< 1 Krönikeboken 27 >
1 Men Israels barn efter sitt tal voro höfdingar öfver fäderna, och öfver tusende, och öfver hundrade; och ämbetsmän, som på Konungen vaktade, efter deras ordning, till att draga till och frå, hvar i sin månad, i hvar månad om året. Hvart skiftet hade fyra och tjugu tusend.
Hii ndiyo orodha ya Waisraeli: viongozi wa jamaa, majemadari wa maelfu, majemadari wa mamia na maafisa wao, waliomtumikia mfalme kwa lolote lililohusu vikosi vya jeshi vilivyokuwa zamu mwezi baada ya mwezi katika mwaka mzima. Kila kikosi kimoja kilikuwa na watu 24,000.
2 Öfver första skiftet i första månadenom var Jasabeam, Sabdiels son; och i hans skifte voro fyra och tjugu tusend.
Msimamizi wa kikosi cha kwanza kwa mwezi wa kwanza alikuwa Yashobeamu mwana wa Zabdieli. Kulikuwa na watu 24,000 katika kikosi chake.
3 Men af Perez barnom var den öfverste öfver alla höfvitsmännerna i härarna i första månadenom.
Yeye alikuwa mzao wa Peresi, na mkuu wa maafisa wote wa jeshi kwa mwezi wa kwanza.
4 Öfver det skiftet i den andra månaden var Dodai den Ahohiten; och Mikloth var Förste öfver hans skifte; och i hans skifte voro fyra och tjugu tusend.
Msimamizi wa kikosi kwa mwezi wa pili alikuwa Dodai Mwahohi. Miklothi ndiye alikuwa kiongozi wa kikosi chake. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
5 Den tredje härhöfvitsmannen i tredje månadenom, den öfverste, var Benaja, Jojada Prestens son; och i hans skifte voro fyra och tjugu tusend.
Jemadari wa kikosi cha tatu kwa mwezi wa tatu alikuwa Benaya mwana wa kuhani Yehoyada. Ndiye alikuwa mkuu wa kikosi chake kilichokuwa na watu 24,000.
6 Denne är Benaja, den hjelten ibland tretio, och öfver tretio; och hans skifte var under hans son Ammisabad.
Huyu ndiye yule Benaya aliyekuwa shujaa miongoni mwa wale Thelathini na ndiye alikuwa juu yao hao Thelathini. Mwanawe Amizabadi ndiye alikuwa mkuu katika kikosi chake.
7 Den fjerde i fjerde månadenom var Asahel, Joabs broder, och efter honom Sebadia, hans son; och i hans skifte voro fyra och tjugu tusend.
Jemadari wa nne kwa mwezi wa nne alikuwa Asaheli nduguye Yoabu, mwanawe Zebadia ndiye aliingia mahali pake kwenye uongozi. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
8 Den femte i femte månadenom var Samhuth den Jisrahiten; och i hans skifte voro fyra och tjugu tusend.
Jemadari wa kikosi cha tano kwa mwezi wa tano alikuwa Shamhuthi Mwizrahi. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
9 Den sjette i sjette månadenom var Ira, Ikkes den Thekoitens son; och i hans skifte voro fyra och tjugu tusend.
Jemadari wa kikosi cha sita kwa mwezi wa sita alikuwa Ira, mwana wa Ikeshi Mtekoa. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
10 Den sjunde i sjunde månadenom var Helez den Peloniten, af Ephraims barn; och i hans skifte voro fyra och tjugu tusend.
Jemadari wa kikosi cha saba kwa mwezi wa saba alikuwa Helesi Mpeloni wa Waefraimu. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
11 Den åttonde i åttonde månadenom var Sibbechai den Husathiten, af de Sarhiter; och i hans skifte voro fyra och tjugu tusend.
Jemadari wa nane kwa mwezi wa nane, alikuwa Sibekai Mhushathi wa Wazera. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
12 Den nionde i nionde månadenom var Abieser den Anthothiten, af Jemini barn; och i hans skifte voro fyra och tjugu tusend.
Jemadari wa tisa kwa mwezi wa tisa alikuwa Abiezeri Mwanathothi wa Wabenyamini. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
13 Den tionde i tionde månadenom var Maharai den Netophathiten, af de Serahiter; och i hans skifte voro fyra och tjugu tusend.
Jemadari wa kumi kwa mwezi wa kumi alikuwa Maharai Mnetofathi wa Wazera. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
14 Den ellofte i ellofte månadenom var Benaja den Pirgathoniten, af Ephraims barn; och i hans skifte voro fyra och tjugu tusend.
Jemadari wa kumi na moja kwa mwezi wa kumi na moja alikuwa Benaya Mpirathoni wa Waefraimu. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
