< 2 Mosebok 29 >

1 Detta måste du ock göra dem, att de skola varda mig vigde till Prester. Tag en ungan stut, och två vädrar utan vank;
Sasa Hivi ndivyo wapaswa kufanya kuwatenga ili wanitumikie kama makuhani. Chukuwa mtoto wa ng'ombe dume na kondoo bila lawama,
2 Osyradt bröd och osyrade kakor, blandade med oljo, och osyrade tunnkakor, smorda med oljo; af hvetemjöl skall du allt görat;
mkate bila hamira, na keki bila hamira iliyo changanywa na mafuta. Pia chukuwa maandazi bila hamira yalio pakwa mafuta. Fanya maandazi kwa unga mzuri wa ngano.
3 Och skall läggat uti en korg, och uti korgenom bära det fram, samt med stutenom, och de två vädrarna.
Lazima uweke kwenye ndoo moja, leta kwenye ndoo, na kuleta pamoja na ng'ombe dume na wana kondoo wawili.
4 Och du skall hafva Aaron och hans söner fram för dörrena af vittnesbördsens tabernakel, och två dem med vatten;
Lazima nawe umlete Aruni na wana wake wawili katika lango la kuingilia hema la kukutania. Lazima uwasafishe Aruni na wana wake kwenye maji.
5 Och taga kläden, och kläda uppå Aaron den trånga kjortelen, och den silkeskjortelen, och lifkjortelen, och skölden till lifkjortelen, och skall begjorda honom utanuppå lifkjortelen;
Kisha twaa hayo mavazi na kumvika Haruni; itie kanzu, na joho ya naivera, na naivera, na kifuko cha kifuani, na kumkaza kwa huo mshipi wa naivera uliosukwa kwa ustadi.
6 Och sätta hatten uppå hans hufvud, och den helga kronona uppå hatten;
Nawe mvike kile kilemba kichwani, na ile taji takatifu utaitia katika kile kilemba.
7 Och skall taga smörjoolja, och gjuta uppå hans hufvud, och smörja honom.
Ndipo utakapotwaa hayo mafuta ya kutiwa, na kummiminia kichwani mwake, na kumtia mafuta.
8 Och hans söner skall du ock hafva fram, och kläda uppå dem den trånga kjortelen;
Kisha walete hao wanawe na kuwavika kanzu.
9 Och begjorda både Aaron och dem med bälter, och binda hufvorna på dem, att de skola hafva Presterskapet till ett evigt sätt. Och du skall fylla händerna uppå Aaron och hans söner;
Nawe uwakaze mishipi, Aruni na wanawe, na kuwavika kofia. Nao watakuwa na huo ukuhani kwa amri ya milele. Nawe utawaweka Haruni na wanawe kwa kazi takatifu.
10 Och skall hafva stuten fram för dörrena af vittnesbördsens tabernakel. Och Aaron med hans söner skola lägga sina händer på hufvudet af stutenom.
Kisha utamleta huyo ng’ombe mbele ya hema ya kukutania; na Haruni na wanawe wataweka mikono yao juu ya kichwa cha huyo ng’ombe.
11 Och du skall slagta stuten för Herranom, inför dörrena af vittnesbördsens tabernakel;
Kisha utamchinja huyo ng’ombe mbele ya Yahweh pa hema ya kukutania. BWANA,
12 Och skall taga af hans blod, och stryka uppå altarens horn med ditt finger, och allt det andra blodet kasta neder på bottnen till altaret;
Kisha twaa baadhi ya damu ya ng’ombe, uitie katika pembe za madhabahu kwa kidole chako; na kuimimina damu yote chini ya madhabahu.
13 Och skall taga allt det feta, som är på tarmarna, och det nätet öfver lefrena, och båda njurarna, med det feta som deruppå är, och skall bränna det upp på altarena.
Kisha chukuwa mafuta yote yafunikayo matumbo, na kitambi kilicho katika ini, na figo mbili, na mafuta yaliyo juu yake, uyateketeze yote juu ya madhabahu.
