< Ester 1 >

1 Uti Ahasveros tid, hvilken rådandes var, allt ifrån Indien intill Ethiopien, öfver hundrade sju och tjugu land;
Hili ndilo lililotokea wakati wa utawala wa Mfalme Ahasuero, yule aliyetawala juu ya majimbo mia na ishirini na saba tangu Bara Hindi hadi Kushi.
2 Då han satt på sinom Konungsliga stol, i den staden Susan;
Wakati huo Mfalme Ahasuero alitawala katika kiti chake cha enzi katika ngome ya mji wa Shushani.
3 I tredje årena hans rikes, gjorde han ett gästabåd när sig, åt alla sina Förstar och tjenare; nämliga dem väldigom i Persien och Meden, landshöfdingom och öfverstom i sin land;
Katika mwaka wa tatu wa utawala wake, alifanya karamu kwa ajili ya wakuu wake wote pamoja na maafisa. Akawaalika viongozi wa jeshi wa Uajemi na Umedi, wana wa wafalme na wakuu wa majimbo.
4 På det han skulle låta se sins rikes härliga rikedomar och det kosteliga prål af sitt majestät, i många dagar, nämliga i hundrade och åttatio dagar.
Kwa siku zote 180 mfalme alionyesha utajiri mwingi wa ufalme wake, fahari na utukufu wa enzi yake.
5 Då de dagar ute voro, gjorde Konungen ett gästabåd allo folkena, som i stadenom Susan var, både stora och små, i sju dagar, uti en sal i trägårdenom invid Konungshuset.
Siku hizo zilipopita, mfalme alifanya karamu kwa muda wa siku saba, katika bustani ya ndani katika jumba la kifalme, kwa ajili ya watu wote kuanzia mdogo hadi mkubwa, waliokuwa katika ngome ya mji wa Shushani.
6 Der voro upphängd hvit, röd och gul tapeter, fattad med linnen och skarlakanståg, uti silfringar på marmorstodar. Bänkerna voro af guld och silfver, på golfvena, som lagdt var med grön, hvit, gul och svart marmorsten.
Bustani ilikuwa na mapazia ya kitani nyeupe na buluu, yaliyofungiwa kamba za kitani nyeupe na kitambaa cha zambarau, kwenye pete za fedha juu ya nguzo za marmar. Kulikuwepo viti vya dhahabu na vya fedha vilivyokuwa vimewekwa kwenye ile sakafu iliyotengenezwa kwa mawe ya rangi, marmar, lulumizi na mawe mengine ya thamani.
7 Och dryckerna bar man in uti gyldene kar, och ju annor och annor kar, och Konungsligit vin tillfyllest, såsom Konungen det väl förmådde.
Vyombo vya dhahabu vilitumika kwa watu kunywea mvinyo, kila kimoja tofauti na kingine, naye mfalme akatoa mvinyo kwa wingi kwa kadiri ya ukarimu wake.
8 Och man lade ingom före hvad han dricka skulle; ty Konungen hade befallt alla föreståndarena i sitt hus, att hvar och en skulle göra såsom honom lyste.
Kwa amri ya mfalme kila mgeni aliruhusiwa kunywa alichotaka, kwa kuwa mfalme alitoa maagizo kwa watumishi wote wa kuhudumu mvinyo kumhudumia kila mtu kwa jinsi alivyotaka.
9 Och Drottningen Vasthi gjorde också ett gästabåd för qvinnorna uti Konungshusena, der Konung Ahasveros plägade vistas.
Malkia Vashti pia akawafanyia wanawake karamu katika jumba la kifalme la Mfalme Ahasuero.
10 Och på sjunde dagen, då Konungen vardt lustig af vinet, sade han till Mehuman, Bistha, Harbona, Bigtha, Abagtha, Sethar och Charcas, de sju kamererare, som för Konung Ahasveros tjente,
Siku ya saba, wakati Mfalme Ahasuero alikuwa amesisimka roho yake kwa mvinyo, aliamuru matowashi saba waliokuwa wakimhudumia, yaani, Mehumani, Biztha, Harbona, Bigtha, Abagtha, Zethari na Karkasi,
11 Att de skulle hafva Drottning Vasthi in för Konungen, med Drottningakrono, på det han skulle låta folket och Förstarna se hennes dägelighet; ty hon var dägelig.
kumleta Malkia Vashti mbele ya mfalme akiwa amevaa taji lake la kifalme, ili aonyeshe uzuri wake kwa watu na wakuu, kwa kuwa alikuwa ni mzuri wa kupendeza.
12 Men Drottning Vasthi ville icke komma efter Konungens ord, genom hans kamererare. Då vardt Konungen ganska vred, och upptänd i grymhet.
