< 2 Mosebok 27 >
1 Och du skall göra ett altare af furoträ, fem alnar långt och bredt, så att det varder rätt fyrakant, och tre alnar högt.
Nawe fanya madhabahu ya mti wa mshita, urefu wake utakuwa ni dhiraa tano na upana wake dhiraa tano. Hiyo madhabahu itakuwa mraba na kwenda juu kwake kutakuwa dhiraa tatu.
2 Horn skall du göra på alla fyra hörnen, och du skall öfverdraga det med koppar.
Nawe fanya pembe nne kama mfano wa pembe za ng'ombe. Hizo pembe zitakuwa za kitu kimoja na madhabahu, nawe utayafunika kwa shaba.
3 Gör ock askokäril, skoflar, bäcken, gafflar, kolpannor; allt det dertill hörer, skall du göra af koppar.
Lazima vyombo vyake vya kuyaondoa majivu yake utavifanya, na majembe yake, na mabakuli yake, na uma zake, na meko yake. Vyombo vyake vyote utavifanya vya shaba.
4 Du skall ock göra ett galler, såsom ett nät, af koppar, och fyra kopparringar på dess fyra hörn.
Nawe uifanyie hiyo madhabahu wavu wa shaba. Kisha utie pete nne za shaba katika hizo pembe nne za ule wavu.
5 Du skall ock görat ifrå nedan uppåt kringom altaret, så att gallret räcker midt uppå altaret.
Nawe lazima uweke huo wavu chini ya kizingo kiizungukacho madhabahu upande wa chini.
6 Och skall du göra stänger till altaret af furoträ, öfverdragna med koppar.
Nawe fanya miti kwa ajili ya madhabahu, miti ya mshita, na kuifunika shaba.
7 Och skall du stinga stängerna in i ringarna, så att stängerna äro på båda sidor af altaret, der man må bära det med.
Na hiyo miti itatiwa katika viduara, na ile miti itakuwa katika pande mbili za madhabahu, wakati wa kuichukua.
8 Och skall du så görat af bräder, att det blifver ihålt, såsom dig på berget vist är.
Uifanye ya mbao, yenye mvungu ndani yake kama ulivyooneshwa mlimani.
9 Du skall ock göra en gård till tabernaklet; en bonad af hvitt tvinnadt silke, på den ena sidon, hundrade alnar lång söderut;
Nawe ufanye ua wa maskani. Upande wa kusini wa kuelekea kusini kutakuwa na chandarua ya nguo ya kitani nzuri yenye kusokotwa, kwa huo ua, urefu wake upande mmoja utakuwa ni dhiraa mia moja.
10 Och tjugu stolpar på tjugu kopparfötter; och deras knappar med deras gjordar af silfver.
Na nguzo zake zitakuwa nguzo ishirini, na vitako vyake ishirini, vitako vyake vitakuwa vya shaba kulabu za zile nguzo na vitanzi vyake vitakuwa vya fedha.
11 Sammalunda ock norruppå en bonad, hundrade alnar lång; tjugu stolpar på tjugu kopparfötter, och deras knappar med deras gjordar af silfver.
Ni vivyo hivyo upande wa kaskazini, urefu wake hiyo chandarua utakuwa ni dhiraa mia moja, na nguzo zake ishirini, na vitako vyake ishirini vitakuwa vya shaba, kulabu za zile nguzo na vitanzi vyake vitakuwa vya fedha.
12 Men vesterut öfver gårdsens bredd skall vara en bonad, femtio alnar lång; tio stolpar på tio fötter.
Na upande wa magharibi, upana wa ua kutakuwa na chandarua ya dhiraa hamsini; nguzo zake kumi, na vitako vyake kumi.
13 Österut öfver gårdsens bredd skall vara femtio alnar;
Na upana wa ule ua upande wa mashariki kuelekea mashariki utakuwa ni dhiraa hamsini.
14 Så att bonaden hafver på ene sidone femton alnar; dertill tre stolpar på tre fötter;
Chandarua upande mmoja wa lango itakuwa dhiraa kumi na tano upana wake. Lazima nguzo zake zitakuwa tatu na vitako vyake vitatu.
15 Och femton alnar på den andra sidone; dertill tre stolpar på tre fötter.
Upande wa pili ni vivyo hivyo chandarua ya dhiraa kumi na tano; nguzo zake tatu, na vitako vyake vitatu.
16 Men i gårdsens ingång skall vara ett kläde, tjugu alnar bredt, stickadt med gult silke, skarlakan, rosenrödt och hvitt tvinnadt silke; dertill fyra stolpar på deras fyra fötter.
Na kwa lile lango la ua patakuwa na kisitiri cha dhiraa ishirini, kitakuwa cha nguo ya rangi ya buluu, zambarau na nyekundu, na kitani nzuri yenye kusokotwa, kazi ya mshonaji taraza; nguzo zake zitakuwa nne, na vitako vyake vinne.
17 Alle stolparna kringom gården skola hafva silfvergjordar, och silfverknappar, och kopparfötter.
Nguzo zote za ule ua ziuzungukao pande zote zitakuwa na vitanzi vya fedha; kulabu zake za fedha, na vitako vyake vya shaba.
18 Och längden på gården skall vara hundrade alnar, bredden femtio, höjden fem alnar, af hvitt tvinnadt silke, och deras fötter skola vara af koppar.
Urefu wa huo ua utakuwa dhiraa mia moja, na upana wake utakuwa dhiraa hamsini kotekote, na kwenda juu kwake dhiraa tano; yawe ya nguo ya kitani nzuri, na vitako vyake vitakuwa vya shaba.
19 Och allt det som tabernaklet tillhörer till allahanda ämbete, och alle dess pålar, och alle gårdsens pålar, skola vara af koppar.
Vyombo vyote vya maskani vitumiwavyo katika utumishi wake wote, na vigingi vyake vyote, na vigingi vyote vya ule ua, vitakuwa vya shaba.
20 Bjud Israels barnom, att de bära till dig den aldraklaresta oljo, stött af oljoträ, till lysning; att man alltid deraf låter i lamporna;
awe waamuru wana wa Israeli wakuletee mafuta ya zeituni safi ya kupondwa kwa ajili ya nuru, ili kufanya ile taa kuwaka daima.
21 Uti vittnesbördsens tabernakel utanför förlåten, som hänger för vittnesbördet. Och Aaron med hans söner skola detta sköta, ifrå morgonen allt intill aftonen för Herranom. Det skall vara eder en evig sed intill edra efterkommande, ibland Israels barn.
Ndani ya ile hema ya kukutania, nje ya hilo pazia, lililo mbele ya huo ushuhuda, Haruni na wanawe wataitengeza tangu jioni hadi asubuhi mbele ya BWANA; itakuwa ni amri ya milele katika vizazi vyao vyote kwa ajili ya wana wa Israeli.