< 1 Kungaboken 7 >

1 Men uppå sitt hus byggde Salomo i tretton år, förr än det allt fullbygdt var, nämliga:
Ilimchukua Solomoni miaka kumi na mitatu kukamilisha ujenzi wa Jumba lake la kifalme.
2 Han byggde ett hus af Libanons skog, hundrade alnar långt, femtio alnar bredt, och tretio alnar högt. På det samma fyrhörnada lade han bottnen af cedrebräde, på cedrestodar å rad;
Alijenga Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni, urefu wake ulikuwa dhiraa 100, upana wake dhiraa hamsini na kimo chake dhiraa thelathini, likiwa na safu nne za nguzo za mierezi zikishikilia boriti za mierezi zilizorembwa.
3 Och der ofvanuppå en sal af ceder på samma stodar, hvilka voro fem och fyratio, ju femton i hvar rad.
Ilipauliwa kwa mierezi juu ya boriti zile zilizolala juu ya nguzo arobaini na tano, kumi na tano kwa kila safu.
4 Och voro fenster efter de tre radarna, tvärtemot hvartannat, tre emot tre;
Madirisha yake yaliwekwa juu kwa safu tatu, yakielekeana.
5 Och voro i deras bågar fyrahörnad.
Milango yote ilikuwa na miimo ya mstatili, ilikuwa upande wa mbele katika safu tatu, ikielekeana.
6 Han byggde ock ett förhus med stodar, femtio alnar långt, och tretio alnar bredt; och ändå ett förhus för desso, med stodar och tjocka, bjelkar,
Akajenga ukumbi wa nguzo, ambao urefu wake ulikuwa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa thelathini. Mbele ya jengo hilo kulikuwepo baraza. Mbele ya baraza kulikuwepo na nguzo na paa lililoningʼinia.
7 Och byggde desslikes ett förhus till domstolen, der man rättgång uti hålla skulle, och telde båda bottnarna med cedreträ;
Akajenga ukumbi wa kiti cha enzi, Ukumbi wa Hukumu, mahali ambapo angelitolea hukumu, akaufunika kwa mierezi kutoka sakafuni hadi darini.
8 Dertill sitt hus, der han uti bodde, i bakgårdenom bak vid förhuset, gjordt såsom de andra. Och gjorde han också ett hus såsom förhuset till Pharaos dotter, den Salomo till hustru tagit hade.
Kwenye jumba la kifalme ambamo angeliishi, aliiweka nyuma zaidi, ikiwa na mjengo wa aina moja na hiyo nyingine. Pia Solomoni akajenga jumba la kifalme linalofanana na huo ukumbi mkubwa kwa ajili ya binti Farao, aliyekuwa amemwoa.
9 Allt detta voro kostelige stenar huggne efter mått, och med såg skorne på alla sidor, ifrå grundvalen allt upp till taket; dertill ock utantill den store gården.
Ujenzi huu wote, kuanzia nje mpaka kwenye ua mkuu na kuanzia kwenye msingi hadi upenuni, ulifanywa kwa mawe ya ubora wa hali ya juu yaliyokuwa yamechongwa kwa vipimo na kusawazishwa kwa msumeno nyuso zake za ndani na za nje.
10 Grundvalarne voro af kosteliga och stora stenar, tio och åtta alnar stora;
Misingi iliwekwa kwa mawe makubwa yaliyo bora, yenye urefu wa dhiraa kumi na mengine yenye urefu wa dhiraa nane
11 Och deruppå kostelige huggne stenar efter mått, och ceder.
Sehemu za juu kulikuwepo na mawe yenye ubora wa hali ya juu, yaliyokatwa kwa vipimo na boriti za mierezi.
12 Men den store gården omkring hade tre radar huggen sten, och en rad af cedrebräde. Sammalunda ock gården till Herrans hus innantill, och förhuset till huset.
Ule ua mkuu ulizungukwa na ukuta wa safu tatu za mawe yaliyochongwa na safu moja ya boriti za mierezi zilizorembwa, kama ulivyokuwa ua wa ndani wa Hekalu la Bwana na baraza yake.
13 Och Konung Salomo sände bort, och lät hemta Hiram af Tyro,
Mfalme Solomoni akatuma watu Tiro kumleta Hiramu,
14 Ene enkos son af Naphthali slägte, och hans fader hade varit en man af Tyro; han var en mästare på koppar, full med visdom, förstånd och konst, till att arbeta allahanda kopparverk. Då han kom till Konung Salomo, gjorde han allt hans verk;
ambaye mama yake alikuwa mjane kutoka kabila la Naftali na baba yake alikuwa mtu wa Tiro tena fundi wa shaba. Hiramu alikuwa na ustadi wa hali ya juu na mzoefu katika aina zote za kazi ya shaba. Alikuja kwa Mfalme Solomoni na kufanya kazi zake zote alizopangiwa.
