< 5 Mosebok 3 >

1 Och vi vände om, och drogo upp, den vägen till Basan. Och Og, Konungen i Basan, drog ut emot oss med allt sitt folk, till att strida vid Edrei.
Kisha tukageuka tukakwea kufuata njia iliyoelekea Bashani, Ogu mfalme wa Bashani akaondoka na jeshi lake lote kupigana na sisi huko Edrei.
2 Men Herren sade till mig: Frukta dig intet för honom; ty jag hafver gifvit honom i dina händer, och allt hans folk med hans land, och du skall göra med honom, såsom du gjorde med Sihon, de Amoreers Konung, den i Hesbon satt.
Bwana akaniambia, “Usimwogope kwa kuwa nimekwisha mkabidhi mikononi mwako pamoja na jeshi lake lote na nchi yake. Umfanyie sawasawa na ulivyomfanyia Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala huko Heshboni.”
3 Alltså gaf Herren vår Gud ock Konung Og i Basan i våra händer, med allt hans folk, så att vi sloge honom, tilldess honom intet igenblef.
Hivyo Bwana Mungu wetu pia akamweka Ogu mfalme wa Bashani pamoja na jeshi lake lote mikononi mwetu. Tuliwaangamiza wote, hakubakia hata mmoja.
4 På samma tid vunne vi alla hans städer, och var ingen stad den vi honom icke aftogom; sextio städer, hela den ängden Argob i Ogs rike, som var i Basan;
Wakati huo tuliteka miji yake yote. Hakuna mji hata mmoja kati ya ile sitini ambao hatukuuteka, yaani eneo lote la Argobu, utawala wa Mfalme Ogu katika Bashani.
5 Alle desse städer voro faste med höga murar, portar och bommar, förutan andra ganska många små städer, som ingen mur hade;
Miji yote hii ilijengewa ngome zenye kuta ndefu zenye malango na makomeo, pia kulikuwako na vijiji vingi ambavyo havikujengewa kuta.
6 Och gåfvom dem tillspillo, såsom vi, med Sihon, Konungenom i Hesbon, gjort hade; alla städer gåfve vi tillspillo, både med män, qvinnor och barn.
Tuliwaangamiza kabisa, kama tulivyomfanyia Sihoni mfalme wa Heshboni, tukiangamiza kila mji, yaani wanaume, wanawake na watoto.
7 Men allan boskapen, och rofvet af städerna toge vi för oss.
Lakini wanyama wote wa kufuga pamoja na nyara kutoka kwenye miji yao tulichukua vikawa vyetu.
8 Alltså toge vi i den tiden landet utu de två Amoreers Konungars händer på hinsidon Jordan, ifrå den bäcken vid Arnon, allt intill det berget Hermon;
Hivyo kwa wakati huo tukachukua kutoka kwa wafalme hawa wawili wa Waamori nchi ya mashariki ya Yordani, kutoka Bonde la Arnoni mpaka kufika kwenye Mlima Hermoni.
9 Hvilket de Sidonier Sirion kalla; men de Amoreer kalla det Senir;
(Wasidoni huuita mlima huo Sirioni, nao Waamori huuita Seniri.)
10 Alla de städer på slättene, och hela Gilead, och hela Basan, allt intill Salcha och Edrei, som äro städer i Ogs rike i Basan.
Tuliteka miji yote kwenye uwanda wa juu, Gileadi yote, Bashani yote mpaka kufika Saleka na Edrei, miji ya utawala wa Ogu huko Bashani.
11 Ty allena Konung Og i Basan var ännu igen utaf de Resar. Si, hans säng af jern är här i Rabbath, som hörer Ammons barnom till, nio alnar lång, och fyra alnar bred, efter ens mans armbåga.
(Mfalme Ogu wa Bashani ndiye peke yake aliyesalia miongoni mwa mabaki ya Warefai. Kitanda chake kilikuwa cha chuma chenye urefu wa dhiraa tisa na upana wa dhiraa nne. Mpaka sasa kinaweza kuonekana katika mji wa Waamoni wa Raba.)
12 Så toge vi då landet in på den tiden, ifrån Aroer, som ligger när bäcken vid Arnon; och halfva landet af Gileads berg, med dess städer, gaf jag de Rubeniter och Gaditer.
Katika nchi tuliyoiteka wakati ule, niliwapa kabila la Reubeni na Gadi eneo lililoko kaskazini la Aroeri kando ya Bonde la Arnoni, na nusu ya eneo la milima ya Gileadi, pamoja na miji yake.
13 Men det öfver var i Gilead, och hela Basan af Ogs rike, gaf jag den halfva slägtene Manasse; den hela ängden Argob med hela Basan, som kallas de Resars land.
Kisha nusu ya kabila la Manase niliwapa sehemu ya Gileadi iliyobaki pamoja na Bashani yote, ambayo ilikuwa utawala wa Ogu. (Eneo lote la Argobu katika Bashani lilikuwa linajulikana kama nchi ya Warefai.
14 Jair, Manasse son, fick den hela ängden Argob, allt intill Gessuri och Maachathi landsändar; och kallade Basan efter sitt namn, HavothJair, allt intill denna dag.
