< 1 Krönikeboken 23 >

1 Alltså gjorde David Salomo, sin son, till Konung öfver Israel, då han gammal, och af lefvande mätt var.
Daudi alipokuwa mzee aliyeshiba siku, akamfanya Solomoni mwanawe kuwa mfalme juu ya Israeli.
2 Och David församlade alla öfverstar i Israel, och Presterna och Leviterna,
Pia akawakusanya pamoja viongozi wote wa Israeli, pamoja na makuhani na Walawi.
3 Att man skulle räkna Leviterna, ifrå tretio år och derutöfver; och deras tal var, ifrå hufvud till hufvud, det starke män voro, åtta och tretio tusend;
Walawi waliokuwa na umri wa miaka thelathini au zaidi walihesabiwa, nayo hesabu ya wanaume ilikuwa 38,000.
4 Af hvilkom voro fyra och tjugu tusend, som drefvo arbetet på Herrans hus; och sextusend ämbetsmän och domare;
Daudi akasema, “Miongoni mwa hawa, 24,000 watasimamia kazi ya Hekalu la Bwana na 6,000 watakuwa maafisa na waamuzi,
5 Och fyratusend dörravaktare; och fyratusend lofsångare Herranom med strängaspel, som jag till lofsång gjort hade.
na 4,000 watakuwa mabawabu, na wengine 4,000 watamsifu Bwana kwa ala za uimbaji nilizotoa kwa ajili ya kusudi hilo.”
6 Och David gjorde en ordning ibland Levi barn, nämliga ibland Gerson, Kehath och Merari.
Daudi akawagawa Walawi katika makundi kufuatana na wana wa Lawi: Gershoni, Kohathi na Merari.
7 Då Gersoniter voro: Laedan och Simei.
Wana wa Wagershoni walikuwa wawili: Ladani na Shimei.
8 Laedans barn: Den förste Jehiel, Setam och Joel, de tre.
Wana wa Ladani walikuwa watatu: Yehieli wa kwanza, Zethamu na Yoeli.
9 Men Simei barn voro: Selomith, Hasiel och Haran, de tre. Desse voro de ypperste ibland fäderna af Laedan.
Wana wa Shimei walikuwa watatu: Shelomothi, Hazieli na Harani. Hawa watatu walikuwa viongozi wa jamaa za Ladani.
10 Voro också desse Simei barn: Jahath, Sina, Jeus och Beria. Desse fyra voro ock Simei barn.
Nao wana wa Shimei walikuwa wanne: Yahathi, Zina, Yeushi na Beria.
11 Jahath var den förste, Sisa den andre. Men Jeus och Beria hade icke mång barn; derföre vordo de räknade för ens faders hus.
Yahathi alikuwa wa kwanza na Ziza wa pili, lakini Yeushi na Beria hawakuwa na wana wengi; kwa hiyo walihesabiwa kama jamaa moja, wakapewa wajibu kwa pamoja.
12 Kehaths barn voro: Amram, Jizear, Hebron och Ussiel, de fyra.
Wana wa Kohathi walikuwa wanne: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.
13 Amrams barn voro: Aaron och Mose. Men Aaron vardt afskild, så att han vardt helgad till det aldrahelgasta, han och hans söner, till evig tid, till att röka för Herranom, och till att tjena och välsigna i Herrans Namn i evig tid;
Wana wa Amramu walikuwa: Aroni na Mose. Aroni waliwekwa wakfu, yeye na wazao wake milele, wawe wakiweka wakfu vitu ambavyo ni vitakatifu mno, kutoa dhabihu mbele za Bwana, kuhudumu mbele zake na kutamka baraka katika Jina la Bwana milele.
14 Och Mose, den Guds mansens, barn vordo nämnde ibland de Leviters slägte.
Wana wa Mose mtu wa Mungu walihesabiwa kama sehemu ya kabila la Lawi.
15 Mose barn voro: Gersom och Elieser.
Wana wa Mose walikuwa: Gershomu na Eliezeri.
16 Gersoms barn: Den förste var Sebuel.
Wazao wa Gershomu: Shebueli alikuwa wa kwanza.
17 Eliesers barn: Den förste var Rehabia. Och Elieser hade inga annor barn; men Rehabia barn voro mycket flere.
Wazao wa Eliezeri: Rehabia alikuwa wa kwanza. Eliezeri alikuwa na mwana mmoja tu, lakini wana wa Rehabia walikuwa wengi sana.
18 Jizears barn voro: Selomith den förste.
Wana wa Ishari: Shelomithi alikuwa wa kwanza.
