< Warumi 3 >
1 Basi, Myahudi ana nini zaidi kuliko watu wengine? Au kutahiriwa kuna faida gani?
Quelle est donc la prérogative du Juif, ou quelle est l'utilité de la circoncision?
2 Naam, iko faida kwa kila upande. Kwanza, Mungu aliwakabidhi Wayahudi ujumbe wake.
Elle est grande à tous égards. Et tout d'abord en ceci: c'est aux Juifs que les oracles de Dieu ont été confiés.
3 Lakini itakuwaje iwapo baadhi yao hawakuwa waaminifu? Je, jambo hilo litaondoa uaminifu wa Mungu?
Eh quoi! Si quelques-uns d'entre eux ont été infidèles, leur infidélité anéantira-t-elle la fidélité de Dieu?
4 Hata kidogo! Mungu hubaki mwaminifu daima, ingawaje kila binadamu ni mwongo. Kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: “Kila usemapo, maneno yako ni ya haki; na katika hukumu, wewe hushinda.”
Non certes! Dieu doit être reconnu vrai, et tout homme menteur, comme il est écrit: «C'est ainsi que tu seras trouvé juste dans tes paroles, et que tu gagneras ta cause quand on te jugera.»
5 Lakini, ikiwa uovu wetu unathibitisha kwamba Mungu anatenda kwa haki, tutasema nini? Je, tutasema kwamba anakosa haki akituadhibu? (Hapa naongea kibinadamu).
Mais alors, si notre injustice fait éclater la justice de Dieu, que dirons-nous? Dieu est-il injuste — je parle ici comme les hommes — quand il déploie sa colère? —
6 Hata kidogo! Ingekuwa hivyo, Mungu angewezaje kuuhukumu ulimwengu?
Non certes! Autrement comment Dieu jugerait-il le monde?
7 Labda utasema: “Ikiwa ukosefu wa uaminifu kwa upande wangu unamdhihirisha Mungu kuwa mwaminifu zaidi na hivyo kumpatia utukufu, basi singepaswa kuhukumiwa kuwa mwenye dhambi!”
Cependant, si la vérité de Dieu reçoit une plus grande gloire par mon mensonge, pourquoi suis-je encore jugé comme pécheur? —
8 Ni sawa na kusema: tufanye maovu ili tupate mema! Ndivyo wengine walivyotukashifu kwa kutushtaki kwamba tumefundisha hivyo. Watahukumiwa wanavyostahili!
Alors, pourquoi ne ferions-nous pas le mal pour qu'il en arrive du bien, ainsi que des calomniateurs nous en accusent et comme ils prétendent que nous l'enseignons? La condamnation de ces hommes-là est juste!
9 Tuseme nini, basi? Je, sisi Wayahudi ni bora zaidi kuliko wengine? Hata kidogo! Kwa maana nimekwisha bainisha hapo mwanzoni kwamba Wayahudi na watu wa mataifa mengine wote wako chini ya utawala wa dhambi.
Quoi donc! Avons-nous quelque chose à faire valoir en notre faveur? Nullement, car nous avons déjà prouvé que tous, Juifs et Grecs, sont sous l'empire du péché,
10 Kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: “Hakuna hata mmoja aliye mwadilifu!
ainsi qu'il est écrit: «Il n'y a point de juste, pas même un seul.
11 Hakuna mtu anayeelewa, wala anayemtafuta Mungu.
Il n'y en a pas un seul qui soit intelligent; il n'y en a pas un qui cherche Dieu.
12 Wote wamepotoka wote wamekosa; hakuna atendaye mema, hakuna hata mmoja.
Ils se sont tous égarés, ils se sont pervertis tous ensemble; il n'y en a point qui fasse le bien, non pas même un seul.
13 Makoo yao ni kama kaburi wazi, ndimi zao zimejaa udanganyifu, midomoni mwao mwatoka maneno yenye sumu kama ya nyoka.
Leur gosier est un sépulcre ouvert; ils se sont servis de leurs langues pour tromper; il y a un venin d'aspic sous leurs lèvres.
14 Vinywa vyao vimejaa laana chungu.
Leur bouche est pleine de malédiction et d'amertume.
15 Miguu yao iko mbioni kumwaga damu,
Ils ont les pieds légers pour répandre le sang.
16 popote waendapo husababisha maafa na mateso;
La destruction et la ruine sont sur leurs sentiers,
17 njia ya amani hawaijui.
et ils n'ont point connu le chemin de la paix.
