< Warumi 1 >
1 Kutoka kwangu mimi Paulo, mtumishi wa Kristo Yesu, na mtume niliyeteuliwa na kuitwa kwa ajili ya kuhubiri Habari Njema ya Mungu.
Paul slave Christ Jesus called apostle to separate toward gospel God
2 Hapo kale, Mungu aliwaahidia watu hii Habari Njema kwa njia ya manabii wake katika Maandiko Matakatifu.
which to promise through/because of the/this/who prophet it/s/he in/on/among a writing holy
3 Hii Habari Njema inamhusu Mwana wa Mungu, Bwana wetu Yesu Kristo, ambaye mintarafu ubinadamu wake, alikuwa mzawa wa Daudi;
about the/this/who son it/s/he the/this/who to be out from seed: offspring David according to flesh
4 mintarafu utakatifu wake wa kimungu, alithibitishwa kwa uwezo mkuu kwamba ni Mwana wa Mungu kwa kufufuliwa kutoka wafu.
the/this/who to determine son God in/on/among power according to spirit/breath: spirit holiness out from resurrection dead Jesus Christ the/this/who lord: God me
5 Kwa njia yake, mimi nimepewa neema ya kuwa mtume, ili kwa ajili yake niwaongoze watu wa mataifa yote wapate kuamini na kutii.
through/because of which to take grace and apostleship toward obedience faith in/on/among all the/this/who Gentiles above/for the/this/who name it/s/he
6 Ninyi ni miongoni mwa watu hao; mmeitwa muwe watu wake Yesu Kristo.
in/on/among which to be and you called Jesus Christ
7 Basi, ninawaandikia ninyi nyote mlioko Roma ambao Mungu anawapenda, akawateua muwe watu wake. Nawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo.
all the/this/who to be in/on/among Rome beloved God called holy: saint grace you and peace away from God father me and lord: God Jesus Christ
8 Awali ya yote, namshukuru Mungu wangu kwa njia ya Yesu Kristo kwa ajili yenu nyote, kwa sababu imani yenu inasikika duniani kote.
first on the other hand to thank the/this/who God me through/because of Jesus Christ (about *N(k)O*) all you that/since: since the/this/who faith you to proclaim in/on/among all the/this/who world
9 Mungu, ambaye ninamtumikia kwa moyo wangu wote katika kuhubiri Habari Njema ya Mwanae, ni shahidi wangu kwamba ninawakumbukeni
witness for me to be the/this/who God which to minister in/on/among the/this/who spirit/breath: spirit me in/on/among the/this/who gospel the/this/who son it/s/he as/when unceasingly remembrance you to do/make: do always upon/to/against the/this/who prayer me
10 daima katika sala zangu. Namwomba Mungu akipenda, anipatie nafasi nzuri ya kuja kwenu sasa.
to pray if how already once/when to get along well in/on/among the/this/who will/desire the/this/who God to come/go to/with you
11 Kwa maana ninatamani sana kuwaoneni ili nipate kuwagawieni zawadi ya kiroho na kuwaimarisha.
to long for for to perceive: see you in order that/to one to share gift you spiritual toward the/this/who to establish you
12 Ndiyo kusema, tutaimarishana: imani yenu itaniimarisha mimi, na yangu itawaimarisha ninyi.
this/he/she/it then to be to encourage in/on/among you through/because of the/this/who in/on/among one another faith you and/both and I/we
13 Ndugu zangu, nataka mjue kwamba mara nyingi nilikusudia kuwatembeleeni, lakini mpaka sasa nimezuiwa. Ningependa kupata mafanikio mema kati yenu kama nilivyopata kati ya watu wa mataifa mengine.
no to will/desire then you be ignorant brother that/since: that often to plan/present to come/go to/with you and to prevent until the/this/who come in order that/to one fruit to have/be and in/on/among you as/just as and in/on/among the/this/who remaining Gentiles
14 Ninalo jukumu kwa watu wote, waliostaarabika na wasiostaarabika, wenye elimu na wasio na elimu.
Greek, Gentile and/both and barbarian wise and/both and foolish debtor to be
15 Ndiyo maana ninatamani pia kuihubiri Habari Njema kwenu ninyi mlioko huko Roma.
thus(-ly) the/this/who according to I/we eager and you the/this/who in/on/among Rome to speak good news
16 Sioni aibu kutangaza Habari Njema; yenyewe ni nguvu ya Mungu inayowaokoa wote wanaoamini: Wayahudi kwanza, na wasio Wayahudi pia.
no for be ashamed of the/this/who gospel (the/this/who Christ *K*) power for God to be toward salvation all the/this/who to trust (in) Jew and/both first and Greek, Gentile
17 Kwa maana Habari Njema inaonyesha wazi jinsi Mungu anavyowakubali watu kuwa waadilifu; jambo hili hufanyika kwa imani, tangu mwanzo mpaka mwisho. Kama ilivyoandikwa: “Mwadilifu kwa imani ataishi.”
righteousness for God in/on/among it/s/he to reveal out from faith toward faith as/just as to write the/this/who then just out from faith to live
18 Ghadhabu ya Mungu imedhihirishwa kutoka mbinguni dhidi ya uasi na uovu wote wa binadamu ambao kwa njia zao mbaya wanaupinga ukweli usijulikane.
