< Warumi 16 >

1 Napenda kumjulisha kwenu dada yetu Foibe ambaye ni mtumishi katika kanisa la Kenkrea.
Je vous recommande notre soeur Phoebé, diaconesse de l'église de Kenchrées,
2 Mpokeeni kwa ajili ya Bwana kama iwapasavyo watu wa Mungu. Mpeni msaada wowote atakaohitaji kutoka kwenu, maana yeye amekuwa mwema sana kwa watu wengi na kwangu pia.
pour que l'accueil que vous lui ferez en notre Seigneur soit digne des fidèles, et que vous l'assistiez dans toute affaire où elle pourrait avoir besoin de vous. Elle a rendu service à plusieurs personnes, à moi en particulier.
3 Salamu zangu ziwafikie Priska na Akula, wafanyakazi wenzangu katika utumishi wa Kristo Yesu.
Saluez Prisca et Aquilas, mes collaborateurs en Jésus-Christ,
4 Wao walihatarisha maisha yao kwa ajili yangu. Wanastahili shukrani; si tu kutoka kwangu, bali pia kutoka kwa makanisa yote ya watu wa mataifa mengine.
qui, pour me sauver la vie, ont exposé la leur, et je ne suis pas le seul à les en remercier, mais encore toutes les Églises des païens.
5 Salamu zangu pia kwa kanisa linalokutana nyumbani kwao. Salamu zangu zimfikie rafiki yangu Epaineto ambaye ni kwa kwanza katika mkoa wa Asia kumwamini Kristo.
Saluez aussi l'Église qui s'assemble dans leur maison. Saluez mon cher Épénète, le premier-né de l'Asie en Christ.
6 Nisalimieni Maria ambaye amefanya kazi kwa bidii kwa ajili yenu.
Saluez Marie, elle s'est donnée beaucoup de peine pour vous.
7 Salamu zangu kwa Androniko na Yunia, wananchi wenzangu waliofungwa gerezani pamoja nami; wao wanajulikana sana kati ya mitume; tena walikuwa Wakristo kabla yangu mimi.
Saluez Andronicus et Junias, mes parents et mes compagnons de captivité; ils sont distingués entre les apôtres et même ont été en Christ avant moi.
8 Salamu zangu kwa Ampliato, rafiki yangu katika kuungana na Bwana.
Saluez Amplias; il m'est cher dans le Seigneur.
9 Salamu zangu zimfikie Urbano, mfanyakazi mwenzangu katika utumishi wa Kristo; salamu zangu pia kwa rafiki yangu Staku.
Saluez Urbanus, notre collaborateur en Christ, ainsi que mon cher Stachys.
10 Nisalimieni Apele ambaye uaminifu wake kwa Kristo umethibitishwa. Salamu zangu kwa wote walio nyumbani mwa Aristobulo.
Saluez Apellès, qui est un honnête homme en Christ. Saluez les gens de la maison d'Aristobule.
11 Salamu zangu kwa Herodiana, mwananchi mwenzangu; na kwa jamaa yote ya Narkisi iliyojiunga na Bwana.
Saluez Hérodion, mon parent. Saluez les gens de la maison de Narcisse qui sont au Seigneur,
12 Nisalimieni Trufena na Trufosa wanaofanya kazi katika utumishi wa Bwana, na rafiki yangu Persi ambaye amefanya mengi kwa ajili ya Bwana.
Saluez Triphaina et Tryphosa, ouvrières dans l'oeuvre du Seigneur. Saluez ma chère Persis, elle a bien travaillé pour le Seigneur.
13 Nisalimieni Rufo, mtu hodari sana katika kazi ya Bwana, na mama yake ambaye ni mama yangu pia.
Saluez Rufus, homme distingué dans le Seigneur, et sa mère que j'appelle ma mère.
14 Nisalimieni Asunkrito, Flegoni, Herme Patroba, Herma na ndugu wote walio pamoja nao.
Saluez Asyncrytus, Phlégon, Hermès, Patrobas, Hermas et les frères qui sont avec eux.