Yairi, mzao wa kabila la Manase, alichukua eneo lote la nchi ya Argobu hadi kufikia mpaka wa Wageshuri na Wamaaka, ukaitwa kwa jina lake; kwa hiyo mpaka leo hii Bashani inaitwa Hawoth-Yairi.)
15 Men Machir gaf jag Gilead.
Nikampa Makiri nchi ya Gileadi.
16 Och de Rubeniter och Gaditer gaf jag en del af Gilead, allt intill bäcken vid Arnon, midt i bäcken, der landamäret är, och allt intill den bäcken Jabbok, der landamäret är för Ammons barn;
Lakini niliwapa Wareubeni na Wagadi eneo kuanzia Gileadi hadi Bonde la Arnoni (katikati ya bonde ulikuwa ndio mpaka), kuelekea mpaka Mto Yaboki, ambao ndio mpaka wa Waamoni.
17 Dertill den slättmarkena, och Jordan, den landamäret är, ifrå Cinnereth intill hafvet vid slättmarkena; nämliga salthafvet nedan vid berget Pisga österut.
Kwa upande wa magharibi mpaka wao ulikuwa Yordani katika Araba, toka ziwa Galilaya hadi Bahari ya Araba (yaani Bahari ya Chumvi), kwenye miteremko ya Pisga upande wa mashariki.
18 Och jag böd eder på samma tiden, och sade: Herren edar Gud hafver gifvit eder detta landet att intaga det; så drager nu väpnade för edra bröder Israels barn, alle I som stridsamme ären;
Wakati huo nilikuamuru: “Bwana Mungu wako amekupa nchi hii uimiliki. Lakini ni lazima wanaume wenu wote wenye uwezo, wakiwa wamejiandaa tayari kwa vita, wavuke ngʼambo wakiwatangulia ndugu zako Waisraeli.
19 Förutan edra hustrur, barn och boskap; ty jag vet, att I hafven mycken boskap; låter dem blifva uti edra städer, som jag eder gifvit hafver;
Lakini wake zenu, watoto wenu na mifugo yenu (kwani najua mnayo mifugo mingi) wanaweza kukaa katika miji niliyowapa,
20 Tilldess Herren låter ock edra bröder komma till rolighet såsom eder, att de ock intaga det land, som Herren deras Gud dem gifva skall på hinsidon Jordan; sedan skolen I omvända till edor besittning, den jag eder gifvit hafver.
mpaka hapo Bwana atakapowapa ndugu zenu kupumzika kama alivyowapa ninyi, wao pia wamiliki ile nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa, ngʼambo ya Yordani. Baada ya hapo, kila mmoja wenu anaweza kurudi kwenye milki niliyowapa.”
21 Och jag böd Josua på samma tiden, och sade: Din ögon hafva sett allt det som Herren edar Gud dessa två Konungar gjort hafver; så varder Herren ock görandes all Konungarike, dit du drager.
Wakati huo nilimwamuru Yoshua, “Umejionea kwa macho yako mwenyewe yale yote ambayo Bwana Mungu wenu amewafanyia wafalme hawa wawili. Bwana atazifanyia falme zote huko mnakokwenda vivyo hivyo.
22 Frukter eder intet för dem; ty Herren edar Gud strider för eder.
Msiwaogope, Bwana Mungu wenu atapigana kwa ajili yenu.”
23 Och jag bad Herran på den tiden, och sade:
Wakati huo nilimsihi Bwana:
24 Herre, Herre, du hafver begynt visa dinom tjenare dina härlighet och dina starka hand; ty hvilken är den Gud i himmelen eller på jordene, som förmår efter din verk och din magt göra?
“Ee Bwana Mwenyezi, umemwonyesha mtumishi wako ukuu wako na mkono wako wenye uweza. Kwa kuwa ni mungu yupi aliye mbinguni au duniani anayeweza kufanya kazi na matendo makuu kama ufanyayo wewe?
25 Låt mig gå och se det goda landet, på hinsidon Jordan; de goda berg, och Libanon.
Acha niende nikaione hiyo nchi nzuri ngʼambo ya Yordani, ile nchi nzuri ya vilima na Lebanoni.”
26 Men Herren vardt vred på mig för edra skull, och bönhörde mig intet; utan Herren sade till mig: Låt blifvat: tala intet mer derom för mig.
Lakini kwa sababu yenu Bwana alinikasirikia na hakutaka kunisikiliza. Bwana aliniambia, “Hilo latosha; usiseme nami jambo hili tena.
27 Stig upp på höjden af berget Pisga, och häf din ögon upp vesterut, och norrut, och söderut, och österut, och se det med ögonen; ty du skall intet gå utöfver denna Jordan;
Kwea juu ya kilele cha Pisga uangalie magharibi, kaskazini, kusini na mashariki. Iangalie hiyo nchi kwa macho yako, kwa vile wewe hutavuka Yordani.
28 Utan bjud Josua, att han är tröst och frimodig; förty han skall gå öfver Jordan för folket, och skall utskifta dem landet, som du seendes varder.
Lakini mwagize Yoshua, mtie moyo na umtie nguvu, kwa kuwa yeye atawaongoza watu hawa hadi ngʼambo na kuwarithisha nchi utakayoiona.”
29 Så blefvo vi då i den dalen in mot Peors hus.
Kwa hiyo tulikaa kwenye bonde karibu na Beth-Peori.

< 5 Mosebok 3 >