19 Hebrons barn voro: Jeria den förste, Amaria den andre, Jahasiel den tredje, och Jekameam den fjerde.
Wana wa Hebroni walikuwa: Yeria alikuwa wa kwanza, wa pili Amaria, wa tatu Yahazieli, na wa nne Yekameamu.
20 Ussiels barn voro: Micha den förste, och Jissija den andre.
Wana wa Uzieli walikuwa: Mika wa kwanza na Ishia wa pili.
21 Merari barn voro: Maheli och Musi. Maheli barn voro: Eleazar och Kis.
Wana wa Merari walikuwa: Mahli na Mushi. Wana wa Mahli walikuwa: Eleazari na Kishi.
22 Men Eleazar blef död, och hade inga söner, utan döttrar; och Kis barn, deras bröder, togo dem.
Eleazari akafa bila ya kuwa na wana: alikuwa na binti tu. Binamu zao, wana wa Kishi, wakawaoa.
23 Musi barn voro: Maheli, Eder och Jeremoth, de tre.
Wana wa Mushi: Mahli, Ederi na Yeremothi; wote walikuwa watatu.
24 Detta äro Levi barn i deras faders hus, och de ypperste af fäderna, som räknade vordo, efter namnens tal efter hufvuden, hvilke gjorde de sysslor i ämbeten i Herrans hus, ifrå tjugu år, och derutöfver.
Hawa walikuwa wazao wa Lawi kwa jamaa zao. Wakuu wa jamaa kama walivyoandikwa kwa majina yao na kuhesabiwa kila mmoja, yaani, wenye uwezo wa kufanya kazi kuanzia miaka ishirini au zaidi, waliohudumu katika Hekalu la Bwana.
25 Ty David sade: Herren Israels Gud hafver gifvit sino folke ro, och skall bo i Jerusalem till evig tid.
Kwa maana Daudi alikuwa amesema, “Kwa vile Bwana, Mungu wa Israeli amewapa watu wake raha na amekuja kuishi Yerusalemu milele,
26 Leviterna behöfde ock icke bära tabernaklet, med all dess redskap, efter deras ämbete;
Walawi hawahitaji tena kubeba Maskani wala chombo chochote cha utumishi wake.”
27 Utan, efter Davids yttersta ord, vordo Levi barn räknade ifrå tjugu år, och derutöfver;
Kulingana na maagizo ya mwisho ya Daudi, Walawi waliohesabiwa ni wale wa kuanzia umri wa miaka ishirini au zaidi.
28 Att de skulle stå under Aarons barnas händer, till att tjena i Herrans hus, i gårdenom, och till kistorna, och till reningen, och till allahanda helgedom, och till alla ämbetens sysslor i Guds hus;
Wajibu wa Walawi ulikuwa kuwasaidia wazao wa Aroni kuhudumu katika Hekalu la Bwana: Kuwa wasimamizi wa nyua, vyumba vya pembeni, kutakasa vyombo vitakatifu na utendaji mwingine wowote katika nyumba ya Mungu.
29 Och till skådobröd, till semlomjöl, till spisoffer, till osyrade kakor, till pannor, till halster, och till all vigt och mått;
Walikuwa wasimamizi wa mikate iliyowekwa mezani, unga kwa ajili ya sadaka za nafaka, mikate isiyotiwa chachu, uokaji na uchanganyaji, pamoja na vipimo vyote vya wingi na ukubwa.
30 Och till att stå om morgonen, och tacka och lofva Herran; om aftonen desslikes;
Pia ulikuwa wajibu wao kila asubuhi kumshukuru na kumsifu Bwana. Iliwapasa pia kufanya hivyo jioni
31 Och till att offra Herranom all bränneoffer på Sabbatherna, nymånadom och högtidom, efter talet och sättet, alltid för Herranom;
na wakati wowote sadaka za kuteketezwa zilipotolewa kwa Bwana siku za Sabato na kwenye sikukuu za Mwezi Mwandamo na katika sikukuu nyingine zilizoamriwa. Iliwapasa kuhudumu mbele za Bwana mara kwa mara kwa idadi maalum na kwa namna waliyokuwa wamepewa maelekezo.
32 Att de skulle taga vara på vaktena vid vittnesbördsens tabernakel, och helgedomens; och Aarons barnas, deras bröders, till att tjena i Herrans hus.
Hivyo Walawi wakafanya wajibu wao katika Hema la Kukutania, katika Mahali Patakatifu chini ya uongozi wa ndugu zao wazao wa Aroni, kwa ajili ya utumishi katika Hekalu la Bwana.

< 1 Krönikeboken 23 >