Lakini wakati watumishi walipotoa amri ya mfalme, Malkia Vashti alikataa kuja. Ndipo mfalme alighadhibika, na hasira yake ikawaka.
13 Och Konungen sade till de visa, som i landsseder förfarne voro; ty Konungens ärende måste hafvas inför alla förståndiga i lag och rätt;
Kwa kuwa ilikuwa desturi ya mfalme kupata ushauri kwa wataalamu katika mambo ya sheria na haki, alizungumza na watu wenye busara, ambao walijua nyakati,
14 Men de näste, som när honom voro, voro Charsena, Sethar, Admatha, Tharsis, Meres, Marsena och Memuchan, de sju Förstar af Persien och Meden, som sågo på Konungens ansigte, och såto främst i rikena;
nao waliokuwa karibu na mfalme ni Karshena, Shethari, Admatha, Tarshishi, Meresi, Marsena na Memukani, wakuu saba wa Uajemi na Umedi waliokuwa na nafasi ya pekee kwa mfalme nao walikuwa na vyeo vya juu kabisa katika utawala wake.
15 Hvad man göra skulle Drottning Vasthi för en rätt, derföre, att hon icke gjort hade efter Konungens ord, genom hans kamererare.
Mfalme akauliza, “Kulingana na sheria, Malkia Vashti anapaswa kutendewa nini? Malkia hakutii amri ya Mfalme Ahasuero ambayo matowashi walimpelekea.”
16 Då sade Memuchan inför Konungenom och Förstarna: Drottning Vasthi hafver icke allenast illa gjort emot Konungen, utan ock emot alla Förstar, och allt folk uti Konung Ahasveros landom.
Kisha Memukani akajibu mbele ya mfalme na wakuu, “Malkia Vashti si kwamba amemkosea mfalme tu bali pia amewakosea wakuu wote na watu wa himaya yote ya Mfalme Ahasuero.
17 Förty detta stycket af Drottningen kommer väl ut till alla qvinnor, så att de skola förakta sina män för sin ögon, och skola säga: Konung Ahasveros böd Drottningene Vasthi komma inför sig, men hon ville icke.
Kwa maana tendo hili la malkia litajulikana kwa wanawake wote, kwa hiyo watawadharau waume zao na kusema, ‘Mfalme Ahasuero aliagiza Malkia Vashti aletwe mbele yake, lakini alikataa.’
18 Så varda nu de Förstinnor i Persien och Meden sammalunda sägande till alla Konungens Förstar, när de få detta Drottningenes stycke höra; så skall föraktelse och vrede nog upphäfva sig.
Leo hii wanawake wa wakuu wa Uajemi na Umedi ambao wamesikia juu ya tabia ya malkia watawatendea wakuu wote wa mfalme vivyo hivyo. Hapatakuwepo na mwisho wa dharau na magomvi.
19 Om Konungenom så täckes, så låte han ett Konungsligit bud af sig utgå, och skrifva efter de Persers och Meders lag, hvilken man icke öfverträda tör, att Vasthi icke mer skall komma inför Konung Ahasveros; och Konungen gifve hennes rike hennes nästo, den bättre är än hon.
“Kwa hiyo, kama itampendeza mfalme, atoe amri ya kifalme na iandikwe katika sheria ya Uajemi na Umedi, ambayo haitabadilika, kwamba Vashti kamwe asije tena mbele ya Mfalme Ahasuero. Pia mfalme na atoe hiyo nafasi yake ya umalkia kwa mwanamke mwingine aliye bora kumliko yeye.
20 Och att detta Konungens bref, som göras skall, må förkunnadt varda i hela rikena, det väl stort är, att alla qvinnor måga hålla sina män för ögon, ibland både små och stora.
Kisha mbiu hii ya mfalme itakapotangazwa katika himaya yake iliyo kubwa sana, wanawake wote watawaheshimu waume zao, kuanzia mdogo hadi mkubwa.”
21 Detta täcktes Konungenom och Förstarna; och Konungen gjorde efter Memuchans ord.
Mfalme na wakuu wake walipendezwa na shauri hili, hivyo basi mfalme akafanya kama Memukani alivyopendekeza.
22 Då vordo bref utsänd i all Konungens land, i hvart landet efter dess skrift, och till hvart folk efter dess tungomål, att hvar och en man skulle vara husbonde i sitt hus; och lät tala efter sins folks tungomål.
Alipeleka barua katika sehemu zote za ufalme wake, kwa kila jimbo kwa maandishi yake mwenyewe na kwa kila watu katika lugha yao wenyewe, akitangaza kwa msemo wa kila watu kwamba inampasa kila mwanaume kuwa mtawala wa nyumba yake mwenyewe.

< Ester 1 >