15 Och gjorde två kopparstodar, hvardera aderton alnar hög; och en tråd, tolf alnar lång, var måttet omkring hvarjo stodena;
Hiramu akasubu nguzo mbili za shaba, kila moja ikiwa na urefu wa dhiraa kumi na nane, kila nguzo ikiwa na mzingo wa dhiraa kumi na mbili kwa mstari.
16 Och gjorde två knappar, gjutna af koppar, till att sätta ofvanpå stoderna; och hvar knappen var fem alnar hög:
Pia alitengeneza mataji mawili ya shaba ya kusubu ili kuyaweka juu ya hizo nguzo; kila taji lilikuwa na kimo cha dhiraa tano kwenda juu.
17 Och på hvar knappen ofvanpå stoderna sju flätade gjordar såsom kedjor;
Wavu wa mikufu iliyosokotewa kwenye zile taji juu ya zile nguzo, saba kwa kila taji.
18 Och gjorde till hvar knappen två radar granatäple omkring, till ena gjord, der knappen med öfvertäckt vardt.
Akatengeneza makomamanga katika safu mbili kuzunguka kila wavu kuremba mataji yaliyo juu ya nguzo. Alifanya hivyo kwa kila nguzo.
19 Och knapparna voro såsom roser för förhusena, fyra alnar store.
Mataji yaliyokuwa juu ya nguzo kwenye baraza, yalikuwa katika umbo la yungiyungi, kimo chake ni dhiraa nne
20 Och de granatäplen i radarna omkring voro tuhundrad, ofvan och under på gjorden, som gick midt om knappen, om hvar knapp på båda stoderna.
Juu ya mataji ya zile nguzo mbili, juu ya ile sehemu yenye umbo kama bakuli, karibu na ule wavu, kulikuwa na yale makomamanga 200 katika safu kuzunguka pande zote.
21 Och han uppreste de stoderna inför förhusena af templet, och den som han satte på högra sidon, kallade han Jachin; och den som han satte på venstra sidon, kallade han Boas.
Hiramu akasimamisha nguzo kwenye baraza ya Hekalu. Nguzo ya upande wa kusini akaiita Yakini, na ile ya upande wa kaskazini Boazi.
22 Och det stod ofvanpå stoderna såsom roser. Alltså vardt fullkomnadt de stoders verk.
Mataji yaliyokuwa juu yalikuwa na umbo la yungiyungi. Hivyo kazi ya nguzo ikakamilika.
23 Och han gjorde ett haf gjutet, tio alnar bredt, ifrå den ena bräddene till den andra, rundt omkring; och fem alnar högt, och måttet rätt omkring var tretio alnar.
Hiramu akasubu Bahari ya chuma, yenye umbo la mviringo, ya dhiraa kumi kutoka ukingo hadi ukingo na kimo cha dhiraa tano. Mzunguko wake ulikuwa dhiraa thelathini.
24 Och om det samma hafvet, det tio alnar bredt var, gick en krusering utmed dess brädd, allt omkring hafvet; den kruseringen var gjuten i två radar.
Chini ya ukingo, ilizungukwa na maboga, kumi kwenye kila dhiraa moja. Maboga yalikuwa yamesubiwa katika safu mbili ili kuwa kitu kimoja na hiyo bahari.
25 Och det stod på tolf oxar; tre af dem vände sig norrut, tre vesterut, tre söderut, och tre österut; och hafvet der ofvanuppå; så att all bakdelen af dem var inunder.
Bahari iliwekwa juu ya mafahali kumi na wawili, watatu wakielekea kaskazini, watatu wakielekea magharibi, watatu wakielekea kusini na watatu wakielekea mashariki. Bahari iliwekwa juu yao na sehemu zao za nyuma zilielekeana.
26 Tjockheten af thy var en tvärhand; och brädden deruppå var såsom brädden på en bägare, såsom en utsprungen ros; och tutusende bath gick deruti.
Ilikuwa na unene wa nyanda nne na ukingo wake ulifanana na ukingo wa kikombe, kama ua la yungiyungi iliyochanua. Iliweza kuchukua bathi 2,000.
