< Warumi 6 >
1 Tuseme nini basi? Je, twendelee kubaki katika dhambi ili neema ya Mungu iongezeke?
Et maintenant comment conclure? En disant que nous persisterons à pécher pour faire abonder la grâce?
2 Hata kidogo! Kuhusu dhambi sisi tumekufa—tutaendeleaje kuishi tena katika dhambi?
Non, certes. Nous qui sommes morts au péché, comment y vivrions-nous encore?
3 Maana, mnajua kwamba sisi tuliobatizwa tukaungana na Kristo Yesu, tulibatizwa na kuungana na kifo chake.
Ne savez-vous pas que nous tous qui avons été baptisés en Jésus-Christ, c'est en sa mort que nous l'avons été? Nous avons été ensevelis avec lui par le baptême en sa mort,
4 Tulipobatizwa tuliungana na kifo chake, tukazikwa pamoja naye, ili kama vile Kristo alivyofufuliwa kutoka wafu kwa kitendo kitukufu cha Baba, sisi pia tuweze kuishi maisha mapya.
et de même que Christ a été ressuscité des morts par la gloire du Père, de même nous devons vivre d'une vie nouvelle.
5 Maana, kama sisi tumeungana naye katika kufa kama yeye, vivyo hivyo tutaungana naye kwa kufufuliwa kutoka wafu kama yeye.
Si nous sommes étroitement unis à lui par une mort semblable à la sienne, nous le serons aussi par une même résurrection;
6 Tunajua kwamba utu wetu wa kale ulisulubiwa pamoja na Kristo, ili hali ya dhambi iharibiwe, tusiwe tena watumwa wa dhambi.
nous savons que notre vieil homme a été crucifié avec lui, afin que ce corps de péché soit détruit, et que nous ne soyons plus esclaves du péché.
7 Kwa maana, mtu aliyekufa, amenasuliwa kutoka katika nguvu ya dhambi.
Celui qui est mort est déclaré juste et est délivré du péché.
8 Basi, ikiwa tumekufa pamoja na Kristo, tunaamini kwamba tutaishi pia pamoja naye.
Si nous sommes morts avec le Christ, nous croyons que nous vivrons aussi avec lui,
9 Maana, tunajua kwamba Kristo amekwisha fufuliwa kutoka wafu na hafi tena; kifo hakimtawali tena.
car nous savons que Christ ressuscité des morts ne meurt plus; la mort n'a plus de pouvoir sur lui.
10 Hivyo, kwa kuwa alikufa—mara moja tu—dhambi haina nguvu tena juu yake; na sasa anaishi maisha yake katika umoja na Mungu.
Il est mort, en effet, et c'est à cause du péché qu'il est mort une fois pour toutes; puis il est revenu à la vie, et c'est pour Dieu qu'il vit.
11 Hali kadhalika nanyi lazima mjione kuwa mmekufa kuhusu dhambi, lakini kama mnaoishi katika umoja na Mungu kwa njia ya Kristo Yesu.
De même considérez-vous aussi comme morts au péché et comme vivants pour Dieu en Jésus-Christ.
12 Kwa hiyo, dhambi isiitawale tena miili yenu ambayo hufa, na hivyo kuzitii tamaa zake.
Que le péché ne règne donc pas dans votre corps mortel, n'obéissez pas à ses passions;
13 Wala msitoe hata sehemu moja ya miili yenu iwe chombo cha kutenda uovu na dhambi. Badala yake, jitoleeni ninyi wenyewe kwa Mungu kama watu waliofufuliwa kutoka wafu; toeni nafsi zenu zote kwa Mungu kwa ajili ya uadilifu.
ne livrez pas vos membres au péché; n'en faites pas les instruments du vice, mais donnez-vous à Dieu, vous qui étiez morts et qui vivez, consacrez vos membres à Dieu, faites-en des instruments de justice.
14 Maana, dhambi haitawatawala ninyi tena, kwani hamko chini ya Sheria, bali chini ya neema.
Le péché n'aura plus de pouvoir sur vous, car vous n'êtes pas sous la Loi, mais sous la grâce.
15 Basi, tuseme nini? Je, tutende dhambi ati kwa sababu hatuko chini ya Sheria bali chini ya neema? Hata kidogo!
Mais quoi? Devons-nous pécher parce que nous ne sommes pas sous la Loi, mais sous la grâce? Oh! nullement.
16 Mnajua kwamba mkijitolea ninyi wenyewe kama watumwa na kumtii fulani, mnakuwa kweli watumwa wake mtu huyo—au watumwa wa dhambi, na matokeo yake ni kifo, au wa utii, na matokeo yake ni kukubaliwa kuwa waadilifu.
Ne savez-vous pas que si vous vous asservissez à quelqu'un et lui obéissez, vous devenez ses esclaves? soit du péché qui mène à la mort, soit de la soumission qui mène à la justice.
17 Ingawa mlikuwa watumwa wa dhambi zamani, sasa lakini—namshukuru Mungu—mmetii kwa moyo wote yale maazimio na mafundisho mliyopokea.
Grâces soient rendues à Dieu, de ce qu'autrefois, esclaves du péché, vous vous êtes soumis de coeur au type de doctrine qui vous a été offert!
18 Mlikombolewa kutoka utumwa wa dhambi, mkawa watumwa wa uadilifu.
Mais du moment que vous avez été délivrés du péché, vous êtes devenus esclaves de la justice (j'emploie cette expression usuelle: esclaves, à cause de votre faiblesse naturelle);
19 (Hapa natumia lugha ya kawaida ya watu kwa sababu ya udhaifu wenu wenyewe.) Kama vile wakati fulani mlivyojitolea ninyi wenyewe kutumikia uchafu na uhalifu kwa ajili ya uovu, vivyo hivyo sasa jitoleeni nafsi zenu wenyewe kutumikia uadilifu kwa ajili ya utakatifu.
de même, veux-je dire, que vous avez mis vos membres au service de l'impureté et de l'iniquité pour violer la Loi, de même vous devez mettre maintenant vos membres au service de la justice pour vous sanctifier.
20 Mlipokuwa watumwa wa dhambi, mlikuwa huru mbali na uadilifu.
Lorsque vous étiez esclaves du péché, vous étiez libres à l'égard de la justice.
21 Sasa, mlipata faida gani siku zile kutokana na mambo yale ambayo mnayaonea aibu sasa? Maana, matokeo ya mambo haya ni kifo!
Quel avantage en retiriez-vous? Un avantage qui vous fait honte aujourd'hui; cela vous menait à la mort.
22 Lakini sasa, mmekwisha kombolewa kutoka utumwa wa dhambi na mmekuwa watumishi wa Mungu; faida mliyo nayo sasa ni utakatifu, na matokeo yake ni uzima wa milele. (aiōnios )
Mais maintenant, délivrés du péché et esclaves de Dieu, l'avantage que vous retirez, c'est la sanctification qui mène à la vie éternelle. (aiōnios )
23 Kwa maana mshahara wa dhambi ni kifo; lakini zawadi anayotoa Mungu ni uzima wa milele katika kuungana na Kristo Yesu, Bwana wetu. (aiōnios )
Le salaire du péché, c'est la mort; mais le don de la grâce de Dieu, c'est la vie éternelle en Jésus-Christ notre Seigneur. (aiōnios )