< 2 Samuelsboken 21 >
1 Så vardt en hård tid i Davids dagar i tre år efter hvartannat; och David sökte Herrans ansigte; och Herren sade: För Sauls skull, och för det blodhus skull, derföre att han drap de Gibeoniter.
Kulikuwa na njaa kwa miaka mitatu katika siku za utawala wa Daudi, na Daudi akautafuta uso wa Yahwe. “Hivyo Yahwe akasema, “njaa hii ni kwa sababu ya mauaji ya Sauli na familia yake, kwa kuwa aliwauwa Wagibeoni.”
2 Då lät Konungen kalla de Gibeoniter, och talade med dem; men de Gibeoniter voro icke utaf Israels barn, utan voro igenblefne utaf de Amoreer; men Israels barn hade svorit dem; och Saul sökte efter att slå dem i sitt nit för Israels barn och Juda.
Basi Wagibeoni hawakuwa uzao wa Israeli; walikuwa ni masalia ya Waamori. Watu wa Israeli walikuwa wameapa kutowauwa, lakini Sauli alitaka kuwaangamiza wote kwa husuda kwa ajili ya watu wa Israeli na Yuda.
3 Så sade nu David till de Gibeoniter: Hvad skall jag göra eder? Och hvarmed skall jag försonat, att I mågen välsigna Herrans arfvedel?
Ndipo Daudi alipowaita pamoja Wagibeoni na kuwaambia, “Niwafanyie nini kwa ajili ya upatanisho? Ili kwamba mweze kuwabariki watu wa Yahwe wanaorithi wema na ahadi zake?”
4 De Gibeoniter svarade honom: Oss är intet om guld eller silfver af Saul eller hans hus; och är oss intet om, att någor skall dräpas af Israel. Han sade: Hvad sägen I då, det jag eder göra skall?
Wagibeoni wakamjibu, “Hili siyo jambo la fedha wala dhahabu kati yatu na Sauli au familia yake. Na siyo hitaji letu kumwua mtu yeyote katika Israeli.” Daudi akasema, “Chochote mtakacho omba nitawafanyia.”
5 De sade till Konungen: Den mannen, som oss förderfvat och tillintetgjort hafver, honom skole vi förderfva, så att intet blifver qvart af honom i alla Israels gränsor.
Wakamjibu mfalme, “Mtu aliyetaka kutuuwa aliyepanga kunyume chetu, ili kutuangamiza na kukosa eneo katika mipaka ya Israeli -
6 Gif oss sju män utaf hans hus, att vi upphänge dem Herranom i Gibea Sauls, Herrans utvaldas. Konungen sade: Jag vill få eder dem.
haya na tupewe watu saba kutoka katika uzao wake, nasi tutawatundika mbele ya Yahwe katika Gibea ya Sauli, palipochaguliwa na Yahwe.” Mfalme akasema, “Nitawapeni”
7 Men Konungen skonade MephiBoseth, Jonathans son, Sauls sons, för Herrans eds skull, som emellan dem var, nämliga, emellan David och Jonathan, Sauls son.
Lakini mfalme akamwifadhi Mefiboshethi mwana wa Yonathani mwana wa Sauli, kwa ajili ya kiapo cha Yahwe kati ya Daudi na Yonathani mwana wa Sauli.
8 Men de två Rizpa söner, Aja dotters, hvilka hon Saul födt hade, Armoni och MephiBoseth; dertill de fem Michals söner Sauls dotters, hvilka hon Adriel, Barsillai den Meholathitens son, födt hade, tog Konungen;
Mfalme akawachukua wana wawili wa Rispa binti Ayia aliomzalia Sauli, hawa wana wawili waliitwa Armoni na Mefiboshethi; na pia Daudi akawachukua wana watano wa Mikali binti Sauli, aliomzalia Adrieli mwana wa Berzilai Mmeholathi.
9 Och fick dem uti de Gibeoniters hand; dem upphängde de på bergena för Herranom. Och så föllo desse sju på eno reso; och blefvo döde i första andene, när bjugganden uppågick.
Akawaweka katika mikono ya Wagibeoni. Nao wakawatundika juu ya mlima mbele za Bwana, na wote saba wakafa pamoja. Waliuawa katika kipindi cha mavuno, katika siku ya kwanza mwanzoni mwa mavuno ya shayiri.
10 Då tog Rizpa, Aja dotter, en säck och bredde honom på ena håll i andenes begynnelse, intilldess vattnet af himmelen dröp uppå dem; och lät i den dagen inga himmelens foglar sätta sig på dem; ej heller markenes djur om nattena.
Kisha Rispa, binti Aiya, akachukua nguo ya gunia na akajitanda mwenyewe juu ya mlima kando ya miili ya waliokufa tangu mwanzo wa mavuno mpaka wakati mvua ilipoanza kunyesha. Hakuruhusu ndege wa angani kutua juu ya miili mchana wala ayawani wa mwituni wakati wa usiku.
