< Warumi 8 >

1 Kwa hiyo, sasa hakuna hukumu kwa wale ambao katika maisha yao wameungana na Kristo.
There is therefore now no condemnation to those who are in Christ Jesus.
2 Maana, sheria ya Roho iletayo uzima kwa kuungana na Kristo Yesu imenikomboa kutoka katika sheria ya dhambi na kifo.
For the law of the Spirit of life in Christ Jesus has set you free from the law of sin and of death.
3 Mungu ametekeleza jambo lile ambalo Sheria haikuweza kutekeleza kwa sababu ya udhaifu w binadamu. Mungu alimtuma Mwanae akiwa mwenye mwili sawa na miili yetu sisi wenye dhambi, ili aikabili dhambi, na kwa mwili huo akaiangamiza dhambi.
For what the law could not do, in that it was weak through the flesh, God did, sending his own Son in the likeness of sinful flesh and for sin, he condemned sin in the flesh;
4 Mungu alifanya hivyo kusudi matakwa ya haki ya Sheria yatekelezwe kikamilifu ndani yetu sisi ambao tunaishi, si kwa nguvu za kibinadamu, bali kwa nguvu ya Roho.
so that the requirement of the law might be fulfilled in us, who do not walk according to the flesh but according to the Spirit.
5 Maana, wale wanaoishi kufuatana na matakwa ya mwili, hutawaliwa na fikira za mwili. Lakini wale wanaoishi kufuatana na matakwa ya Roho Mtakatifu, hutawaliwa na fikira za Roho.
For those who live according to the flesh set their minds on the things of the flesh, but those who live according to the Spirit, the things of the Spirit.
6 Fikira za mwili huleta kifo; fikira za Roho huleta uzima na amani.
For the mind set on the flesh is death, but the mind set on the Spirit is life and peace;
7 Maana, mwenye kutawaliwa na fikira za mwili ni adui wa Mungu; haitii sheria ya Mungu, wala hawezi kuitii.
because the mind set on the flesh is hostile towards God, for it does not submit to God's law; indeed, it cannot.
8 Watu wanaotii matakwa ya mwili hawawezi kumpendeza Mungu.
And those who are in the flesh cannot please God.
9 Lakini ninyi hamuishi kufuatana na matakwa ya mwili, bali kufuatana na matakwa ya Roho, ikiwa Roho wa Mungu anaishi ndani yenu. Yeyote asiye na Roho wa Kristo, huyo si wake Kristo.
But you are not in the flesh but in the Spirit, if it is so that the Spirit of God dwells in you. But if anyone does not have the Spirit of Christ, he does not belong to him.
10 Lakini kama Kristo yumo ndani yenu, ingawa miili yenu itakufa kwa sababu ya dhambi, kwenu Roho ndiye uhai kwa sababu mmekubaliwa kuwa waadilifu.
And if Christ is in you, the body is dead because of sin, but the Spirit gives life because of righteousness.
11 Ikiwa Roho wa Mungu aliyemfufua Kristo kutoka wafu anaishi ndani yenu, basi huyo aliyemfufua Kristo kutoka wafu ataipa uzima miili yenu yenye hali ya kufa; atafanya hivyo kwa njia ya Roho wake akaaye ndani yenu.
But if the Spirit of him who raised up Jesus from the dead dwells in you, he who raised up Christ from the dead will also give life to your mortal bodies through his Spirit who dwells in you.
12 Hivyo basi, ndugu zangu, tunalo jukumu, lakini si la kuishi kufuatana na maumbile ya kibinadamu.
So then, brothers, we have no obligation to the flesh, to live after the flesh.
13 Kwa maana, kama mkiishi kufuatana na matakwa ya maumbile ya kibinadamu, hakika mtakufa. Lakini, kama kwa njia ya Roho mnayaua matendo yenu maovu, basi, mtaishi.
For if you live after the flesh, you must die; but if by the Spirit you put to death the deeds of the body, you will live.
14 Wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu ni watoto wa Mungu.
For as many as are led by the Spirit of God, these are sons of God.
15 Kwa maana, Roho mliyempokea si Roho mwenye kuwafanya ninyi watumwa na kuwatia tena hofu; sivyo, bali mmempokea Roho mwenye kuwafanya ninyi watoto wa Mungu, na kwa nguvu ya huyo Roho, sisi tunaweza kumwita Mungu, “Aba,” yaani “Baba!”
For you did not receive the spirit of bondage again to fear, but you received the Spirit of adoption, by whom we cry, "Abba. Father."
16 Naye Roho mwenyewe anajiunga na roho zetu na kuthibitisha kwamba sisi ni watoto wa Mungu.
The Spirit himself testifies with our spirit that we are children of God;
17 Basi, kwa vile sisi ni watoto wa Mungu, tutapokea baraka zote Mungu alizowawekea watu wake, na tutashiriki urithi huo pamoja na Kristo; maana, tukiyashiriki mateso yake Kristo, tutaushiriki pia utukufu wake.
and if children, then heirs; heirs of God and fellow heirs with Christ; if indeed we suffer with him, that we may also be glorified with him.
18 Naona kuwa mateso ya wakati huu wa sasa si kitu kamwe kama tukiyafananisha na ule utukufu utakaodhihirishwa kwetu.
For I consider that the sufferings of this present time are not worthy to be compared with the glory which will be revealed to us.
19 Viumbe vyote vinatazamia kwa hamu Mungu awadhihirishe watoto wake.
For the creation waits with eager expectation for the sons of God to be revealed.
