< 1 Krönikeboken 5 >
1 Rubens barn, första Israels sons, ty han var förste sonen; men derföre, att han sins fäders säng besmittade, vardt hans förstfödslorätt gifven Josephs barnom, Israels sons; och han vardt icke räknad till förstfödslona.
Wana wa Reubeni mzaliwa wa kwanza wa Israeli (yeye alikuwa mzaliwa wa kwanza, lakini kwa kuwa alikinajisi kitanda cha baba yake, haki zake za mzaliwa wa kwanza walipewa wana wa Yosefu mwana wa Israeli. Hivyo hakuorodheshwa kwenye orodha ya ukoo wao kulingana na haki yake ya kuzaliwa.
2 Ty Juda, som mägtig var ibland sina bröder, honom vardt Förstadömet för honom gifvet, och Joseph förstfödslorätten.
Na ingawa Yuda alikuwa na nguvu zaidi ya ndugu zake wote, na mtawala alitoka kwake, haki za mzaliwa wa kwanza zilikuwa za Yosefu.)
3 Så äro nu Rubens, första Israels sons, barn: Hanoch, Pallu, Hezron och Charmi.
Wana wa Reubeni mzaliwa wa kwanza wa Israeli walikuwa: Hanoki, Palu, Hesroni na Karmi.
4 Joels barn voro: Semaja. Hans son var Gog. Hans son var Simei.
Wazao wa Yoeli walikuwa: Shemaya mwanawe, Gogu mwanawe; Shimei mwanawe,
5 Hans son var Micha. Hans son var Reaja. Hans son var Baal.
Mika mwanawe, Reaya mwanawe, Baali mwanawe,
6 Hans son var Beera, hvilken ThiglathPilneser, Konungen i Assyrien, bortförde fången; han är en Förste ibland de Rubeniter.
na Beera mwanawe, ambaye Tiglath-Pileseri mfalme wa Ashuru alimchukua kwenda uhamishoni. Beera alikuwa kiongozi wa Wareubeni.
7 Men hans bröder i deras ätter, då de i deras börd räknade vordo, hade Jegiel och Zacharia för höfvitsmän.
Jamaa zao kulingana na koo zao, walioorodheshwa kwa kufuata koo zao kama ifuatavyo: Yeieli aliyekuwa mkuu wao, Zekaria,
8 Och Bela, Asas son, Serna sons, Joels sons, han bodde i Aroer, och intill Nebo och BaalMeon;
Bela mwana wa Azazi, mwana wa Shema, mwana wa Yoeli. Hao waliishi katika eneo kuanzia Aroeri mpaka Nebo na Baal-Meoni.
9 Och bodde emot öster intill man kommer till öknena vid den älfvena Phrath; förty deras boskap var mycken i Gileads land.
Kwa upande wa mashariki walienea hadi pembeni mwa jangwa linaloenea mpaka kwenye Mto Frati, kwa sababu mifugo yao ilikuwa imeongezeka huko Gileadi.
10 Och i Sauls tid förde de örlig emot de Hagariter, så att de föllo genom desses hand, och bodde i deras hyddor, in mot alla den östra ängden Gilead.
Wakati wa utawala wa Mfalme Sauli, walipigana vita dhidi ya Wahagari, wakaanguka kwa mikono yao, kisha wakaishi katika mahema ya Wahagari katika eneo lote la mashariki ya Gileadi.
11 Gads barn bodde tvärtöfver ifrå dem, uti de landena Basan, allt intill Salcha:
Wagadi waliishi jirani nao katika nchi ya Bashani, mpaka Saleka.
12 Joel den främste, Sapham den andre, Jaenai och Saphat i Basan.
Yoeli ndiye alikuwa mkuu wao, Shafamu wa pili, na wakafuata Yanai na Shafati, huko Bashani.
13 Och deras bröder i deras fäders hus voro: Michael, Mesullam, Seba, Jorai, Jaecan, Sia och Eber, de sju.
Ndugu zao kulingana na koo zao walikuwa saba: Mikaeli, Meshulamu, Sheba, Yorai, Yakani, Zia na Eberi.
14 Desse äro Abihails barn, Huri sons, Jaroahs sons, Gileads sons, Michaels sons, Jesisai sons, Jahdo sons, Bus sons.
Hawa walikuwa ndio wana wa Abihaili mwana wa Huri, mwana wa Yaroa, mwana wa Gileadi, mwana wa Mikaeli, mwana wa Yeshishai, mwana wa Yahdo, mwana wa Buzi.