14 Men stutens kött, hudena och gåret, skall du uppbränna med eld utanför lägret; ty det är ett syndoffer.
Lakini nyama yake huyo ng’ombe, na ngozi yake, na mavi yake, utayachoma kwa moto nje ya marago; ni sadaka kwa ajili ya dhambi.
15 Men den ena väduren skall du taga; och Aaron med hans söner skola lägga deras händer på hans hufvud.
Pia mtwae kondoo mume mmoja; na Aruni na wanawe wataweka mikono yao juu ya kichwa chake huyo kondoo mume.
16 Sedan skall du slagta honom, och taga hans blod, och stänka uppå altaret allt omkring.
Kisha utamchinja huyo kondoo mume, na kuitwaa damu yake, na kuinyunyiza katika madhabahu kuizunguka kando-kando.
17 Men väduren skall du hugga i stycker, och två hans inelfver och fötter, och skall lägga det på hans stycker och hufvud;
Kisha utamkata-kata kondoo vipande vyake, na kuyaosha matumbo yake na miguu yake, na kuiweka pamoja na vipande vyake na kichwa chake,
18 Och bränna upp allan väduren på altaret; ty det är ett bränneoffer Herranom, en söt lukt Herranom.
nawe mteketeze kondoo mzima juu ya madhabahu. Ni sadaka ya kuteketezwa kwa ajili yaYahweh; ni harufu nzuri, sadaka iliyosongezwa kwa Yahweh kwa njia ya moto.
19 Den andra väduren skall du taga; och Aaron med hans söner skola lägga sina händer på hans hufvud;
Kisha mtwae huyo kondoo mwingine; na Aruni na wanawe wataweka mikono yao juu ya kichwa chake huyo kondoo.
20 Och skall slagtan, och taga af hans blod, och stryka på högra örnatimpen af Aaron och hans söner, och uppå tumman af deras högra hand, och på största tån af deras högra fot, och skall stänka blodet på altaret allt omkring.
Kisha utamchinja kondoo, na kuitwaa damu yake, na kuitia katika ncha ya sikio la Aruni la upande wa kuume, na katika ncha za masikio ya kuume ya wanawe, na katika vyanda vya gumba vya mikono yao ya kuume, na katika vidole vikuu vya miguu yao ya kuume, na kuinyunyiza hiyo damu katika madhabahu kuizunguka kando-kando.
21 Och skall taga blodet på altarena, och smörjooljo, och stänka på Aaron och hans kläder, hans söner och deras kläder; så varder han och hans kläder, hans söner och deras kläder vigd.
Kisha twaa katika hiyo damu iliyo juu ya madhabahu, na katika hayo mafuta ya kutiwa, na kumnyunyizia Aruni, juu ya mavazi yake, na wanawe, na mavazi yao pia, pamoja naye; naye atatakaswa, na mavazi yake, na wanawe, na mavazi ya wanawe, pamoja naye.
22 Sedan skall du taga det feta af väduren, stjerten, och det feta som är på inelfven, nätet som är öfver lefrena, och båda njurarna med det feta, som deröfver är, och den högra bogen; ty det är fyllelsens vädur;
Tena yatwae mafuta ya huyo kondoo mume, na mkia wake wa mafuta, na mafuta yafunikayo matumbo, na kitambi kilicho katika ini, na figo mbili, na mafuta yaliyo katika hizo figo, na paja la kuume; kwani ni kondoo ambaye ni wa kuwekwa kwa kazi takatifu.
23 Och ett bröd, och en oljokako, och en tunnkako, utu korgenom, der det osyrade brödet i är, den för Herranom står.
Utwae na mkate mmoja wa unga, na mkate mmoja ulioandaliwa kwa mafuta, na kaki moja katika kile kikapu cha mikate isiyotiwa chachu, kilichowekwa mbele ya Yahweh.
24 Och lägg allt detta på Aarons och hans söners händer; och vefta det Herranom.
Nawe utavitia hivi vyote katika mikono ya Aruni, na katika mikono ya wanawe; nawe utavitikisa-tikisa viwe sadaka ya kutikiswa mbele za Yahweh.
