< 2 Kungaboken 25 >

1 Och det begaf sig i nionde årena af hans rike, på tionde dagen i tionde månadenom, kom NebucadNezar, Konungen i Babel, med all sin magt för Jerusalem, och de lägrade sig der före, och byggde skansar allt omkring.
Ilitokea kwamba katika mwaka wa tisa wa utawala wa mfalme Sedekia, katika mwezi wa kumi, na siku ya kumi ya huo mwezi, Nebukadreza mfalme wa Babeli alikuja pamoja na jeshi lake lote kwa ajili ya kupigana dhidi ya Yerusalemu. Akaweka kambi kuelekeana nayo, na wakajenga ukuta kuizunguka.
2 Alltså vardt staden belagd, allt intill ellofte året af Konung Zedekia rike.
Hivyo mji huo ulizungukwa mpaka miaka kumi na moja ya utawala wa Sedekia.
3 Men i nionde månadenom vardt hungren stark i stadenom, så att folket i landena hade intet äta.
Katika siku ya tisa ya mwezi wa nne wa huo mwaka, njaa ilikuwa kali sana kwenye huo mji kwamba hapakuwa na chakula kwa ajili ya watu wa nchi.
4 Då föll man in i staden, och alle krigsmän flydde om nattena, den vägen ifrå porten, som går emellan de två murar åt Konungsträgården. Och de Chaldeer lågo omkring staden. Och han flydde den vägen åt hedmarkena.
Wakati huo ule mji ulikuwa umebomoka ndani, na wapiganaji wote wakakimbia usiku kwa njia ya lango kati ya kuta mbili, karibu na bustani ya mfalme, ingawa Wakaldayo walikuwa wote wameuzunguka mji. Mfalme akaenda kuelekea upande wa Araba.
5 Men de Chaldeers magt jagade efter Konungen, och grepo honom på hedmarkene vid Jericho. Och alle krigsmännerna, som när honom voro, vordo förskingrade ifrå honom.
Lakini jeshi la Wakaldayo likamfuata mfalme Sedekia na kumchukua katika tambarare ya bonde la Mto Yoradani karibu na Yeriko. Jeshi lake lote lilitawanyika wakamwacha.
6 Men Konungen grepo de, och förde honom upp till Konungen af Babel till Riblath; och de sade en dom öfver honom.
Wakamkamata mfalme na kumleta mpaka kwa mfalme wa Babeli huko Ribla, ambapo walipitisha hukumu juu yake.
7 Och de slogo Zedekia barn ihjäl för hans ögon, och stungo Zedekia hans ögon ut, och bundo honom med kedjor, och förde honom till Babel.
Kama kwa watoto wa Sedekia, wakawachinja mbele ya macho yake. Kisha akamtoa macho Sedekia, wakamfunga pingu, na kumpeleka hadi Babeli.
8 På sjunde dagen i femte månadenom, det är nittonde året NebucadNezars, Konungens i Babel, kom NebusarAdan hofmästaren, Konungens tjenare i Babel, till Jerusalem;
Basi katika mwezi wa tano, katika siku ya saba ya mwezi, ambapo ulikuwa mwaka wa kumi na tisa wa utawala wa Nebukadreza mfalme wa Babeli, Nebuzaradani, mtumishi wa mfalme wa Babeli na amrijeshi wa walinzi wake, wakaja hadi Yerusalemu.
9 Och uppbrände Herrans hus, och Konungshuset, och all hus i Jerusalem, och all stor hus brände han upp med eld.
Akaichoma moto nyumba ya Yahwe, nyumba ya mfalme, na nyumba zote za Yeruselemu; pia kila jengo la muhimu katika mji akayachoma.
10 Och hela de Chaldeers magt, som med hofmästarenom var, bröt omkull murarna, som omkring Jerusalem voro.
Kama kwa kuta zote zilizoizunguka Yerusalemu, jeshi lote la Wababeli ambao walikuwa chini ya amrishi wa walinzi wakaziharibu.
11 Men det andra folket, som qvart var i stadenom, och de som till Konungen af Babel fallne voro, och det andra meniga folket, förde NebusarAdan hofmästaren bort.
