< Tito 3 >
1 Wakumbushe watu kuwastahi watawala na wenye mamlaka, kuwatii na kuwa tayari kwa kila namna kutenda mambo yote mema.
Rappelle aux fidèles le devoir d’être soumis aux magistrats et aux autorités, de leur obéir, d’être prêts à toute bonne œuvre,
2 Waambie wasimtukane mtu yeyote; bali waishi kwa amani na masikizano, wawe daima wapole kwa kila mtu.
de ne dire du mal de personne, d’éviter les contestations, mais d’être condescendants, et de témoigner la plus grande douceur à l’égard de tous les hommes.
3 Maana, wakati mmoja sisi tulikuwa wapumbavu, wakaidi na wapotovu. Tulikuwa watumwa wa tamaa na anasa za kila aina. Tuliishi maisha ya uovu na wivu; watu walituchukia nasi tukawachukia.
Car nous aussi, nous étions autrefois insensés, indociles, égarés, esclaves de toutes sortes de convoitises et de jouissances, vivant dans la malignité et l’envie, dignes de haine, et nous haïssant les uns les autres.
4 Lakini wakati wema na upendo wa Mungu, Mwokozi wetu, ulipofunuliwa,
Mais lorsque Dieu notre Sauveur a fait paraître sa bonté et son amour pour les hommes,
5 alituokoa. alituokoa si kwa sababu ya jambo lolote jema tulilotenda sisi, bali alituokoa kwa sababu ya huruma yake, kwa njia ya Roho Mtakatifu anayetujalia tuzaliwe upya na kuwa na maisha mapya kwa kutuosha kwa maji.
il nous a sauvés, non à cause des œuvres de justice que nous faisions, mais selon sa miséricorde, par le bain de la régénération et en nous renouvelant par le Saint-Esprit,
6 Mungu alitumiminia Roho Mtakatifu bila kipimo kwa njia ya Yesu Kristo, Mwokozi wetu,
qu’il a répandu sur nous largement par Jésus-Christ notre Sauveur,
7 ili kwa neema yake tupate kukubaliwa kuwa waadilifu na kuupokea uzima wa milele tunaoutumainia. (aiōnios )
afin que, justifiés par sa grâce, nous devenions héritiers de la vie éternelle selon notre espérance. (aiōnios )
8 Jambo hili ni kweli. Ninakutaka uyatilie mkazo mambo haya, ili wale wanaomwamini Mungu, wawe na hamu ya kuutumia wakati wao katika kutenda mema, ambayo ni mambo mazuri na ya manufaa kwa watu.
C’est là une parole certaine, et je désire que tu affirmes ces choses, afin que ceux qui croient en Dieu s’appliquent à être les premiers dans la pratique des bonnes œuvres. C’est ce qui est bon et utile aux hommes.
9 Lakini jiepushe na ubishi wa kipumbavu, ugomvi na mabishano juu ya Sheria. Mambo hayo hayana faida yoyote na ni ya bure tu.
Quant aux questions folles, aux généalogies, aux querelles, aux disputes relatives à la Loi, évite-les, car elles sont inutiles et vaines.
10 Mtu anayesababisha mafarakano mpe onyo la kwanza na la pili, kisha achana naye.
Pour celui qui fomente des divisions, après un premier et un second avertissement, éloigne-le de toi,
11 Wajua kwamba mtu wa namna hiyo amepotoka kabisa, na dhambi zake zathibitisha kwamba amekosea.
sachant qu’un tel homme est entièrement perverti, et qu’il est un pécheur condamné de son propre jugement.
12 Baada ya kumtuma kwako Artema au Tukiko, fanya bidii kuja Nikopoli unione, maana nimeamua kukaa huko wakati wa majira ya baridi.
Lorsque je t’aurai envoyé Artémas ou Tychique, hâte-toi de venir me rejoindre à Nicopolis, car j’ai résolu d’y passer l’hiver.
13 Jitahidi kumsaidia mwana sheria Zena na Apolo ili waweze kuanza ziara zao na uhakikishe kwamba wana kila kitu wanachohitaji.
Pourvois avec soin au voyage de Zénas, le docteur de la loi, et d’Apollos, en sorte que rien ne leur manque.
14 Ni lazima watu wetu wajifunze kuutumia wakati wao katika kutenda mema ili wasaidie katika mahitaji ya kweli, na maisha yao yawe ya kufaa.
De plus que les nôtres aussi apprennent à se porter aux bonnes œuvres, de manière à subvenir aux besoins urgents, afin qu’ils ne soient pas sans fruits.
15 Watu wote walio pamoja nami wanakusalimu. Wasalimu rafiki zetu katika imani. Nawatakieni nyote neema ya Mungu.
Tous ceux qui sont avec moi te saluent; salue ceux qui nous aiment dans la foi. Que la grâce soit avec vous tous. Amen!