< Warumi 4 >
1 Tuseme nini basi, juu ya Abrahamu baba yetu?
Que diremos pois ter achado Abraão, nosso pai segundo a carne?
2 Kama Abrahamu alikubaliwa kuwa mwadilifu kutokana na matendo yake, basi, anacho kitu cha kujivunia mbele ya Mungu.
Porque, se Abraão foi justificado pelas obras, tem de que se glóriar, mas não diante de Deus.
3 Kwa maana, Maandiko Matakatifu yasema: “Abrahamu alimwamini Mungu, naye Mungu akamkubali kuwa mwadilifu.”
Pois, que diz a escritura? Creu Abraão a Deus, e isso lhe foi imputado como justiça.
4 Mfanyakazi hulipwa mshahara; mshahara wake si zawadi bali ni haki yake.
Ora àquele que obra não lhe é imputado o galardão segundo a graça, mas segundo a dívida.
5 Lakini mtu asiyetegemea matendo yake mwenyewe, bali anamwamini Mungu ambaye huwasamehe waovu, basi, Mungu huijali imani ya mtu huyo, na hivi humkubali kuwa mwadilifu.
Porém àquele que não obra, mas crê naquele que justifica o ímpio, a sua fé lhe é imputada como justiça.
6 Naye Daudi asema hivi juu ya furaha ya mtu ambaye Mungu amemkubali kuwa mwadilifu bila kuyajali matendo yake:
Como também David declara bem-aventurado o homem a quem Deus imputa a justiça sem as obras, dizendo:
7 “Heri wale waliosamehewa makosa yao ambao makosa yao yamefutwa.
Bem-aventurados aqueles cujas maldades são perdoadas, e cujos pecados são cobertos:
8 Heri mtu yule ambaye Bwana hataziweka dhambi zake katika kumbukumbu.”
Bem-aventurado o homem a quem o Senhor não imputa o pecado.
9 Je, hiyo ni kwa wale waliotahiriwa tu, ama pia kwa wale wasiotahiriwa? Ni kwa wale wasiotahiriwa pia. Kwa maana tumekwisha sema: “Abrahamu aliamini, naye Mungu akamkubali kuwa mwadilifu.”
Vem pois esta benaventurança sobre a circuncisão só, ou também sobre a incircuncisão? Porque dizemos que a fé foi imputada como justiça a Abraão.
10 Je, Abrahamu alikubaliwa kabla ya kutahiriwa ama baada ya kutahiriwa? Kabla ya kutahiriwa, na si baada ya kutahiriwa.
Como lhe foi pois imputada? Estando na circuncisão ou na incircuncisão? Não na circuncisão, mas na incircuncisão.
11 Abrahamu alitahiriwa baadaye, na kutahiriwa huko kulikuwa alama iliyothibitisha kwamba Mungu alimkubali kuwa mwadilifu kwa sababu ya imani yake aliyokuwa nayo kabla ya kutahiriwa. Kwa hiyo, Abrahamu amekuwa baba wa wale wote ambao, ingawa hawakutahiriwa, wamemwamini Mungu, wakafanywa waadilifu.
E recebeu o sinal da circuncisão, selo da justiça da fé que teve na incircuncisão, para que fosse pai de todos os que crêem, estando na incircuncisão; a fim de que também a justiça lhes seja imputada:
12 Vilevile yeye ni baba wa wale waliotahiriwa; lakini si kwa kuwa wametahiriwa, bali kwa sababu wanafuata njia ileile ya imani baba yetu Abrahamu aliyofuata kabla ya kutahiriwa.
E fosse pai da circuncisão, daqueles que não somente são da circuncisão, mas que também andam nas pisadas da fé de nosso pai Abraão, que tivera na incircuncisão.
13 Mungu alimwahidi Abrahamu na wazawa wake kwamba ulimwengu ungekuwa mali yao. Ahadi hiyo haikufanywa kwa sababu Abrahamu aliitii Sheria, bali kwa kuwa aliamini, akakubaliwa kuwa mwadilifu.
Porque a promessa de que havia de ser herdeiro do mundo não foi feita pela lei a Abraão, ou à sua posteridade, mas pela justiça da fé.
14 Maana kama watakaopewa hayo aliyoahidi Mungu ni wale tu wanaoitii Sheria, basi, imani haina maana yoyote, nayo ahadi ya Mungu si kitu.
Porque, se os que são da lei são herdeiros, logo a fé é vã e a promessa é aniquilada.
15 Sheria husababisha ghadhabu; lakini kama hakuna Sheria, haiwezekani kuivunja.
Porque a lei obra a ira. Porque onde não há lei também não há transgressão.
16 Kwa sababu hiyo, jambo hili lategemea imani, hivyo kwamba ahadi hiyo yatokana na neema ya Mungu, na kwamba ni hakika kuwa ahadi hiyo ni kwa ajili ya wote: si kwa wale tu wanaoishika Sheria, bali pia kwa wale waishio kwa imani kama Abrahamu. Yeye ni baba yetu sisi sote.
Portanto é pela fé, para que seja segundo a graça, a fim de que a promessa seja firme a toda a posteridade, não somente à que é da lei, mas também à que é da fé de Abraão, o qual é pai de todos nós;
17 Kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: “Nimekuweka uwe baba wa mataifa mengi.” Ahadi hiyo ni kweli mbele ya Mungu ambaye Abrahamu alimwamini—Mungu ambaye huwapa wafu uzima, na kwa amri yake, vitu ambavyo havikuwapo huwa.
(Como está escrito: Por pai de muitas nações te constitui) perante aquele no qual creu, a saber, Deus, o qual vivifica os mortos, e chama as coisas que não são como se já fossem.
18 Abrahamu aliamini na kutumaini ingawa hali yenyewe ilikuwa bila matumaini, na hivyo amekuwa baba wa mataifa mengi kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: “Wazao wako watakuwa wengi kama nyota!”
O qual, em esperança, creu contra a esperança, que seria feito pai de muitas nações, conforme o que lhe fôra dito: Assim será a tua descendência.
19 Alikuwa mzee wa karibu miaka mia moja, lakini imani yake haikufifia ingawa alijua kwamba mwili wake ulikuwa kama umekufa, na pia mkewe, Sara, alikuwa tasa.
E não enfraqueceu na fé, nem atentou para o seu próprio corpo já amortecido, pois era já de quase cem anos, nem tão pouco para o amortecimento do ventre de Sarah.
20 Abrahamu hakuionea mashaka ile ahadi ya Mungu; alipata nguvu kutokana na imani, akamtukuza Mungu.
E não duvidou da promessa de Deus por desconfiança, mas foi fortificado na fé, dando glória a Deus;
21 Alijua kwamba Mungu anaweza kuyatekeleza yale aliyoahidi.
E estando certíssimo de que o que ele tinha prometido também era poderoso para o fazer.
22 Ndiyo maana Mungu alimkubali kuwa mwadilifu.
Pelo que isso lhe foi também imputado como justiça.
23 Inaposemwa, “Alimkubali,” haisemwi kwa ajili yake mwenyewe tu.
Ora não só por ele está escrito, que lhe fosse imputado,
24 Jambo hili linatuhusu sisi pia ambao tunamwamini Mungu aliyemfufua Yesu, Bwana wetu, kutoka wafu.
Mas também por nós, a quem será imputado, os que cremos naquele que dos mortos resuscitou a Jesus nosso Senhor;
25 Yeye alitolewa auawe kwa ajili ya dhambi zetu, akafufuka ili tupate kukubaliwa kuwa waadilifu na Mungu.
O qual por nossos pecados foi entregue, e resuscitou para nossa justificação.