15 Den tolfte i tolfte månadenom var Heldai den Netophathiten, af Athniel; och i hans skifte voro fyra och tjugu tusend.
Jemadari wa kumi na mbili kwa mwezi wa kumi na mbili alikuwa Heldai Mnetofathi kutoka jamaa ya Othnieli. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
16 Öfver Israels slägter voro desse: För de Rubeniter var Förste Elieser, Sichri son; för de Simeoniter var Sephatia, Maacha son;
Maafisa waliokuwa wanaoongoza makabila ya Israeli walikuwa: Kwa Wareubeni: Eliezeri mwana wa Zikri; kwa Wasimeoni: Shefatia mwana wa Maaka;
17 För de Leviter var Hasabia, Kemuels son; för de Aaroniter var Zadok;
kwa Walawi: Hashabia mwana wa Kemueli; kwa Aroni: Sadoki;
18 För Juda var Elihu af Davids bröder; för Isaschar var Omri, Michaels son;
kwa Yuda: Elihu, nduguye Daudi; kwa Waisakari: Omri mwana wa Mikaeli;
19 För Sebulon var Jismaja, Obadja son; för Naphthali var Jerimoth, Asriels son;
kwa Wazabuloni: Ishmaya mwana wa Obadia; kwa Wanaftali: Yeremothi mwana wa Azrieli;
20 För Ephraims barn var Hosea, Asasia son; för den halfva slägtene Manasse var Joel, Phedaja son;
kwa Waefraimu: Hoshea mwana wa Azazia; kwa nusu ya kabila la Manase: Yoeli mwana wa Pedaya;
21 För den halfva slägtene Manasse i Gilead var Jiddo, Zacharia son; för BenJamin var Jaasiel, Abners son;
kwa nusu nyingine ya kabila la Manase huko Gileadi: Ido mwana wa Zekaria; kwa Wabenyamini: Yaasieli mwana wa Abneri;
22 För Dan var Asarel, Jerohams son Detta äro de Förstar för Israels slägter.
kwa Wadani: Azareli mwana wa Yerohamu. Hao ndio waliokuwa maafisa wa makabila ya Israeli.
23 Men David tog intet tal af dem som voro tjugu åra, och der för nedan; ty Herren hade sagt, att han skulle föröka Israel såsom stjernorna på himmelen.
Daudi hakuwahesabu watu waliokuwa chini ya miaka ishirini, kwa sababu Bwana alikuwa ameahidi kuwafanya Israeli kuwa wengi kama nyota za angani.
24 Men Joab, ZeruJa son, hade begynt räkna, och lyktade det icke; ty en vredo kom fördenskull öfver Israel, derföre kom det talet icke uti Konung Davids Chrönico.
Yoabu mwana wa Seruya alianza kuwahesabu watu lakini hakumaliza. Kwa sababu ya kuwahesabu watu, hasira ya Mungu iliwaka juu ya Israeli, nayo hiyo hesabu yao haikuingizwa katika kitabu cha kumbukumbu za Mfalme Daudi.
25 Öfver Konungens håfvor var Asmaveth, Adiels son; och öfver de håfvor på landena, i städer, byar och slott, var Jonathan, Ussija son.
Azmawethi mwana wa Adieli ndiye alikuwa msimamizi wa hazina za mfalme. Msimamizi wa hazina katika mashamba, miji, vijiji na kwenye ngome alikuwa Yonathani mwana wa Uzia.
26 Öfver åkermännerna till landsbruket var Esri, Chelubs son.
Ezri mwana wa Kelubu alikuwa msimamizi wa wafanyakazi waliolima katika mashamba.
27 Öfver vingårdarna var Simei den Ramathiten; öfver vinkällarena och vinet var Sabdi den Siphmiten.
Shimei Mramathi alikuwa msimamizi wa mashamba ya mizabibu. Zabdi Mshifmi alikuwa msimamizi wa zabibu, utengenezaji na uhifadhi wa divai katika mapipa makubwa.
28 Öfver oljogårdarna, och mulbärträ i markene var BaalHanan den Gederiten; öfver oljona var Joas.
Baal-Hanani Mgederi ndiye alikuwa mwangalizi wa mashamba ya mfalme ya mizeituni na mikuyu katika tambarare za vilima vya magharibi. Yoashi alikuwa msimamizi wa ghala za mafuta ya zeituni.
29 Öfver den boskap, som i bet var i Saron, var Sithrai den Saroniten; men öfver den boskap i dalomen var Saphat, Adlai son.
Shitrai Msharoni alikuwa msimamizi wa makundi ya ngʼombe waliojilisha huko Sharoni. Shafati mwana wa Adlai alikuwa msimamizi wa yale makundi ya ngʼombe yaliyokuwa makondeni.
30 Öfver camelarna var Obil den Ismaeliten; öfver åsnarna var Jehdeja den Meronothiten.
Obili Mwishmaeli alikuwa msimamizi wa ngamia. Yedeya Mmeronothi alikuwa msimamizi wa punda.
31 Öfver fåren var Jasis den Hagariten, Desse voro alle öfverstar öfver Konung Davids ägodelar.
Yazizi Mhagri alikuwa msimamizi wa makundi ya kondoo na mbuzi. Hawa wote ndio waliokuwa maafisa wasimamizi wa mali alizokuwa nazo Mfalme Daudi.
32 Men Jonathan, Davids faderbroder, var rådgifvare, hofmästare och canceller; Jehiel, Hachmoni son, var när Konungens barnom.
Yonathani mjomba wa Daudi alikuwa mshauri, mtu mwenye ufahamu mkubwa na mwandishi. Yehieli mwana wa Hakmoni alikuwa akiwahudumia wana wa mfalme.
33 Achitophel var ock Konungens rådgifvare; Husai den Arachiten var Konungens vän.
Ahithofeli alikuwa mshauri wa mfalme. Hushai Mwariki alikuwa rafiki wa mfalme.
34 Efter Achitophel var Jojada, Benaja son, och AbJathar; men Joab var Konungens härhöfvitsman.
Baada ya Ahithofeli, Yehoyada mwana wa Benaya aliingia mahali pake kama mshauri wa mfalme pamoja na Abiathari. Yoabu alikuwa ndiye jemadari wa majeshi ya mfalme.