< Warumi 8 >

1 Kwa hiyo, sasa hakuna hukumu kwa wale ambao katika maisha yao wameungana na Kristo.
Thus there is now no condemnation to those who are in Christ Jesus;
2 Maana, sheria ya Roho iletayo uzima kwa kuungana na Kristo Yesu imenikomboa kutoka katika sheria ya dhambi na kifo.
for the law of the spirit of life in Christ Jesus has set me free from the law of sin and of death.
3 Mungu ametekeleza jambo lile ambalo Sheria haikuweza kutekeleza kwa sababu ya udhaifu w binadamu. Mungu alimtuma Mwanae akiwa mwenye mwili sawa na miili yetu sisi wenye dhambi, ili aikabili dhambi, na kwa mwili huo akaiangamiza dhambi.
For God has done what the Law could not do, weakened as it was by flesh. By sending his own Son in the likeness of sinful flesh, and on account of sin, he condemned sin in the flesh;
4 Mungu alifanya hivyo kusudi matakwa ya haki ya Sheria yatekelezwe kikamilifu ndani yetu sisi ambao tunaishi, si kwa nguvu za kibinadamu, bali kwa nguvu ya Roho.
in order that the Law might be fulfilled in us who order our lives not after the flesh, but after the spirit.
5 Maana, wale wanaoishi kufuatana na matakwa ya mwili, hutawaliwa na fikira za mwili. Lakini wale wanaoishi kufuatana na matakwa ya Roho Mtakatifu, hutawaliwa na fikira za Roho.
For they who live after the flesh, give their attention to the things of the flesh; But they who live after the spirit, give their attention to spiritual things.
6 Fikira za mwili huleta kifo; fikira za Roho huleta uzima na amani.
To be earthly minded means death; To be spiritually minded means life and peace.
7 Maana, mwenye kutawaliwa na fikira za mwili ni adui wa Mungu; haitii sheria ya Mungu, wala hawezi kuitii.
For to be earthly minded is enmity against God; For such a mind is not subject to the Law of God, Nor can it be;
8 Watu wanaotii matakwa ya mwili hawawezi kumpendeza Mungu.
And they who are earthly minded cannot please God.
9 Lakini ninyi hamuishi kufuatana na matakwa ya mwili, bali kufuatana na matakwa ya Roho, ikiwa Roho wa Mungu anaishi ndani yenu. Yeyote asiye na Roho wa Kristo, huyo si wake Kristo.
But you are not earthly, but spiritual, if indeed the Spirit of God is really dwelling in you. If any one does not have the Spirit of Christ, he is none of his.
10 Lakini kama Kristo yumo ndani yenu, ingawa miili yenu itakufa kwa sababu ya dhambi, kwenu Roho ndiye uhai kwa sababu mmekubaliwa kuwa waadilifu.
But if Christ is in you, though your bodily self is dead because of sin, your spirit is full of life because of righteousness.
11 Ikiwa Roho wa Mungu aliyemfufua Kristo kutoka wafu anaishi ndani yenu, basi huyo aliyemfufua Kristo kutoka wafu ataipa uzima miili yenu yenye hali ya kufa; atafanya hivyo kwa njia ya Roho wake akaaye ndani yenu.
But if the Spirit of Him who raised up Jesus from dead is dwelling in you, He who raised up Jesus from the dead is dwelling in you, He who raised up Christ Jesus from the dead will also make your dying bodily self live by his indwelling Spirit in your lives.
12 Hivyo basi, ndugu zangu, tunalo jukumu, lakini si la kuishi kufuatana na maumbile ya kibinadamu.
Therefore, brothers, we are debtors - but not to the flesh, to live according to the flesh;
13 Kwa maana, kama mkiishi kufuatana na matakwa ya maumbile ya kibinadamu, hakika mtakufa. Lakini, kama kwa njia ya Roho mnayaua matendo yenu maovu, basi, mtaishi.
for if you go on living according to the flesh, you are on the road to die; but if by the Spirit you keep putting to death the deeds of the body, you will live.
