< Warumi 3 >
1 Basi, Myahudi ana nini zaidi kuliko watu wengine? Au kutahiriwa kuna faida gani?
Qual é logo a vantagem do judeu? Ou qual a utilidade da circuncisão?
2 Naam, iko faida kwa kila upande. Kwanza, Mungu aliwakabidhi Wayahudi ujumbe wake.
Muita, em toda a maneira, porque, quanto ao primeiro, as palavras de Deus lhe foram confiadas,
3 Lakini itakuwaje iwapo baadhi yao hawakuwa waaminifu? Je, jambo hilo litaondoa uaminifu wa Mungu?
Pois que? Se alguns foram incrédulos, a sua incredulidade aniquilará a fé de Deus?
4 Hata kidogo! Mungu hubaki mwaminifu daima, ingawaje kila binadamu ni mwongo. Kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: “Kila usemapo, maneno yako ni ya haki; na katika hukumu, wewe hushinda.”
De maneira nenhuma; antes seja Deus verdadeiro, e todo o homem mentiroso; como está escrito: Para que sejas justificado em tuas palavras, e venças quando fores julgado.
5 Lakini, ikiwa uovu wetu unathibitisha kwamba Mungu anatenda kwa haki, tutasema nini? Je, tutasema kwamba anakosa haki akituadhibu? (Hapa naongea kibinadamu).
E, se a nossa injustiça recomendar a justiça de Deus, que diremos? Porventura será Deus injusto, trazendo ira sobre nós? ( falo como homem)
6 Hata kidogo! Ingekuwa hivyo, Mungu angewezaje kuuhukumu ulimwengu?
De maneira nenhuma: de outro modo, como julgará Deus o mundo?
7 Labda utasema: “Ikiwa ukosefu wa uaminifu kwa upande wangu unamdhihirisha Mungu kuwa mwaminifu zaidi na hivyo kumpatia utukufu, basi singepaswa kuhukumiwa kuwa mwenye dhambi!”
Porque, se pela minha mentira abundou mais a verdade de Deus para glória sua, porque sou ainda julgado também como pecador?
8 Ni sawa na kusema: tufanye maovu ili tupate mema! Ndivyo wengine walivyotukashifu kwa kutushtaki kwamba tumefundisha hivyo. Watahukumiwa wanavyostahili!
E não dizemos (como somos blasfemados, e como alguns dizem que dizemos): Façamos males, para que venham bens: cuja condenação é justa.
9 Tuseme nini, basi? Je, sisi Wayahudi ni bora zaidi kuliko wengine? Hata kidogo! Kwa maana nimekwisha bainisha hapo mwanzoni kwamba Wayahudi na watu wa mataifa mengine wote wako chini ya utawala wa dhambi.
Pois que? Somos nós mais excelentes? de maneira nenhuma, pois já de antes demonstramos que, tanto judeus como gregos, todos estão debaixo do pecado;
10 Kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: “Hakuna hata mmoja aliye mwadilifu!
Como está escrito: Não há justo, nem ainda um:
11 Hakuna mtu anayeelewa, wala anayemtafuta Mungu.
Não há ninguém que entenda; não há ninguém que busque a Deus:
12 Wote wamepotoka wote wamekosa; hakuna atendaye mema, hakuna hata mmoja.
Todos se extraviaram, e juntamente se fizeram inúteis. Não há quem faça o bem, não há nem um só
13 Makoo yao ni kama kaburi wazi, ndimi zao zimejaa udanganyifu, midomoni mwao mwatoka maneno yenye sumu kama ya nyoka.
A sua garganta é um sepulcro aberto: com as suas línguas tratam enganosamente: peçonha de áspides está debaixo de seus lábios:
14 Vinywa vyao vimejaa laana chungu.
Cuja boca está cheia de maldição e amargura:
15 Miguu yao iko mbioni kumwaga damu,
Os seus pés são ligeiros para derramar sangue:
16 popote waendapo husababisha maafa na mateso;
Em seus caminhos há destruição e miséria:
17 njia ya amani hawaijui.
