< Tito 1 >
1 Mimi Paulo, mtumishi wa Mungu na mtume wa Yesu Kristo naandika. Mimi nimechaguliwa kuijenga imani ya wateule wa Mungu na kuwaongoza waufahamu ukweli wa dini yetu,
Paul, a servant of God and an apostle of Jesus Christ, appointed to further the faith of God's chosen ones and the knowledge of the truth that is in accordance with godliness,
2 ambayo msingi wake ni tumaini la kupata uzima wa milele. Mungu ambaye hasemi uongo, alituahidia uzima huo kabla ya mwanzo wa nyakati, (aiōnios )
in the hope of eternal life, which God, who does not lie, promised before time began; (aiōnios )
3 na wakati ufaao ulipowadia, akaudhihirisha katika ujumbe wake. Mimi nilikabidhiwa ujumbe huo nuutangaze kufuatana na amri ya Mungu, Mwokozi wetu.
in his own time he revealed his word through the preaching with which I was entrusted by the command of God our Savior;
4 Ninakuandikia wewe Tito, mwanangu wa kweli katika imani tunayoshiriki. Nakutakia neema na amani kutoka kwa Mungu Baba, na kutoka kwa Kristo Yesu, Mkombozi wetu.
to Titus, my true child in our common faith: Grace, mercy, and peace from God the Father and the Lord Jesus Christ our Savior.
5 Nilikuacha Krete ili urekebishe yale mambo ambayo hayakuwa yamekamilika bado, na kuwateua wazee wa kanisa katika kila mji. Kumbuka maagizo yangu:
The reason I left yoʋ in Crete was for yoʋ to put in order what remained to be done and to appoint elders in every town, as I directed yoʋ.
6 mzee wa kanisa anapaswa kuwa mtu asiye na hatia; aliye na mke mmoja tu, na watoto wake wanapaswa kuwa waumini, wasiojulikana kuwa wakorofi au wakaidi.
An elder must be above reproach, the husband of one wife, with faithful children who are not rebellious and cannot be accused of debauchery.
7 Maana kwa vile kiongozi wa kanisa ni mkurugenzi wa kazi ya Mungu, anapaswa kuwa mtu asiye na hatia. Asiwe mwenye majivuno, mwepesi wa hasira, mlevi, mkorofi au mchoyo.
For an overseer, as God's steward, must be above reproach, not self-willed, not quick-tempered, not given to wine, not violent, not greedy for sordid gain,
8 Anapaswa kuwa mkarimu na anayependa mambo mema. Anapaswa kuwa mtu mtaratibu, mwadilifu, mtakatifu na mwenye nidhamu.
but hospitable, a lover of goodness, sensible, just, holy, and self-controlled,
9 Ni lazima ashike kikamilifu ujumbe ule wa kuaminika kama unavyofundishwa. Ndivyo atakavyoweza kuwatia wengine moyo kwa mafundisho ya kweli na kuyafichua makosa ya wale wanaoyapinga mafundisho hayo.
holding firmly to the trustworthy message as it has been taught, so that he can encourage others with sound doctrine and refute those who contradict it.
10 Maana, wako watu wengi, hasa wale walioongoka kutoka dini ya Kiyahudi, ambao ni wakaidi, wanaowapotosha wengine kwa upumbavu wao.
For there are many rebellious people, full of meaningless talk and deception, especially those of the circumcision faction.
11 Lazima kukomesha maneno yao, kwani wanavuruga jumuiya nzima kwa kufundisha mambo ambayo hawapaswi kufundisha; wanafanya hivyo kwa nia mbaya ya kupata faida ya fedha.
They must be silenced, because they are ruining entire households by teaching what they ought not to teach, for the sake of sordid gain.
12 Hata mmoja wa manabii wao, ambaye naye pia ni Mkrete, alisema: “Wakrete, husema uongo daima; ni kama wanyama wabaya, walafi na wavivu!”
One of their very own prophets said, “Cretans are always liars, evil beasts, and lazy gluttons.”
13 Naye alitoboa ukweli kwa sababu hiyo, unapaswa kuwakaripia vikali, ili wawe na imani kamilifu.
This testimony is true. Therefore rebuke them sharply, so that they may become sound in the faith,
14 Wasiendelee kushikilia hadithi tupu za Kiyahudi na maagizo ya kibinadamu yanayozuka kwa watu walioukataa ukweli.
not paying any attention to Jewish myths or the commandments of men who turn away from the truth.
15 Kila kitu ni safi kwa watu walio safi; lakini hakuna chochote kilicho safi kwa wale waliochafuliwa na wasioamini, maana dhamiri na akili zao zimechafuliwa.
To the pure, all things are pure; but to those who are defiled and do not believe, nothing is pure. In fact, both their minds and their consciences are defiled.
16 Watu kama hao hujidai kwamba wanamjua Mungu, lakini kwa matendo yao humkana. Ni watu wa kuchukiza mno na wakaidi, hawafai kwa jambo lolote jema.
They profess to know God, but by their works they deny him. They are detestable, disobedient, and have proven themselves to be unqualified for any good work.