27 Han gjorde ock tio kopparstolar; hvardera fyra alnar lång och bred, och tre alnar hög.
Pia akatengeneza vitako kumi vya shaba vinavyoweza kuhamishika, kila kimoja kilikuwa na urefu wa dhiraa nne, upana dhiraa nne na kimo chake dhiraa tatu
28 Och var stolen så gjord, att han hade sidor emellan listor.
Hivi ndivyo vile vitako vilivyotengenezwa: Vilikuwa na mbao za pembeni zilizoshikamanishwa na mihimili.
29 Och på sidomen emellan listorna voro lejon, oxar och Cherubim, och sidorna, der lejonen, oxarna och Cherubim voro uppå, hade listor ofvan och nedan, och fötter deruppå.
Juu ya mbao kati ya hiyo mihimili kulikuwa na simba, mafahali na makerubi, pia kwenye mihimili yake. Juu na chini ya simba na mafahali kulikuwa kumesokotewa taji za kufuliwa.
30 Och hvar stolen hade fyra kopparhjul med kopparaxlar. Och uppå fyra hörnen voro gjutna styltor, hvar emot den andra stödjandes under kettilen.
Kila kitako kilikuwa na magurudumu manne ya shaba, na vyuma vya katikati vya kuyazungusha hayo magurudumu na kila kimoja kilikuwa na sinia kwenye vishikizo vinne vya taji iliyosubiwa kila upande.
31 Men halsen midt på stolen var en aln hög och trind; half annan aln bred, och på halsenom voro bulor i planarna, hvilke fyrkant voro, och icke runde.
Ndani ya kitako kulikuwa na nafasi ya wazi iliyokuwa na umbile la mviringo lenye kina cha dhiraa moja. Nafasi hii ya wazi ilikuwa ya mviringo, pamoja na kitako chake ilikuwa dhiraa moja na nusu. Kuzunguka huo mdomo wake kulitiwa nakshi. Papi za vitako zilikuwa mraba na si za mviringo.
32 Men de fyra hjul stodo nedan under sidorna, och axlarna åt hjulen voro vid stolen; hvart hjulet var halfannor aln högt;
Magurudumu manne yalikuwa chini ya papi, na vyuma vya katikati vya kuzungushia magurudumu hayo vilikuwa vimeunganishwa kwenye kitako. Kipenyo cha kila gurudumu kilikuwa dhiraa moja na nusu.
33 Och voro hjul såsom vagnshjul; och deras axlar, naf, ekrar och löter, voro allt gjutne.
Magurudumu yalitengenezwa kama ya magari ya vita ya kukokotwa, vyuma vya katikati vya magurudumu, duara zake, matindi yake na vikombe vyake vyote vilikuwa vya kusubu.
34 Och de fyra styltor, på de fyra hörnen af hvar stolen, voro ock alla fasta vid stolen.
Kila kitako kilikuwa na mikono minne, moja kwenye kila pembe, ukitokeza kutoka kwenye kitako.
35 Och på halsenom, ofvanuppå stolen en half aln högt allt omkring, voro listor och sidor på stolenom.
Juu ya kitako kulikuwepo na utepe wa mviringo wenye kina cha nusu dhiraa. Vishikio na papi vilishikamana upande wa juu wa kitako.
36 Och han lät grafva på det slätt var, på samma sidor och listor, Cherubim, lejon och palmträ, det ena efter det andra allt omkring.
Alitia nakshi za makerubi, simba na miti ya mitende juu ya uso wa vishikio na juu ya papi, katika kila nafasi iliyopatikana, pamoja na mataji yaliyosokotwa kuzunguka pande zote.
37 Vid det sättet gjorde han de tio gjutna stolar; enahanda mått och rum var på dem allom.
Hivi ndivyo Hiramu alivyotengeneza vile vitako kumi. Vyote vilikuwa vya kusubu kwenye kalibu za kufanana kwa vipimo na kwa umbo.
38 Och han gjorde tio kopparkettlar, så att fyratio bath gingo uti hvar kettilen; och den var fyra alnar stor, och på hvar stol var en kettil.
Kisha akatengeneza masinia kumi ya shaba, kila moja likiwa na ujazo wa bathi arobaini, yakiwa na kipenyo cha dhiraa nne kila sinia moja kwa kila kimoja ya vile vitako kumi.
39 Och han satte fem stolar på högra sidone i huset, och de andre fem på venstra; men hafvet satte han rätt framföre på högra sidone, söderut.