to reveal for wrath God away from heaven upon/to/against all ungodlinessness and unrighteousness a human the/this/who the/this/who truth in/on/among unrighteousness to hold back/fast
19 Kwa maana, yote yanayoweza kujulikana juu ya Mungu ni wazi kwao; maana Mungu mwenyewe ameyadhirisha.
because the/this/who acquainted with the/this/who God clear to be in/on/among it/s/he the/this/who God for it/s/he to reveal
20 Tangu Mungu alipoumba ulimwengu, uwezo wake wa milele na uungu wake, ingawa havionekani kwa macho, vinafahamika wazi. Watu wanaweza kuyajua mambo hayo kutokana na vitu hivyo alivyoumba Mungu. Kwa hiyo hawana njia yoyote ya kujitetea! (aïdios )
the/this/who for invisible it/s/he away from creation world the/this/who workmanship to understand to perceive the/this/who and/both eternal it/s/he power and divinity toward the/this/who to exist it/s/he inexcusable (aïdios )
21 Ingawa wanajua kuna Mungu, lakini hawampi heshima anayostahili, wala hawamshukuru. Badala yake, fikira zao zimekuwa batili na akili zao tupu zimejaa giza.
because to know the/this/who God no as/when God to glorify or to thank but to make futile in/on/among the/this/who reasoning it/s/he and to darken the/this/who senseless it/s/he heart
22 Wanajidai kuwa wenye hekima, kumbe ni wapumbavu.
to claim to exist wise be foolish
23 Wanaacha kumwabudu Mungu aishiye milele, na badala yake, wanaabudu sanamu zilizo mfano wa binadamu ambaye hufa, mfano wa wanyama, ndege, au wanyama watambaao.
and to change the/this/who glory the/this/who incorruptible God in/on/among likeness image perishable a human and bird and four-footed and reptile
24 Kwa sababu hiyo, Mungu amewaacha wafuate tamaa mbaya za mioyo yao na kufanyiana mambo ya aibu kwa miili yao.
therefore (and *k*) to deliver it/s/he the/this/who God in/on/among the/this/who desire the/this/who heart it/s/he toward impurity the/this/who to dishonor the/this/who body it/s/he in/on/among (it/s/he *N(k)O*)
25 Wanaubadili ukweli juu ya Mungu kwa uongo; wanaheshimu na kuabudu kiumbe badala ya Muumba mwenyewe, ambaye ndiye astahiliye sifa milele! Amina. (aiōn )
who/which to exchange the/this/who truth the/this/who God in/on/among the/this/who lie and to worship and to minister the/this/who creation from/with/beside the/this/who to create which to be praiseworthy toward the/this/who an age: eternity amen (aiōn )
26 Kwa hiyo, Mungu amewaacha wafuate tamaa mbaya. Hata wanawake wanabadili matumizi yanayopatana na maumbile.
through/because of this/he/she/it to deliver it/s/he the/this/who God toward passion dishonour the/this/who and/both for female it/s/he to exchange the/this/who natural use toward the/this/who from/with/beside nature
27 Nao wanaume hali kadhalika, wanaacha kufuata matumizi ya maumbile ya mume na mke wakawakiana tamaa wao kwa wao. Wanaume wanafanyiana mambo ya aibu, na hivyo wanajiletea wenyewe adhabu wanayostahili kwa vitendo vyao viovu.
similarly and/both and the/this/who male to release: permit the/this/who natural use the/this/who female be enflamed in/on/among the/this/who lust it/s/he toward one another male in/on/among male the/this/who indecency to workout/produce and the/this/who recompense which be necessary the/this/who error it/s/he in/on/among themself to get back
28 Kwa vile watu walikataa kumtambua Mungu, Mungu amewaacha katika fikira zao potovu, wakafanya yale ambayo hawangestahili kufanya.
and as/just as no to test the/this/who God to have/be in/on/among knowledge to deliver it/s/he the/this/who God toward failing mind to do/make: do the/this/who not be fit
29 Wamejaa kila aina ya uovu, dhuluma, ulafi na ufisadi. Wamejaa wivu, uuaji, ugomvi, udanganyifu na nia mbaya; husengenya,
to fulfill all unrighteousness (sexual sin *K*) evil greediness evil full envy murder quarrel deceit malice gossip
30 na kusingiziana; ni watu wa kuchukiza kwa Mungu, wafidhuli, wenye kiburi na majivuno; hodari sana katika kutenda mabaya, na hawawatii wazazi wao;
slanderous God-hating insolent man arrogant braggart inventor evil/harm: evil parent disobedient
31 hawana dhamiri, hawatimizi ahadi zao, hawana wema wala huruma kwa wengine.
senseless untrustworthy unfeeling (irreconcilable *K*) merciless
32 Wanajua kwamba Sheria ya Mungu yasema kwamba watu wanaoishi mithili hiyo, wanastahili kifo. Zaidi ya hayo, siyo tu kwamba wanafanya mambo hayo wao wenyewe, bali hata huwapongeza wale wanaofanya mambo hayohayo.
who/which the/this/who righteous act the/this/who God to come to know that/since: that the/this/who the/this/who such as this to do/require worthy death to be no alone it/s/he to do/make: do but and to agree to the/this/who to do/require