14 Wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu ni watoto wa Mungu.
For only those are sons of God who are led by God’s Spirit.
15 Kwa maana, Roho mliyempokea si Roho mwenye kuwafanya ninyi watumwa na kuwatia tena hofu; sivyo, bali mmempokea Roho mwenye kuwafanya ninyi watoto wa Mungu, na kwa nguvu ya huyo Roho, sisi tunaweza kumwita Mungu, “Aba,” yaani “Baba!”
For you have not received a spirit of slavery in order that you should once more be afraid; but you have received a spirit of adoption, in which we cry out, "My Father, my dear Father!"
16 Naye Roho mwenyewe anajiunga na roho zetu na kuthibitisha kwamba sisi ni watoto wa Mungu.
For his Spirit himself bears witness with our spirit, that we are children of God;
17 Basi, kwa vile sisi ni watoto wa Mungu, tutapokea baraka zote Mungu alizowawekea watu wake, na tutashiriki urithi huo pamoja na Kristo; maana, tukiyashiriki mateso yake Kristo, tutaushiriki pia utukufu wake.
and if children, then heirs, heirs of God and joint-heirs with Christ; but to share his glory, we must now be sharing his sufferings.
18 Naona kuwa mateso ya wakati huu wa sasa si kitu kamwe kama tukiyafananisha na ule utukufu utakaodhihirishwa kwetu.
For I count as nothing what we now suffer, in comparison with the glory which will soon be unveiled to us.
19 Viumbe vyote vinatazamia kwa hamu Mungu awadhihirishe watoto wake.
All nature even is waiting with eager longing for the unveiling of the vision of God’s sons.
20 Kwa maana, viumbe viliwekwa katika hali ya kutojiweza kabisa, si kwa hiari yao, ila vilifanywa hivyo kwa mapenzi ya Mungu. Hata hivyo yapo matumaini,
For nature was subjected to imperfection, not by its own will, but by the will of Him who thus made it subject -
21 maana hivyo viumbe navyo vitaokolewa kutoka katika utumwa wa uharibifu, vishiriki uhuru mtukufu wa watoto wa Mungu.
yet not without the hope that some day nature itself also will be freed from the thraldom of decay, into the freedom which belongs to the glory of the children of God.
22 Kwa maana tunajua kwamba mpaka hivi sasa, viumbe vyote vinalia kwa maumivu kama ya kujifungua mtoto.
For we know that all nature has been groaning and travailing together until this hour.
23 Wala si hivyo viumbe peke yake, bali hata sisi tulio na huyo Roho, aliye wa kwanza wa zawadi za Mungu; sisi pia tunalalamika ndani yetu, tukitazamia kufanywa watoto wa Mungu, nazo nafsi zenu zikombolewe.
And not only that, we ourselves, although we are grasping the first- fruits of the Spirit, even we ourselves are inwardly groaning, while we are waiting for adoption, the redemption of our body.
24 Maana kwa matumaini hayo sisi tumekombolewa; lakini tumaini halina maana ikiwa tunakiona kile tunachotumainia. Maana ni nani anayetumaini kile ambacho tayari anakiona?
For by hope we are saved; but hope which is clearly seen is no longer hope.
25 Kama tunakitumaini kile ambacho hatujakiona bado, basi, tunakingojea kwa uvumilivu.
Who hopes for what he clearly sees? But if we hope for something that we do not see, we then patiently wait for it.
26 Hali kadhalika, naye Roho anatusaidia katika udhaifu wetu. Maana hatujui inavyotupasa kuomba; lakini Roho mwenyewe anatuombea kwa Mungu kwa mlio wa huzuni usioelezeka.
In the same way the Spirit also takes hold with us in our weakness; for we know knot how to pray as we ought; but the Spirit himself intercedes for us with groanings which cannot be uttered.