Basi watu waliokuwa wamebaki ambao walikuwa wameondoka katika mji, wale waliokuwa wameasi kwa mfalme wa Babeli, na mabaki ya watu-Nebuzadani, amiri jeshi wa mlinzi, wakachukuliwa kwenda utumwani.
12 Och af de ringesta i landena lät hofmästaren blifva till vingårdsmän, och åkermän.
Lakini amiri jeshi wa mlinzi aliwaacha baadhi ya maskini wa nchi ili wafanye kazi kwenye shamba la mizabibu na kulima.
13 Men de kopparstodar i Herrans hus, och stolarna, och kopparhafvet, som i Herrans hus var, slogo de Chaldeer sönder, och förde kopparen till Babel.
Na zile nguzo za shaba ambazo zilikuwa kwenye nyumba ya Yahwe, na misimamio na bahari ya chuma ambayo ilikuwa kwenye nyumba ya Yahwe, Wakaldayo wakazivunja vipande vipande na kubeba shaba kuirudisha Babeli.
14 Och grytor, skoflar, knifvar, skedar, och all kopparkärile, dermed man tjente, togo de bort.
Masufuria, mabeleshi, makasi, vijiko, na vyombo vyote vya shaba ambavyo kuhani alivyokuwa amevitunza kwenye hekalu-Wakaldayo wakavichukua vyote.
15 Dertill tog hofmästaren pannor och bäcken, hvad af guld och silfver var;
Masufuria ya kuhamisha majivu na mabakuli ambayo yalikuwa yametengenezwa kwa dhahabu, na yale yaliyotengenezwa kwa fedha-yule nahodha wa mlinzi wa mfalme akavichukua pia.
16 Två stodar, ett haf, och de stolar, som Salomo hade göra låtit till Herrans hus; kopparen af all denna tygen stod icke till vägandes.
Zile nguzo mbili, ile bahari, na vile vitako ambavyo Suleimani alivitengeneza kwa ajili ya nyumba ya Yahwe shaba ya vyombo hivyo vyote haikuwa na uzani.
17 Aderton alnar hög var en stoden, och knappen derpå var ock af koppar, och tre alnar hög; och gjordarne, och granatäplen allt omkring knappen, var ock allt af koppar; vid samma sättet var ock den andre stoden med gjordar.
Urefu wa ile nguzo ya kwanza ulikuwa ridhaa kumi na nane, na kichwa cha shaba kilikuwa juu yake. Na urefu wa kichwa ulikuwa ridhaa tatu, pamoja na mapambo ya wavu na makomamanga yote yakizunguka kwenye hicho kichwa, vyote vilikuwa vimetengenezwa kwa shaba. Na ile nguzo nyingine ilikuwa vivyo hivyo kama ile ya kwanza pamoja na wavu wake.
18 Och hofmästaren tog Presten Seraja af första skiftet, och Presten Zephania af det andra skiftet, och tre dörravaktare,
Yule amiri jeshi wa mlinzi akamchukua Seraya kuhani mkuu, pamoja za Sefania, yule kuhani wa pili, na walinzi watatu wa kwenye lango.
19 Och en kamerer utu stadenom, som öfver krigsmännerna satt var, och fem män, som allstädes hade ståndit för Konungenom, och i stadenom funne voro, och Sopher, härhöfvitsmannen, som folket i landena strida lärde, och sextio män af landsfolkena, som i stadenom funne voro.
Kutoka mjini akamchukua mlinzi, afisa mmoja ambaye aliyekuwa msimamizi wa maaskari, na watu watano ambao walikuwa wakimshauri mfalme, ambao walikuwa bado katika mji. Pia alimchukua mfungwa wa afisa jeshi la mfalme, kwa ajili ya kuandika watu kwenye jeshi, pamoja na watu sitini muhimu kutoka hiyo nchi ambao walikuwa katika mji.
20 Dessa tog NebusarAdan hofmästaren, och förde dem till Konungen af Babel till Riblath.
Kisha Nebuzaradani, amiri wa mlinzi, akawachukua na kuwapeleka kwa mfalme Babeli huko Ribla.
21 Och Konungen i Babel slog dem ihjäl i Riblath, i de landena Hamath. Alltså vardt Juda bortförd utu sitt land.
Mfalme wa Babeli akawaua huko Ribla katika nchi ya Hamathi. Kwa njia hii, Yuda akaiacha nchi yake kwenda utumwani.