11 Och det vardt sagdt David, hvad Rizpa, Aja dotter, Sauls frilla, gjort hade.
Daudi akaambia alichokifanya Rispa, binti Aiya, suria wa Sauli.
12 Och David gick bort, och tog Sauls ben, och Jonathans hans sons ben ifrå de borgare i Jabes i Gilead, hvilken de utaf Bethsans gato stulit hade; der de Philisteer dem hängt hade, på den tiden då de Philisteer slogo Saul på Gilboa berg;
Hivyo Daudi akaenda na kuchukua mifupa ya Sauli na mifupa ya Yonathani mwanawe kutoka kwa watu wa Yabeshi Gileadi, waliokuwa wameiiba kutoka katika eneo la jumuiya la Beth Shani, Wafilisti walipokuwa wamewatundika baada ya Wafilisti kumwua Sauli katika Gilboa.
13 Och förde dem dädan ditupp, och samkade dem tillhopa med de hängdas ben;
Daudi akaiondoa pale mifupa ya Sauli na mifupa ya Yonathani mwanawe, na wakakusanya pia mifupa ya wale watu saba waliotundikwa.
14 Och begrofvo Sauls och hans sons Jonathans ben i BenJamins land i Zela, i hans faders Kis graf; och gjorde allt såsom Konungen budit hade. Alltså vardt då Gud sedan landena försonad.
Wakaizika mifupa ya Sauli na Yonathani mwanawe huko Zela katika nchi ya Benjamini, katika kaburi la Kishi babaye. Wakafanya kila alichoagiza mfalme. Ndipo Mungu akajibu maombi yao kwa ajili ya nchi.
15 Så hof sig åter ett örlig upp utaf de Philisteer emot Israel. Och David drog neder, och hans tjenare med honom, och stridde emot de Philisteer. Och David vardt trött.
Kisha Wafilisti wakaenda tena katika vita na Israeli. Hivyo Daudi na jeshi lake wakashuka na kupigana na Wafilisti. Akiwa vitani Daudi akachoshwa na vita.
16 Och Jesbi af Nob, hvilken en af Rapha barn var, och hans glafvens vigt var trehundrad kopparsvigter, och han hade ett nytt harnesk uppå, han for efter att slå David.
Ishbibenobu, wa uzao wa majitu, ambaye mkuki wake wa shaba ulikuwa na uzito wa shekeli mia tatu na alikuwa na upanga mpya, alitaka kumwua Daudi.
17 Men Abisai, ZeruJa son, halp honom, och slog den Philisteen ihjäl. Då svoro honom Davids män, och sade: Du skall icke mer draga ut med oss i strid, att icke utsläckes lyktan i Israel.
Lakini Abishai mwana wa Seruya akamwokoa Daudi, akampiga Mfilisti na kumwua. Ndipo watu wa Daudi wakamwapia, kusema, “Hautakwenda vitani pamoja nasi tena usije ukaizima taa ya Israeli.”
18 Sedan hof sig åter ett örlig upp i Gob med de Philisteer; då slog Sibbechai, den Husathiten, Saph, den ock en var utaf de Rapha barn.
Ikawa baadaye kuwa na vita tena kati ya Wafilisti huko Gobu, wakati Sibekai Mhushathi alipomwua Safu, aliyekuwa miongoni mwa uzao wa Warefai.
19 Och sig hof ännu upp ett örlig i Gob med de Philisteer; då slog ElhananJaere, Orgims son, en BethLehemit, Goliath, den Gitthiten, hvilken hade en spets, hvilkens stång var såsom ett väfträ.
Ikawa tena katika vita na Wafilisti huko Gobu, huyo Elhanani mwana wa Jari Mbethlehemu akamwua Goliathi Mgiti, ambaye fumo la mkuki wake lilikuwa kama mti wa mfumaji.
20 Och sig upphof ännu ett örlig i Gath. Der var en lång man, han hade sex finger på sina händer, och sex tår på sina fötter, så att de voro fyra och tjugu på talet; och han var också födder af Rapha.
Ikawa katika vita nyingine huko Gathi kulikuwa na mtu mrefu sana mwenye vidole sita katika kila mkono na vidole sita katika kila mguu, jumla yake ishirini na vinne. Yeye naye alikuwa wa uzao wa Warefai.
21 Och då han talade hädelse till Israel, slog honom Jonathan, Simea son, Davids broders.
Alipowatukana Israeli, Yonathani mwana mwana wa Shama, nduguye Daudi, akamwua.
22 Desse fyra voro Rapha födde i Gath; och föllo igenom Davids och hans tjenares hand.
Hawa walikuwa wa uzao wa Warefai wa Gathi, waliuawa kwa mkono wa Daudi na kwa mkono wa askari wake