27 Naye Mungu aonaye mpaka ndani ya mioyo ya watu, anajua fikira ya huyo Roho; kwani huyo Roho huwaombea watu wa Mungu kufuatana na mapenzi ya Mungu.
And the Searcher of Hearts knows what the Sprit’s meaning is, because his intercessions for the saints are according to the will of God.
28 Tunajua kwamba, katika mambo yote, Mungu hufanya kazi na kuifanikisha pamoja na wote wampendao, yaani wale aliowaita kufuatana na kusudi lake.
Now we know that all things continually work together for good to to those who love God, to those who have been the called according to his purpose.
29 Maana hao aliowachagua tangu mwanzo, ndio aliowateua wapate kufanana na Mwanae, ili Mwana awe wa kwanza miongoni mwa ndugu wengi.
For whom he foreknew, he also foreordained to be conformed to the likeness of his Son, so that he might be the eldest of a great brotherhood;
30 Basi, Mungu aliwaita wale aliokuwa amewateua; na hao aliowaita aliwakubali kuwa waadilifu; na hao aliowakubali kuwa waadilifu aliwashirikisha pia utukufu wake.
and whom he foreordained, those he also called; and whom he called, those he also justified; and whom he justified, those he also glorified.
31 Kutokana na hayo, tuseme nini zaidi? Ikiwa Mungu yuko upande wetu, nani awezaye kutupinga?
What shall we say then, to these things? If God be for us, Who can be against us?
32 Mungu hakumhurumia hata mwanae wa pekee, bali alimtoa kwa ajili yetu sisi sote. Ikiwa amefanya hivyo, je, hatatujalia pia mema yote?
He that spared not his own Son, But freely delivered him up for us all, How shall he not with him also freely give us all things?
33 Ni nani atakayewashtaki wateule wa Mungu? Mungu mwenyewe huwaondolea hatia!
Who shall accuse God’s elect? God acquits them;
34 Ni nani atakayewahukumu? Hakuna! Maana Kristo ndiye aliyekufa, tena alifufuka kutoka wafu na anakaa upande wa kulia wa Mungu. Yeye anatuombea!
Who is there to condemn them? Will Christ who died? Yes, and who rose from the dead, The Christ who is also at the right hand of God, And is interceding for us?
35 Ni nani awezaye kututenga na mapendo ya Kristo? Je, ni taabu, au dhiki, au mateso, au njaa, au ukosefu wa nguo, au hatari, au kuuawa?
What shall separate us from the love of Christ? Shall anguish, or calamity, or persecution, or famine? Shall nakedness, or peril, or sword?
36 Kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: “Kwa ajili yako, twakikabili kifo kutwa kucha: tunatendewa kama kondoo wa kuchinjwa.”
Even as it is written. For thy sake we are killed all the day long; We are accounted as sheep for the slaughter.
37 Lakini, katika mambo haya yote, tumepata ushindi mkubwa kwa msaada wake yeye aliyetupenda.
Nay, in all these things we are more than conquerors Through Him who loved us.
38 Maana ninajua hakika kwamba hakuna kitu kiwezacho kututenganisha na upendo wake: wala kifo, wala uhai; wala malaika, au nguvu nyingine za mbinguni; wala yanayotokea sasa, wala yatakayotokea baadaye; wala mamlaka;
For I am fully persuaded that neither death nor life, Neither angels nor principalities, nor powers, Neither the present world nor the world to come, Nor the powers of Nature,
39 Wala ulimwengu wa juu, wala wa chini kabisa. Hakuna kiumbe chochote kitakachoweza kututenga na upendo wa Mungu kwetu kwa njia ya Kristo Yesu Bwana wetu.
Nor height, nor depth, Nor any other created thing, Shall be able to separate us from the love of God Which is in Christ Jesus our Lord.

< Warumi 8 >