22 Men öfver det folk, som qvart blef i Juda land, som NebucadNezar, Konungen i Babel, qvart blifva lät, satte han Gedalja, Ahikams son, Saphans sons.
Na wale watu waliokuwa wamebakia katika nchi ya Yuda, wale ambao Nebukadreza mfalme wa Babeli aliwaacha, akamuweka Gedalia mwana wa Ahikamu, mwana wa Shafani, msimamizi wao.
23 Då nu allt krigsfolkets höfvitsmän och männerna hörde, att Konungen af Babel hade uppsatt Gedalja, kommo de till Gedalja i Mizpa, nämliga Ismael, Nethania son, och Johanan, Kareahs son, och Seraja, Thanhumeths son, den Netophathiten, och Jaesania, Maachati son, samt med deras män.
Kisha wakati maamiri wote wa majeshi, wao na watu wao, waliposikia kwamba mfalme wa Babeli amemfanya Gedalia kuwa liwali, wakaenda kwa Gedalia huko Mispa. Hawa watu walikuwa Ishmaeli mwana wa Nethania, Yohanani mwana wa Karea, Seraya mwana wa Tanhumethi Mnetofa, na Yezania mwana wa Mmaaka-wao na watu wao.
24 Och Gedalja svor dem, och deras män, och sade till dem: Frukter eder intet att vara de Chaldeers underdånar; blifver i landena, och varer Konungenom af Babel underdånige, så går eder väl.
Gedalia akafanya kiapo kwa watu wake na kuwaambia, “Msiwaogope Wakaldayo. Muishi katika nchi na kumtumikia mfalme wa Babeli, na itakuwa vema kwenu.”
25 Men i sjunde månadenom kom Ismael, Nethania son, Elisama sons, utaf Konungsliga slägt, och tio män med honom, och slogo Gedalja ihjäl; dertill de Judar och Chaldeer, som med honom voro i Mizpa.
Lakini ilitokea kwamba katika mwezi wa saba Ishmaeli mwana wa Nethania mwana wa Elishama, kutoka familia ya kifalme, wakaja na watu kumi na kumshambulia Gedalia. Gedalia akafa, pamoja na watu wa Yuda na Wababeli ambao walikuwa pamoja nae huko Mizpa.
26 Då reste sig upp allt folket, både små och store, och krigsöverstarna, och kommo in uti Egypten; förty de fruktade sig för de Chaldeer.
Kisha wale watu wote, kutoka chini kwenda juu, na maamiri wa jeshi, wakainuka na kwenda Misri, kwasababu walikuwa wanawaogopa Wababeli.
27 Uti sjunde och tretionde årena, sedan Jojachin, Juda Konung, bortförd var, på sjunde och tjugonde dagen i tolfte månadenom, hof EvilMerodach, Konungen i Babel, uti första årena af sitt rike, Jojachins, Juda Konungs, hufvud upp utu fängslehuset;
Ilitokea baadaye katika mwaka wa thelathini na saba wa utumwa wa Yekonia mfalme wa Yuda, katika mwezi wa kumi na mbili, siku ya ishirini na saba ya mwezi, Evil-merodaki mfalme wa Babeli akamtoa Yekonia mfalme wa Yuda kutoka gerezani. Hii ilitokea katika mwaka ambao Evil-Merodaki alipoanza kutawala.
28 Och talade vänliga med honom, och satte hans stol utöfver de Konungars stolar, som när honom voro i Babel;
Akaongea naye kwa ukarimu na kumpatia kiti kizuri zaidi kuliko kile cha wafalme wengine ambao walikuwa pamoja naye Babeli.
29 Och förvandlade hans fängelsekläder; och han åt alltid inför honom i alla sina lifsdagar;
Evil-Merodaki akamvua Yekonia nguo za gerezani,
30 Och satte honom före hans del, den man honom alltid gifva skulle af Konungenom, hvar dag, så länge han lefde.
na Yekinia akala siku zote kwenye meza ya mfalme katika maisha yake yote yaliyokuwa yamebakia.

< 2 Kungaboken 25 >