< Tito 1 >
1 Mimi Paulo, mtumishi wa Mungu na mtume wa Yesu Kristo naandika. Mimi nimechaguliwa kuijenga imani ya wateule wa Mungu na kuwaongoza waufahamu ukweli wa dini yetu,
Ikalata iji jihumile kulyune ne Paulo ne m'bombi ghwa Nguluve, kange ne n'sung'hua ghwa Yeesu Kilisite. Une nisung'ilue nivalungike avabaghulua va Nguluve mulwitiko namuvukagusi uvwa kyang'ani vuno vukuvalongosia mumaghendele amimike.
2 ambayo msingi wake ni tumaini la kupata uzima wa milele. Mungu ambaye hasemi uongo, alituahidia uzima huo kabla ya mwanzo wa nyakati, (aiōnios )
valinuluhuvio ulwa vumi uvwa kisila na kusila vuno uNguluve alyalaghile kuhuma iisi ye jikyale kupelua umwene naijova uvudesi. (aiōnios )
3 na wakati ufaao ulipowadia, akaudhihirisha katika ujumbe wake. Mimi nilikabidhiwa ujumbe huo nuutangaze kufuatana na amri ya Mungu, Mwokozi wetu.
Mun'siki ghwa Nguluve ghuno ghufikile, alyavonesisie ilisio lyake mu mhola jinoalyamelile une kudalikila. jikanighanile kuvomba ndiki kululaghilo lya Nguluve mpoki ghwitu.
4 Ninakuandikia wewe Tito, mwanangu wa kweli katika imani tunayoshiriki. Nakutakia neema na amani kutoka kwa Mungu Baba, na kutoka kwa Kristo Yesu, Mkombozi wetu.
kwa Tiito, umwana ghwa lweli mu lwitiko lwitu. ulusungu, ikisa nulutengano kuhuma kwa Nguluve Nhaata nu Yesu Kiisite mpoki ghwitu.
5 Nilikuacha Krete ili urekebishe yale mambo ambayo hayakuwa yamekamilika bado, na kuwateua wazee wa kanisa katika kila mji. Kumbuka maagizo yangu:
mu uluo nikakulekile kuti, usitende sooni sinasikao kamilike na kuvika avalolesi va tembile mumakaja ghoni ndavule finonikakulaghiile.
6 mzee wa kanisa anapaswa kuwa mtu asiye na hatia; aliye na mke mmoja tu, na watoto wake wanapaswa kuwa waumini, wasiojulikana kuwa wakorofi au wakaidi.
umulolesi ghwa tembile avaghile kuva kisila lupiko, mughosi ghwa n'dala jumo, unyavana vitiki vanonavilolela na vasila lwitiki.
7 Maana kwa vile kiongozi wa kanisa ni mkurugenzi wa kazi ya Mungu, anapaswa kuwa mtu asiye na hatia. Asiwe mwenye majivuno, mwepesi wa hasira, mlevi, mkorofi au mchoyo.
luvaghile kuvalolesi ndavule umwimilisi ghwa likaaja lwa Nguluve, alekaghe piva nulupiko. nangavisaghe munhu ghwa njeghelo au juno naikujisigha, nangavisaghe munhu ghwa kutengulisia uvuhovesi kange nagavisaghe mhojofu.
8 Anapaswa kuwa mkarimu na anayependa mambo mema. Anapaswa kuwa mtu mtaratibu, mwadilifu, mtakatifu na mwenye nidhamu.
looli avisaghe ntengeleli, junoikela inofu, avisaghe nyaluhala lunolukwiliine, mugholofu juno ikum'bingilila uNguluve nyakughela.
9 Ni lazima ashike kikamilifu ujumbe ule wa kuaminika kama unavyofundishwa. Ndivyo atakavyoweza kuwatia wengine moyo kwa mafundisho ya kweli na kuyafichua makosa ya wale wanaoyapinga mafundisho hayo.
junoiwesia kukwimilia imbulanisio sa lweli sinosivulanisivue, neke awesie kuvakangasia mu mbulanisio inono juno iwesia kukuvavunga vooni vanovikunkana.
10 Maana, wako watu wengi, hasa wale walioongoka kutoka dini ya Kiyahudi, ambao ni wakaidi, wanaowapotosha wengine kwa upumbavu wao.
ulwakuva kulinavahosi vinga, vinga vala vano navakundi. amasio ghavanave gheghakijasu, visyanga na kukuvalongosia avanhu muvusyovi.
11 Lazima kukomesha maneno yao, kwani wanavuruga jumuiya nzima kwa kufundisha mambo ambayo hawapaswi kufundisha; wanafanya hivyo kwa nia mbaya ya kupata faida ya fedha.
luvaghile kukuvasigha avanhu ndavule avuo. vivulanisia ghala ghano naghavavaghile kuluvumbulilo lwa soni nakunangania ikaja soni.
12 Hata mmoja wa manabii wao, ambaye naye pia ni Mkrete, alisema: “Wakrete, husema uongo daima; ni kama wanyama wabaya, walafi na wavivu!”
jumonga muvanave, umunhu unyaluhala alyatiile,”avakelete valinuvudesi vusila vusililo, vahene fikanu, voolo na vanyamwojo,”
13 Naye alitoboa ukweli kwa sababu hiyo, unapaswa kuwakaripia vikali, ili wawe na imani kamilifu.
injovele iji je ja lweli, lino uvasighe ku ngufu neke kuti wawesie kujova ilweli mu lwitiko.
14 Wasiendelee kushikilia hadithi tupu za Kiyahudi na maagizo ya kibinadamu yanayozuka kwa watu walioukataa ukweli.
uleke kupulikisia ifipango fino nafyalweli ifya kiyahudi ni ndaghilo sa vanhu, vano vavulekile uvunyakyang'ani.
15 Kila kitu ni safi kwa watu walio safi; lakini hakuna chochote kilicho safi kwa wale waliochafuliwa na wasioamini, maana dhamiri na akili zao zimechafuliwa.
kuvanhu voni vano valogholofu, ifinu fyoni fivalasivue, looli kuvala voni vano vanavano na valamafu kange navitiki, ifinhu fyoni filamafu. ulwakuva amasaghe ghave nuluvumbulilo lwave lulamafu.
16 Watu kama hao hujidai kwamba wanamjua Mungu, lakini kwa matendo yao humkana. Ni watu wa kuchukiza mno na wakaidi, hawafai kwa jambo lolote jema.
vikujova veene kuti vamanyile unguluve, neke kumaghendele ghaave vikun'kaana. avuo vahosi kange navitiki. navanoghile nambe mumbombo jimonga inofu.