15 Nisalimieni Filologo na Yulia, Nerea na dada yake, na Olumpa, pamoja na watu wote wa Mungu walio pamoja nao.
Saluez Philologus et Julie, Nérée et sa soeur, Olympas et tous les fidèles qui sont avec eux.
16 Salimianeni ninyi kwa ninyi kwa ishara ya upendo. Salamu kwenu kutoka kwa makanisa yote ya Kristo.
Saluez-vous les uns les autres d'un saint baiser. Toutes les Églises du Christ vous saluent.
17 Ndugu zangu, nawasihi muwafichue wote wanaosababisha mafarakano na kuwafanya watu wengine waanguke, kinyume cha mafundisho mliyofundishwa. Jiepusheni na watu hao,
Je vous invite, frères, à prendre garde à ceux qui sèment des divisions et des scandales contre la doctrine que vous avez apprise. Évitez-les;
18 maana watu wa namna hiyo hawamtumikii Kristo Bwana wetu, bali wanayatumikia matumbo yao wenyewe. Kwa maneno yao matamu na hotuba za kubembeleza hupotosha mioyo ya watu wanyofu.
car ces gens-là ne servent pas notre Seigneur Christ, mais leur ventre, et, par leurs flatteries et leurs beaux discours, ils séduisent les coeurs des simples.
19 Kila mtu amesikia juu ya utii wenu na hivyo mmekuwa sababu ya furaha yangu. Nawatakeni muwe na hekima katika mambo mema, na bila hatia kuhusu mambo mabaya.
Votre docilité est maintenant partout connue, je me réjouis donc de vous, mais je veux que vous soyez sages pour le bien et innocents devant le mal.
20 Naye Mungu aliye chanzo cha amani hatakawia kumponda Shetani chini ya miguu yenu. Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi.
Le Dieu de paix écrasera bientôt Satan sous vos pieds. La grâce de notre Seigneur Jésus soit avec vous.
21 Timotheo, mfanyakazi mwenzangu, anawasalimu. Hali kadhalika Lukio, Yasoni, na Sosipatro, wananchi wenzangu, wanawasalimu.
Timothée, mon collaborateur, vous salue, ainsi que Lucius, Jason, Sosipater, mes parents.
22 Nami Tertio, ninayeandika barua hii nawasalimuni katika Bwana.
Moi, Tertius, qui ai écrit cette lettre, je vous salue aussi en notre Seigneur.
23 Gayo, mwenyeji wangu, pamoja na kanisa lote linalokutana kwake, anawasalimu. Erasto, mweka hazina wa mji huu, pamoja na Kwarto, wanawasalimu.
Gaïus, qui me donne l'hospitalité, ainsi qu'à toute l'Église, vous salue. Éraste, le receveur de la ville, et le frère Quartus vous saluent.
24 Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi nyote. Amina.
(Que la grâce de notre Seigneur Jésus-Christ soit avec vous tous, amen.)
25 Basi, sasa na tumsifu Mungu! Yeye anaweza kuwaimarisheni katika ile Habari Njema niliyohubiri juu ya ujumbe wa Yesu Kristo, na katika ile siri iliyofunuliwa na ambayo ilikuwa imefichika kwa karne nyinyi zilizopita. (aiōnios g166)
A Celui qui peut vous fortifier dans la foi en mon Évangile et en l'enseignement de Jésus-Christ, conformément à la révélation du mystère caché durant des siècles, (aiōnios g166)
26 Lakini, sasa ukweli huo umefunuliwa kwa njia ya maandiko ya manabii; na kwa amri ya Mungu wa milele umedhihirisha kwa mataifa yote ili wote waweze kuamini na kutii. (aiōnios g166)
mais aujourd'hui dévoilé et publié dans des écrits prophétiques par l'ordre du Dieu éternel, pour amener tous les païens à obéir à la foi, (aiōnios g166)
27 Kwake Mungu aliye peke yake mwenye hekima, uwe utukufu kwa njia ya Yesu Kristo, milele na milele! Amina. (aiōn g165)
au Dieu qui seul est sage soit gloire par Jésus-Christ à jamais! Amen. (aiōn g165)

< Warumi 16 >