengeneza kifuniko cha upatanisho kwa dhahabu safi: urefu wake ulikuwa dhiraa mbili na nusu, na upana wake dhiraa moja na nusu.
7 Och gjorde två Cherubim af tätt guld, på båda ändarna af nådastolenom;
Kisha akatengeneza makerubi wawili wa dhahabu iliyofuliwa katika miisho ya hicho kifuniko.
8 En Cherub på denna ändan; en annan på den andra ändan.
Akatengeneza kerubi mmoja kwenye mwisho mmoja, na kerubi mwingine kwenye mwisho mwingine; akawatengeneza kuwa kitu kimoja na hicho kifuniko katika miisho hiyo miwili.
9 Och de Cherubim uträckte sina vingar ofvan öfver, och öfverskylde dermed nådastolen, och deras anlete stodo tvärtemot hvarsannars; och sågo på nådastolen.
Makerubi hao walikuwa wametandaza mabawa kuelekea juu, wakitia kivuli hicho kifuniko. Makerubi hao walielekeana, wakitazama hicho kifuniko.
10 Och han gjorde bordet af furoträ, två alnar långt, en aln bredt, och halfannor aln högt;
Akatengeneza meza ya mbao za mshita yenye urefu wa dhiraa mbili, upana wa dhiraa moja, na kimo cha dhiraa moja na nusu.
11 Och öfverdrog det med klart guld, och gjorde der en gyldene krans omkring.
Kisha akaifunika kwa dhahabu safi, na kuitengenezea ukingo wa dhahabu kuizunguka pande zote.
12 Och gjorde der ena listo omkring; ena hand bredt hög, och gjorde en gyldene krans omkring listona;
Pia akatengeneza upapi wenye upana wa nyanda nne, na kuufanyia ule upapi ukingo wa dhahabu kuuzunguka pande zote.
13 Och göt dertill fyra gyldene ringar; och satte dem på de fyra hörnen uppå dess fyra fötter;
Akasubu pete nne za dhahabu kwa ajili ya meza hiyo, na kuzifungia kwenye pembe nne, pale penye miguu yake minne.
14 Hardt under listone, så att stängerna voro deruti, der man bordet med bar;
Pete hizo ziliwekwa karibu na ukingo ule ili kuishikilia ile mipiko iliyotumika kuibebea hiyo meza.
15 Och gjorde stängerna af furoträ, och öfverdrog dem med guld, att man skulle bära bordet dermed;
Mipiko hiyo ya kubebea meza ilitengenezwa kwa mti wa mshita, na ilikuwa imefunikwa kwa dhahabu.
16 Och gjorde desslikes, af klart guld, redskapen på bordet, fat, skedar, kannor och skålar, der man med ut och in skänkte;
Vyombo vyote vya mezani vilitengenezwa kwa dhahabu safi: yaani sahani zake, masinia, na bakuli na bilauri zake kwa ajili ya kumiminia sadaka za vinywaji.
17 Och gjorde ljusastakan af klart tätt guld; derpå voro läggen, rör, skålar, knöpar och blommor;
Akatengeneza kinara cha taa cha dhahabu safi iliyofuliwa vizuri katika kitako chake na ufito wake; vikombe vyake vilivyofanana na ua, matovu na maua vilikuwa kitu kimoja.
18 Sex rör gingo ut af sidorna, på hvarjo sidone tre rör;
Matawi sita yalitokeza kuanzia ule ufito wa katikati wa kinara cha taa: matawi matatu upande mmoja na matatu upande mwingine.
19 Tre skålar, såsom mandelnötter, voro på hvar rör, med knöpar och blommor;
Vikombe vitatu vya mfano wa maua ya mlozi yenye matovu na maua vilikuwa katika tawi moja, vikombe vitatu katika tawi jingine, na vivyo hivyo kwa matawi yote sita yaliyotokeza kwenye kile kinara cha taa.
20 Men på ljusastakanom voro fyra skålar med knöpar och blommor;
Juu ya kinara chenyewe kulikuwepo na vikombe vinne vya mfano wa maua ya mlozi yakiwa na matovu yake na maua yake.
21 Inunder två rör en knöp, så att sex rör gingo ut af honom;
Tovu moja lilikuwa chini ya jozi ya kwanza ya matawi yaliyotokeza kwenye kinara cha taa, tovu la pili chini ya jozi ya pili, nalo tovu la tatu chini ya jozi ya tatu, yaani, matawi sita kwa jumla.
22 Och hans knöpar och rör deruppå; och var allt klart tätt guld;
Matovu na matawi yote yalikuwa kitu kimoja na kile kinara cha taa, yakiwa yamefuliwa kwa dhahabu safi.
23 Och gjorde de sju lampor, med deras ljusanäpor och släcketyg, af klart guld.
Akatengeneza taa zake saba, na pia mikasi ya kusawazishia tambi, pamoja na masinia, zote kwa dhahabu safi.
24 Af en centner guld gjorde han honom, och all hans tyg.
Akatengeneza kinara hicho cha taa pamoja na vifaa vyake vyote kutumia talanta moja ya dhahabu safi.
25 Han gjorde ock rökaltaret af furoträ, en aln långt och bredt, rätt fyrakant, och två alnar högt med sin horn;
Akatengeneza madhabahu ya kufukizia uvumba kwa mbao za mshita. Ilikuwa ya mraba, urefu na upana wake dhiraa moja, na kimo cha dhiraa mbili, nazo pembe zake zilikuwa kitu kimoja nayo.
26 Och öfverdrog det med klart guld, dess tak och väggar allt omkring, och dess horn, och gjorde der en krans omkring af klart guld;
Akafunika hayo madhabahu juu na pande zote na pia zile pembe zake kwa dhahabu safi, na akayafanyizia ukingo wa dhahabu kuizunguka.
27 Och två gyldene ringar under kransen på båda sidor, så att man satte stängerna deruti, och bar det dermed.
Akatengeneza pete mbili za dhahabu kwa ajili ya madhabahu chini ya huo ukingo, zikiwa mbili kila upande, za kushikilia hiyo mipiko iliyotumika kuyabebea madhabahu.
28 Men stängerna gjorde han af furoträ, och öfverdrog dem med guld;
Akatengeneza mipiko kwa miti ya mshita na kuifunika kwa dhahabu.
29 Och gjorde den helga smörjooljan, och rökverk af rent speceri, efter apothekarekonst.
Pia akatengeneza mafuta matakatifu ya upako, na uvumba safi wenye harufu nzuri, kazi ya mtengeneza manukato.