25 Och så skall du taga det utaf deras händer, och bränn det upp på altarena för ett bränneoffer, till en söt lukt för Herranom; ty det är Herrans offer.
Kisha uvitwae vile vitu mikononi mwao, na kuviteketeza juu ya madhabahu, juu ya ile sadaka ya kuteketezwa, viwe harufu nzuri mbele yangu; ni sadaka iliyotengenezwa kwangu kwa njia ya moto.
26 Och du skall taga bröstet af fyllelsens vädur Aarons, och skall vefta det för Herranom; det skall vara din del.
Kisha twaa kidari cha huyo kondoo wa kuwekwa kwake Haruni kwa kazi takatifu, na kukitikisa-tikisa kiwe sadaka ya kutikiswa mbele za Yahwe nacho kitakuwa ni sehemu yako.
27 Och skall alltså helga veftebröstet och häfvobogarna, som veftade och häfne äro af fyllelsens vädur, Aarons och hans söners.
Nawe kitakase kile kidari cha ile sadaka ya kutikiswa, na lile paja la sadaka ya kuinuliwa, lililotikiswa, na lililoinuliwa juu, vya yule kondoo wa kuwekwa kwa kazi takatifu, huyo aliyekuwa kwa ajili ya Aruni na wanawe.
28 Och det skall vara Aarons och hans söners, till ett evigt sätt af Israels barnom; ty det är ett häfoffer; och häfoffren skola höra Herranom till af Israels barnom i deras tackoffer och häfoffer.
Navyo vitakuwa vya Haruni na wanawe posho ya lazima sikuzote itokayo kwa hao wana wa Israeli; kwa kuwa ni sadaka ya kuinuliwa; nayo itakuwa ni sadaka ya kuinuliwa itokayo kwa hao wana wa Israeli katika dhabihu zao za sadaka za amani, ni sadaka yao ya kuinuliwa kwa ajili ya Yahweh.
29 Men Aarons helga kläder skola hans söner hafva efter honom, att de derutinnan skola varda smorde, och deras händer fyllda.
Na hayo mavazi matakatifu ya Aruni yatakuwa ya wanawe baada yake, wayavae watakapotiwa mafuta, na watakapowekwa kwa kazi takatifu.
30 Hvilken af hans söner varder Prest i hans stad, han skall kläda dem uppå i sju dagar, att han skall gå in uti vittnesbördsens tabernakel, till att tjena uti de helga.
Huyo mwanawe atakayekuwa kuhani badala yake atayavaa muda wa siku saba, hapo atakapoingia ndani ya hiyo hema ya kukutania, ili atumike ndani ya mahali patakatifu.
31 Du skall ock taga fyllelsens vädur, och koka hans kött på heligt rum.
Nawe twaa huyo kondoo mume aliyekuwa wa kuwekwa kwa kazi takatifu, na kuitokosa nyama yake katika mahali patakatifu.
32 Och Aaron med hans söner skola äta af samma vädurs kötte, med brödet, som i korgenom är, inför dörrena af vittnesbördsens tabernakel.
Na Aruni na wanawe wataila ile nyama ya kondoo, na mikate iliyo katika kile kikapu, hapo mbele ya mlango wa hema ya kukutania.
33 Ty en försoning är dermed skedd, till att fylla deras händer, att de skola vigde varda. Ingen annar skall ätat; ty det är heligt.
Nao watakula vile vitu ambavyo upatanisho ulifanywa kwa hivyo, ili kuwaweka kwa kazi takatifu na kuwatakasa; lakini mgeni asivile, maana, ni vitu vitakatifu.
34 Om något öfverblifver af fyllelsens kötte, och af brödena intill morgonen, det skall du uppbränna på elde, och icke låta ätat; ty det är heligt.