18 Hawajali kabisa kumcha Mungu.”
La crainte de Dieu n'est pas devant leurs yeux.»
19 Tunajua kwamba Sheria huwahusu walio chini ya Sheria hiyo, hata hawawezi kuwa na kisingizio chochote, na ulimwengu wote uko chini ya hukumu ya Mungu.
Or, nous savons que tout ce que la loi dit, elle l'adresse à ceux qui sont sous la loi, afin que toute bouche soit fermée, et que le monde entier soit reconnu coupable devant Dieu;
20 Maana hakuna binadamu yeyote anayekubaliwa kuwa mwadilifu mbele yake Mungu kwa kuishika Sheria; kazi ya Sheria ni kumwonyesha tu mtu kwamba ametenda dhambi.
car aucun homme ne sera justifié devant lui par les oeuvres de la loi, puisque c'est la loi qui donne la connaissance du péché.
21 Lakini sasa, njia ya Mungu ya kuwakubali watu kuwa waadilifu imekwisha dhihirishwa, tena bila kutegemea Sheria. Sheria na manabii hushuhudia jambo hili.
Mais maintenant, c'est indépendamment de la loi que la justice de Dieu a été manifestée, la loi et les prophètes lui rendant témoignage:
22 Mungu huwakubali watu kuwa waadilifu kwa njia ya imani yao kwa Yesu Kristo; Mungu hufanya hivyo kwa wote wanaoamini; hakuna ubaguzi wowote.
la justice de Dieu, par la foi en Jésus-Christ, pour tous ceux qui croient. Il n'y a point de distinction;
23 Watu wote wametenda dhambi na wametindikiwa utukufu wa Mungu.
car tous ont péché et sont privés de la gloire de Dieu,
24 Lakini kwa zawadi ya neema ya Mungu, watu wote hukubaliwa kuwa waadilifu kwa njia ya Yesu Kristo anayewakomboa.
et ils sont justifiés gratuitement par sa grâce, au moyen de la rédemption accomplie en Jésus-Christ,
25 Mungu alimtoa Yesu kusudi, kwa damu yake, awe njia ya kuwaondolea watu dhambi zao kwa imani yao kwake. Alifanya hivyo ili apate kuonyesha kwamba yeye ni mwadilifu. Hapo zamani Mungu alikuwa mvumilivu bila kuzijali dhambi za watu;
que Dieu a établi comme victime expiatoire, par la foi en son sang. Il a ainsi manifesté sa justice, parce qu'il avait laissé impunis les péchés commis auparavant, au temps de sa patience;
26 lakini sasa, wakati huu, anazikabili dhambi za watu apate kuonyesha uadilifu wake. Kwa namna hiyo Mungu mwenyewe huonyesha kwamba yeye ni mwadilifu na kwamba humkubali kuwa mwadilifu mtu yeyote anayemwamini Yesu.
il a, dis-je, manifesté sa justice dans le temps présent, faisant voir qu'il est juste et qu'il justifie celui qui croit en Jésus.
27 Basi, tunaweza kujivunia nini? Hakuna! Kwa nini? Je, kwa sababu ya kutimiza Sheria? La! Bali kwa sababu tunaamini.
Où est donc le sujet de se glorifier? Il est exclu. Par quelle loi? Celle des oeuvres? Non, par la loi de la foi;
28 Maana mtu hukubaliwa kuwa mwadilifu kwa imani, wala si kwa kutimiza matakwa ya Sheria.
car nous estimons que l'homme est justifié par la foi, sans les oeuvres de la loi.
29 Au je, Mungu nu Mungu wa Wayahudi tu, ama pia wa watu wa mataifa mengine? Naam, wa mataifa mengine pia.
Ou bien, Dieu est-il seulement le Dieu des Juifs? N'est-il pas aussi le Dieu des Païens? Oui, il l'est aussi des Païens,
30 Mungu ni mmoja, naye atawakubali Wayahudi kuwa waadilifu kwa imani yao, na watu wa mataifa mengine pia kwa imani yao.
— puisqu'il y a un seul Dieu, qui justifiera par la loi les circoncis et, au moyen de la foi également, les incirconcis.
31 Je, tunaitumia imani kuibatilisha Sheria? Hata kidogo; bali tunaipa Sheria thamani yake kamili.
Anéantissons-nous donc la loi par la foi? Non certes! Au contraire, nous confirmons la loi.