E não conheceram o caminho da paz:
18 Hawajali kabisa kumcha Mungu.”
Não há temor de Deus diante de seus olhos.
19 Tunajua kwamba Sheria huwahusu walio chini ya Sheria hiyo, hata hawawezi kuwa na kisingizio chochote, na ulimwengu wote uko chini ya hukumu ya Mungu.
Ora, nós sabemos que tudo o que a lei diz aos que estão debaixo da lei o diz, para que toda a boca se feche e todo o mundo seja condenável diante de Deus.
20 Maana hakuna binadamu yeyote anayekubaliwa kuwa mwadilifu mbele yake Mungu kwa kuishika Sheria; kazi ya Sheria ni kumwonyesha tu mtu kwamba ametenda dhambi.
Por isso nenhuma carne será justificada diante dele pelas obras da lei, porque pela lei vem o conhecimento do pecado.
21 Lakini sasa, njia ya Mungu ya kuwakubali watu kuwa waadilifu imekwisha dhihirishwa, tena bila kutegemea Sheria. Sheria na manabii hushuhudia jambo hili.
Mas agora se manifestou sem a lei a justiça de Deus, tendo o testemunho da lei e dos profetas;
22 Mungu huwakubali watu kuwa waadilifu kwa njia ya imani yao kwa Yesu Kristo; Mungu hufanya hivyo kwa wote wanaoamini; hakuna ubaguzi wowote.
Isto é, a justiça de Deus pela fé de Jesus Cristo para todos e sobre todos os que crêem; porque não há diferença,
23 Watu wote wametenda dhambi na wametindikiwa utukufu wa Mungu.
Porque todos pecaram e destituídos estão da glória de Deus;
24 Lakini kwa zawadi ya neema ya Mungu, watu wote hukubaliwa kuwa waadilifu kwa njia ya Yesu Kristo anayewakomboa.
Sendo justificados gratuitamente pela sua graça, pela redenção que há em Cristo Jesus:
25 Mungu alimtoa Yesu kusudi, kwa damu yake, awe njia ya kuwaondolea watu dhambi zao kwa imani yao kwake. Alifanya hivyo ili apate kuonyesha kwamba yeye ni mwadilifu. Hapo zamani Mungu alikuwa mvumilivu bila kuzijali dhambi za watu;
Ao qual Deus propôs para propiciação pela fé no seu sangue, para demonstração da sua justiça, pela remissão dos pecados de antes cometidos, sob a paciência de Deus;
26 lakini sasa, wakati huu, anazikabili dhambi za watu apate kuonyesha uadilifu wake. Kwa namna hiyo Mungu mwenyewe huonyesha kwamba yeye ni mwadilifu na kwamba humkubali kuwa mwadilifu mtu yeyote anayemwamini Yesu.
Para demonstração da sua justiça neste tempo presente, para que ele seja justo e justificador daquele que tem fé em Jesus.
27 Basi, tunaweza kujivunia nini? Hakuna! Kwa nini? Je, kwa sababu ya kutimiza Sheria? La! Bali kwa sababu tunaamini.
Onde está logo a jactância? É excluída. Por qual lei? Das obras? Não; mas pela lei da fé
28 Maana mtu hukubaliwa kuwa mwadilifu kwa imani, wala si kwa kutimiza matakwa ya Sheria.
Concluímos pois que o homem é justificado pela fé sem as obras da lei.
29 Au je, Mungu nu Mungu wa Wayahudi tu, ama pia wa watu wa mataifa mengine? Naam, wa mataifa mengine pia.
Deus é porventura somente dos judeus? E não o é também dos gentios? também dos gentios, certamente.
30 Mungu ni mmoja, naye atawakubali Wayahudi kuwa waadilifu kwa imani yao, na watu wa mataifa mengine pia kwa imani yao.
Porque há um só Deus que justificará pela fé a circuncisão, e pela fé a incircuncisão.
31 Je, tunaitumia imani kuibatilisha Sheria? Hata kidogo; bali tunaipa Sheria thamani yake kamili.
Anulamos, pois, a lei pela fé? De maneira nenhuma, antes estabelecemos a lei.