15 Ahi, Abdiels son, Guni sons, var en öfverste uti deras fäders hus;
Ahi mwana wa Abdieli, mwana wa Guni, alikuwa ndiye kiongozi wa jamaa yao.
16 Och bodde uti Gilead i Basan, och i dess döttrar, och i alla Sarons förstäder, allt intill dess ändar.
Wagadi waliishi Gileadi, huko Bashani pamoja na vijiji vilivyoizunguka, pia katika nchi yote ya malisho ya Sharoni kote walikoenea.
17 Desse vordo alle räknade i Jothams, Juda Konungs, och Jerobeams, Israels Konungs tid.
Yote haya yaliwekwa katika kumbukumbu za ukoo wao wakati wa utawala wa Yothamu, mfalme wa Yuda na Yeroboamu mfalme wa Israeli.
18 Rubens barn, de Gaditers, och de halfva slägtenes Manasse, voro stridsamme män, som sköld och svärd föra och båga spänna kunde, och förfarne till att strida; de voro fyra och fyratio tusend, och sjuhundrad och sextio, som i här drogo.
Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase walikuwa na watu mashujaa 44,760 waliokuwa wameandaliwa kwa ajili ya vita: watu wenye nguvu, hodari wa kutumia ngao na upanga, mashujaa wa kutumia upinde, waliokuwa tayari kwa ajili ya kazi hiyo.
19 Och då de stridde med de Hagariter, hulpo dem Jetur, Naphis och Nodab;
Walipigana vita dhidi ya Wahagari, Yeturi, Nafishi na Nodabu.
20 Och gåfvo de Hagariter i deras händer, och allt det som med dem var; förty de ropade till Gud i stridene, och han bönhörde dem; ty de trodde till honom.
Walisaidiwa katika kupigana nao, Mungu akawatia Wahagari pamoja na wote walioungana nao mikononi mwao, kwa sababu walimlilia Mungu wakati wa vita. Alijibu maombi yao, kwa sababu walimtegemea.
21 Och de förde bort deras boskap, femtiotusend camelar, tuhundrad och femtio tusend får, tutusend åsnar, och hundradtusend menniskors själar.
Walitwaa mifugo ya Wahagari: ngamia 50,000, kondoo 250,000, punda 2,000. Pia wakateka watu 100,000,
22 Och der föllo månge såre; ty striden var af Gudi. Och de bodde i deras stad allt intill den tiden de fångne vordo.
na wengine wengi waliuawa kwa sababu vita vilikuwa ni vya Mungu. Nao waliendelea kuikalia nchi hiyo mpaka wakati wa uhamisho.
23 De halfva slägtenes Manasse barn bodde i de landena, ifrå Basan allt intill BaalHermon och Senir, och det berget Hermon, och de voro månge.
Idadi ya nusu ya kabila la Manase walikuwa wengi sana, Wakakaa kuanzia Bashani hadi Baal-Hermoni, yaani mpaka Seniri na mlima Hermoni.
24 Och desse voro höfvitsmän till deras fäders hus: Epher, Jisei, Eliel, Asriel, Jeremia, Hodavia, Jahdiel; väldige, mägtige män, och namnkunnige höfvitsmän uti deras fäders husom.
Hawa ndio waliokuwa viongozi wa jamaa za kabila hilo: Eferi, Ishi, Elieli, Azrieli, Yeremia, Hodavia na Yahdieli. Walikuwa askari shujaa watu maarufu, viongozi wa jamaa zao.
25 Och då de förtogo sig emot deras fäders Gud, och i horeri gingo efter de folks gudar der i landena, som Gud för dem förgjort hade,
Lakini hawakuwa waaminifu kwa Mungu wa baba zao, nao wakafanya ukahaba kwa miungu ya mataifa, ambayo Mungu alikuwa ameyaangamiza mbele yao.
26 Uppväckte Israels Gud Phuls anda, Konungens i Assyrien, och ThiglathPilnesers anda, Konungens i Assyrien, och förde bort de Rubeniter, Gaditer och den halfva slägtena Manasse, och lät komma dem till Halah och Hober och Hara, och till den älfvena Gosan, allt intill denna dag.
Kwa hiyo Mungu wa Israeli akaiamsha roho ya Pulu, mfalme wa Ashuru (ambaye pia alijulikana kama Tiglath-Pileseri), ambaye aliwachukua Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase kwenda uhamishoni. Akawapeleka huko Hala, Habori, Hara na mto Gozani, ambako wamekaa mpaka leo.