< Warumi 3 >
1 Basi, Myahudi ana nini zaidi kuliko watu wengine? Au kutahiriwa kuna faida gani?
What advantage then hath the Jew? or what profit [is there] of circumcision?
2 Naam, iko faida kwa kila upande. Kwanza, Mungu aliwakabidhi Wayahudi ujumbe wake.
Much every way: chiefly, because that unto them were committed the oracles of God.
3 Lakini itakuwaje iwapo baadhi yao hawakuwa waaminifu? Je, jambo hilo litaondoa uaminifu wa Mungu?
For what if some did not believe? shall their unbelief make the faith of God without effect?
4 Hata kidogo! Mungu hubaki mwaminifu daima, ingawaje kila binadamu ni mwongo. Kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: “Kila usemapo, maneno yako ni ya haki; na katika hukumu, wewe hushinda.”
God forbid: yea, let God be true, but every man a liar; as it is written, That thou mightest be justified in thy sayings, and mightest overcome when thou art judged.
5 Lakini, ikiwa uovu wetu unathibitisha kwamba Mungu anatenda kwa haki, tutasema nini? Je, tutasema kwamba anakosa haki akituadhibu? (Hapa naongea kibinadamu).
But if our unrighteousness commend the righteousness of God, what shall we say? [Is] God unrighteous who taketh vengeance? (I speak as a man)
6 Hata kidogo! Ingekuwa hivyo, Mungu angewezaje kuuhukumu ulimwengu?
God forbid: for then how shall God judge the world?
7 Labda utasema: “Ikiwa ukosefu wa uaminifu kwa upande wangu unamdhihirisha Mungu kuwa mwaminifu zaidi na hivyo kumpatia utukufu, basi singepaswa kuhukumiwa kuwa mwenye dhambi!”
For if the truth of God hath more abounded through my lie unto his glory; why yet am I also judged as a sinner?
8 Ni sawa na kusema: tufanye maovu ili tupate mema! Ndivyo wengine walivyotukashifu kwa kutushtaki kwamba tumefundisha hivyo. Watahukumiwa wanavyostahili!
And not [rather], (as we be slanderously reported, and as some affirm that we say, ) Let us do evil, that good may come? whose damnation is just.
9 Tuseme nini, basi? Je, sisi Wayahudi ni bora zaidi kuliko wengine? Hata kidogo! Kwa maana nimekwisha bainisha hapo mwanzoni kwamba Wayahudi na watu wa mataifa mengine wote wako chini ya utawala wa dhambi.
What then? are we better [than they]? No, in no wise: for we have before proved both Jews and Gentiles, that they are all under sin;
10 Kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: “Hakuna hata mmoja aliye mwadilifu!
As it is written, There is none righteous, no, not one:
11 Hakuna mtu anayeelewa, wala anayemtafuta Mungu.
There is none that understandeth, there is none that seeketh after God.
12 Wote wamepotoka wote wamekosa; hakuna atendaye mema, hakuna hata mmoja.
They are all gone out of the way, they are together become unprofitable; there is none that doeth good, no, not one.
13 Makoo yao ni kama kaburi wazi, ndimi zao zimejaa udanganyifu, midomoni mwao mwatoka maneno yenye sumu kama ya nyoka.
Their throat [is] an open sepulchre; with their tongues they have used deceit; the poison of asps [is] under their lips:
14 Vinywa vyao vimejaa laana chungu.
Whose mouth [is] full of cursing and bitterness:
15 Miguu yao iko mbioni kumwaga damu,
Their feet [are] swift to shed blood:
16 popote waendapo husababisha maafa na mateso;
Destruction and misery [are] in their ways:
17 njia ya amani hawaijui.
And the way of peace have they not known:
18 Hawajali kabisa kumcha Mungu.”
There is no fear of God before their eyes.
19 Tunajua kwamba Sheria huwahusu walio chini ya Sheria hiyo, hata hawawezi kuwa na kisingizio chochote, na ulimwengu wote uko chini ya hukumu ya Mungu.
Now we know that what things soever the law saith, it saith to them who are under the law: that every mouth may be stopped, and all the world may become guilty before God.
20 Maana hakuna binadamu yeyote anayekubaliwa kuwa mwadilifu mbele yake Mungu kwa kuishika Sheria; kazi ya Sheria ni kumwonyesha tu mtu kwamba ametenda dhambi.
Therefore by the deeds of the law there shall no flesh be justified in his sight: for by the law [is] the knowledge of sin.
21 Lakini sasa, njia ya Mungu ya kuwakubali watu kuwa waadilifu imekwisha dhihirishwa, tena bila kutegemea Sheria. Sheria na manabii hushuhudia jambo hili.
But now the righteousness of God without the law is manifested, being witnessed by the law and the prophets;
22 Mungu huwakubali watu kuwa waadilifu kwa njia ya imani yao kwa Yesu Kristo; Mungu hufanya hivyo kwa wote wanaoamini; hakuna ubaguzi wowote.
Even the righteousness of God [which is] by faith of Jesus Christ unto all and upon all them that believe: for there is no difference:
23 Watu wote wametenda dhambi na wametindikiwa utukufu wa Mungu.
For all have sinned, and come short of the glory of God;
24 Lakini kwa zawadi ya neema ya Mungu, watu wote hukubaliwa kuwa waadilifu kwa njia ya Yesu Kristo anayewakomboa.
Being justified freely by his grace through the redemption that is in Christ Jesus:
25 Mungu alimtoa Yesu kusudi, kwa damu yake, awe njia ya kuwaondolea watu dhambi zao kwa imani yao kwake. Alifanya hivyo ili apate kuonyesha kwamba yeye ni mwadilifu. Hapo zamani Mungu alikuwa mvumilivu bila kuzijali dhambi za watu;
Whom God hath set forth [to be] a propitiation through faith in his blood, to declare his righteousness for the remission of sins that are past, through the forbearance of God;
26 lakini sasa, wakati huu, anazikabili dhambi za watu apate kuonyesha uadilifu wake. Kwa namna hiyo Mungu mwenyewe huonyesha kwamba yeye ni mwadilifu na kwamba humkubali kuwa mwadilifu mtu yeyote anayemwamini Yesu.
To declare, [I say], at this time his righteousness: that he might be just, and the justifier of him which believeth in Jesus.
27 Basi, tunaweza kujivunia nini? Hakuna! Kwa nini? Je, kwa sababu ya kutimiza Sheria? La! Bali kwa sababu tunaamini.
Where [is] boasting then? It is excluded. By what law? of works? Nay: but by the law of faith.
28 Maana mtu hukubaliwa kuwa mwadilifu kwa imani, wala si kwa kutimiza matakwa ya Sheria.
Therefore we conclude that a man is justified by faith without the deeds of the law.
29 Au je, Mungu nu Mungu wa Wayahudi tu, ama pia wa watu wa mataifa mengine? Naam, wa mataifa mengine pia.
[Is he] the God of the Jews only? [is he] not also of the Gentiles? Yes, of the Gentiles also:
30 Mungu ni mmoja, naye atawakubali Wayahudi kuwa waadilifu kwa imani yao, na watu wa mataifa mengine pia kwa imani yao.
Seeing [it is] one God, which shall justify the circumcision by faith, and uncircumcision through faith.
31 Je, tunaitumia imani kuibatilisha Sheria? Hata kidogo; bali tunaipa Sheria thamani yake kamili.
Do we then make void the law through faith? God forbid: yea, we establish the law.