Aliweka vitako vitano upande wa kusini wa Hekalu na vingine vitano upande wa kaskazini. Akaweka ile bahari upande wa kusini, katika pembe ya kusini ya Hekalu.
40 Och Hiram gjorde desslikes grytor, skoflar, bäcken; och fullkomnade så all verk, som Konung Salomo göra lät i Herrans hus;
Pia akatengeneza masinia, masepetu na mabakuli ya kunyunyizia. Kwa hiyo Huramu akakamilisha kazi zote katika Hekalu la Bwana kama vile Mfalme Solomoni alikuwa amemwagiza, yaani:
41 Nämliga de två stoder, och de två runda knappar ofvanuppå de två stodar, och de två vridna gjordar, till att betäcka de två runda knappar på stoderna;
nguzo mbili; mataji mawili yenye umbo la bakuli juu ya hizo nguzo; nyavu mbili za kupamba hayo mataji mawili yenye umbo la bakuli juu ya hizo nguzo;
42 Och de fyrahundrad granatäple på de två vridna gjordar, ju två rader granatäple på en gjord, till att betäcka de två runda knapparna på stoderna;
makomamanga 400 kwa ajili ya hizo nyavu mbili (safu mbili za makomamanga kwa kila wavu, yakipamba hayo mataji mawili yenye umbo la bakuli juu ya hizo nguzo);
43 Dertill de tio stolar, och de tio kettlar der ofvanuppå;
vitako kumi pamoja na masinia yake kumi;
44 Och hafvet, och de tolf oxar under hafvet;
ile Bahari ya chuma na yale mafahali kumi na wawili chini yake;
45 Och de grytor, skoflar och bäcken; och all denna kärilen, som Hiram gjorde åt Konung Salomo till Herrans hus, voro utaf klar koppar.
masufuria, masepetu na mabakuli ya kunyunyizia. Vyombo hivi vyote ambavyo Huramu alimtengenezea Mfalme Solomoni kwa ajili ya Hekalu la Bwana vilikuwa vya shaba iliyongʼarishwa.
46 I den ängden vid Jordan lät Konungen gjuta dem, i den lermarkene emellan Succoth och Zarthan.
Mfalme akaamuru wavisubu katika kalibu ya udongo wa mfinyanzi katika uwanda wa Yordani ulio kati ya Sukothi na Sarethani.
47 Och Salomo lät all dessa kärilen ovägne blifva; derföre att kopparen var så mycken.
Solomoni akaviacha vitu hivi vyote bila kupima uzani wake, kwa sababu vilikuwa vingi sana hivi kwamba uzito wa shaba haungekadirika.
48 Och gjorde Salomo all tyg, som Herrans hus tillhörde; nämliga ett gyldene altar, ett gyldene bord, der skådobröd på ligga skulle;
Solomoni pia akatengeneza samani zote zilizokuwa ndani ya Hekalu la Bwana: madhabahu ya dhahabu; meza ya dhahabu za kuweka mikate ya Wonyesho;
49 Fem ljusastakar på högra, och fem ljusastakar på den venstra sidone, framför choren, af klart guld, med gyldene blommor, lampor och ljusanäpor;
vinara vya taa vya dhahabu safi (vitano upande wa kuume na vitano upande wa kushoto, mbele ya Patakatifu pa Patakatifu); kazi ya maua ya dhahabu na taa na makoleo;
50 Dertill skålar, fat, bäcken, skedar och pannor, af klart guld. Och voro dörrahängslorna på dörrarna åt innersta huset, som var det aldrahelgasta, och åt templets husdörr, af guld.
masinia ya dhahabu safi, mikasi ya kusawazishia tambi, mabakuli ya kunyunyizia, vyano na vyetezo; na bawaba za dhahabu kwa ajili ya milango ya chumba cha ndani sana, yaani Patakatifu pa Patakatifu, na pia kwa ajili ya milango ya ukumbi mkuu wa Hekalu.
51 Alltså vardt fullkomnadt allt verk, som Konung Salomo gjorde till Herrans hus. Och Salomo bar ditin det som hans fader David helgat hade, af silfver och guld, och käril, och lade det in uti Herrans hus skatt.
Hivyo Mfalme Solomoni alipomaliza kazi ya Hekalu la Bwana, akaviingiza ndani vile vitu ambavyo Daudi baba yake alikuwa ameviweka wakfu: yaani fedha, dhahabu na samani; kisha akaviweka katika hazina za Hekalu la Bwana.

< 1 Kungaboken 7 >