20 Kwa maana, viumbe viliwekwa katika hali ya kutojiweza kabisa, si kwa hiari yao, ila vilifanywa hivyo kwa mapenzi ya Mungu. Hata hivyo yapo matumaini,
For the creation was subjected to futility, not of its own will, but because of him who subjected it, in hope
21 maana hivyo viumbe navyo vitaokolewa kutoka katika utumwa wa uharibifu, vishiriki uhuru mtukufu wa watoto wa Mungu.
that the creation itself also will be delivered from the bondage of decay into the glorious freedom of the children of God.
22 Kwa maana tunajua kwamba mpaka hivi sasa, viumbe vyote vinalia kwa maumivu kama ya kujifungua mtoto.
For we know that the whole creation groans and suffers with labor pains together until now.
23 Wala si hivyo viumbe peke yake, bali hata sisi tulio na huyo Roho, aliye wa kwanza wa zawadi za Mungu; sisi pia tunalalamika ndani yetu, tukitazamia kufanywa watoto wa Mungu, nazo nafsi zenu zikombolewe.
And not only this, but ourselves also, who have the first fruits of the Spirit, even we ourselves groan within ourselves, waiting for adoption, the redemption of our body.
24 Maana kwa matumaini hayo sisi tumekombolewa; lakini tumaini halina maana ikiwa tunakiona kile tunachotumainia. Maana ni nani anayetumaini kile ambacho tayari anakiona?
For we were saved in hope, but hope that is seen is not hope. For who hopes for that which he sees?
25 Kama tunakitumaini kile ambacho hatujakiona bado, basi, tunakingojea kwa uvumilivu.
But if we hope for that which we do not see, we wait for it with patience.
26 Hali kadhalika, naye Roho anatusaidia katika udhaifu wetu. Maana hatujui inavyotupasa kuomba; lakini Roho mwenyewe anatuombea kwa Mungu kwa mlio wa huzuni usioelezeka.
And in the same way, the Spirit also helps our weaknesses, for we do not know how to pray as we ought. But the Spirit himself makes intercession for us with inexpressible groanings.
27 Naye Mungu aonaye mpaka ndani ya mioyo ya watu, anajua fikira ya huyo Roho; kwani huyo Roho huwaombea watu wa Mungu kufuatana na mapenzi ya Mungu.
And he who searches the hearts knows what is on the Spirit's mind, because he makes intercession for the saints in accordance with God.
28 Tunajua kwamba, katika mambo yote, Mungu hufanya kazi na kuifanikisha pamoja na wote wampendao, yaani wale aliowaita kufuatana na kusudi lake.
And we know that all things work together for good for those who love God, to those who are called according to his purpose.
29 Maana hao aliowachagua tangu mwanzo, ndio aliowateua wapate kufanana na Mwanae, ili Mwana awe wa kwanza miongoni mwa ndugu wengi.
For whom he foreknew, he also predestined to be conformed to the image of his Son, that he might be the firstborn among many brothers.
30 Basi, Mungu aliwaita wale aliokuwa amewateua; na hao aliowaita aliwakubali kuwa waadilifu; na hao aliowakubali kuwa waadilifu aliwashirikisha pia utukufu wake.
Whom he predestined, those he also called. Whom he called, those he also justified. Whom he justified, those he also glorified.
31 Kutokana na hayo, tuseme nini zaidi? Ikiwa Mungu yuko upande wetu, nani awezaye kutupinga?
What then are we to say about these things? If God is for us, who can be against us?
32 Mungu hakumhurumia hata mwanae wa pekee, bali alimtoa kwa ajili yetu sisi sote. Ikiwa amefanya hivyo, je, hatatujalia pia mema yote?
He who did not spare his own Son, but delivered him up for us all, how would he not also with him freely give us all things?
33 Ni nani atakayewashtaki wateule wa Mungu? Mungu mwenyewe huwaondolea hatia!
Who could bring a charge against God's chosen ones? It is God who justifies.
34 Ni nani atakayewahukumu? Hakuna! Maana Kristo ndiye aliyekufa, tena alifufuka kutoka wafu na anakaa upande wa kulia wa Mungu. Yeye anatuombea!
Who is he who condemns? It is Christ who died, and more than that, who was raised, who is at the right hand of God, who also makes intercession for us.
35 Ni nani awezaye kututenga na mapendo ya Kristo? Je, ni taabu, au dhiki, au mateso, au njaa, au ukosefu wa nguo, au hatari, au kuuawa?
Who will separate us from the love of Christ? Could oppression, or anguish, or persecution, or famine, or nakedness, or danger, or sword?
36 Kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: “Kwa ajili yako, twakikabili kifo kutwa kucha: tunatendewa kama kondoo wa kuchinjwa.”
Even as it is written, "For your sake we are killed all day long. We were regarded as sheep to be slaughtered."
37 Lakini, katika mambo haya yote, tumepata ushindi mkubwa kwa msaada wake yeye aliyetupenda.
No, in all these things, we are more than conquerors through him who loved us.
38 Maana ninajua hakika kwamba hakuna kitu kiwezacho kututenganisha na upendo wake: wala kifo, wala uhai; wala malaika, au nguvu nyingine za mbinguni; wala yanayotokea sasa, wala yatakayotokea baadaye; wala mamlaka;
For I am persuaded, that neither death, nor life, nor angels, nor rulers, nor things present, nor things to come, nor powers,
39 Wala ulimwengu wa juu, wala wa chini kabisa. Hakuna kiumbe chochote kitakachoweza kututenga na upendo wa Mungu kwetu kwa njia ya Kristo Yesu Bwana wetu.
nor height, nor depth, nor any other created thing, will be able to separate us from the love of God, which is in Christ Jesus our Lord.

< Warumi 8 >