Na kwamba kitu cho chote cha ile nyama, iliyo kwa ajili ya kuweka kwa kazi takatifu, au cho chote cha hiyo mikate, kikisalia hata asubuhi, ndipo utavichoma kwa moto hivyo vilivyosalia; havitaliwa, maana, ni vitu vitakatifu
35 Och alltså skall du göra med Aaron och hans söner, såsom jag hafver budit dig. I sju dagar skall du fylla deras händer;
Ni hivyo utakavyowatendea Aruni na wanawe kama nilivyo kuagiza. Utawaweka kwa kazi takatifu siku saba.
36 Och hvar dag slagta en stut, till ett syndoffer till försoning; och skall skära altaren, när du försonar det, och skall smörja det, att det skall blifva vigdt.
Kila siku utamtoa ng’ombe wa sadaka ya dhambi kwa ajili ya upatanisho; nawe utaisafisha hiyo madhabahu, hapo utakapofanya upatanisho kwa ajili ya hiyo madhabahu; nawe utaitia mafuta, ili kuitakasa.
37 I sju dagar skall du försona och viga altaret, att det skall vara dess aldrahelgestas altare. Ho som vill komma vid altaret, han skall vara vigd.
Utafanya upatanisho kwa ajili ya hiyo madhabahu muda wa siku saba, na kuitakasa; ndipo madhabahu itakapokuwa takatifu sana; kila kitu kiigusacho madhabahu kitakuwa kitakatifu.
38 Och detta skall du göra med altaret; tu lamb årsgammal skall du hvar dag offra deruppå;
Lazima utoe kwenye madhabahu wana-kondoo wa mwaka mmoja wawili siku baada ya siku
39 Ett lamb om morgonen, det andra om aftonen;
daima. Mwana-kondoo mmoja utamchinja asubuhi; na mwana-kondoo wa pili utamchinja jioni
40 Och till ett lamb en tiung semlomjöl, blandadt med en fjerding af ett hin stött oljo; och en fjerding af ett hin vin till drickoffer.
Pamoja na mwana-kondoo mmoja utatoa vibaba vitatu vya unga mzuri uliochanganyika na mafuta yenye kupondwa, kiasi cha kibaba na robo kibaba; na divai kiasi cha kibaba na robo kibaba, iwe sadaka ya kinywaji.
41 Med det andra lambet om aftonen skall du göra såsom med morgonens spisoffer och drickoffer, till en söt lukt Herranom af offrena.
Na huyo mwana-kondoo wa pili utamchinja wakati wa jioni. Nawe utamfanyia vivyo kama ile sadaka ya unga ya asubuhi, na kama ile sadaka yake ya kinywaji. Hii itatoa harufu nzuri, ni dhabihu ya kusongezwa kwangu kwa njia ya moto.
42 Detta är det dageliga bränneoffret intill edra efterkommande, för dörrene af vittnesbördsens tabernakel för Herranom, der jag eder betyga, och med dig tala vill.
Itakuwa ni sadaka ya kuteketezwa milele katika vizazi vyenu vyote mlangoni pa ile hema ya kukutania mbele ya Yahweh, hapo nitakapokutana nanyi, ili niseme na wewe hapo.
43 Der vill jag Israels barnom betygad och helgad varda i mine härlighet;
Nami nitakutana na wana wa Israeli hapo; na hiyo hema itafanywa takatifu na utukufu wangu. Nami nitaitakasa hiyo hema ya kukutania, na hiyo madhabahu.
44 Och vill helga vittnesbördsens tabernakel med altarena, och viga Aaron med hans söner mig till Prester;
Pia Aruni na wanawe nitawatakasa, ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani.
45 Och vill bo ibland Israels barn, och vara deras Gud;
Na mimi nitakaa kati ya wana wa Israeli, nami nitakuwa Mungu wao.
46 Att de veta skola, att jag är Herren deras Gud, som dem förde utur Egypti land, att jag skulle bo ibland dem: Jag Herren deras Gud.
Nao watanijua kuwa mimi ndimi Yahweh, Mungu wao, niliyewaleta watoke katika nchi ya Misri, nipate kukaa kati yao. Ni mimi Yahweh, Mungu wao.

< 2 Mosebok 29 >