< Warumi 14 >

1 Mkaribisheni kwenu mtu aliye dhaifu, lakini msibishane naye juu ya mawazo yake binafsi.
Receive anyone who is weak in faith, but not for the purpose of disputing about opinions.
2 Watu huhitilafiana: mmoja imani yake inamruhusu kula kila kitu; lakini mwingine ambaye imani yake ni dhaifu, hula tu mboga za majani.
One person believes that he may eat anything, but he who is weak eats only vegetables.
3 Mtu ambaye hula kila kitu asimdharau yule ambaye hawezi kula kila kitu; naye ambaye hula tu mboga za majani asimhukumu anayekula kila kitu, maana Mungu amemkubali.
The one who eats must not despise the one who does not eat, and the one who does not eat must not judge the one who eats, for God has received him.
4 Wewe ni nani hata uthubutu kumhukumu mtumishi wa mwingine? Akisimama au akianguka ni shauri la Bwana wake; naam, atasimama imara, maana Bwana anaweza kumsimamisha.
Who are yoʋ to judge the servant of another? To his own master he stands or falls. And he will be made to stand, for God is able to make him stand.
5 Mtu anaweza kufikiria siku fulani kuwa ya maana zaidi kuliko nyingine; mtu mwingine aweza kuzifikiria siku zote kuwa sawa. Kila mmoja na afuate msimamo wa akili yake.
One person considers one day to be more important than another, while another person considers every day to be alike. Each one should be fully convinced in his own mind.
6 Anayeadhimisha siku fulani anaadhimisha siku hiyo kwa ajili ya kumtukuza Mungu; naye anayekula chakula fulani anafanya hivyo kwa kumtukuza Bwana maana anamshukuru Mungu. Kadhalika naye anayeacha kula chakula fulani anafanya hivyo kwa ajili ya kumtukuza Bwana, naye pia anamshukuru Mungu.
He who observes a particular day, observes it in honor of the Lord, while he who abstains from observing a particular day, abstains in honor of the Lord. He who eats, eats in honor of the Lord, for he gives thanks to God, while he who abstains from eating, abstains in honor of the Lord, and he gives thanks to God.
7 Maana hakuna mtu yeyote miongoni mwetu aishiye kwa ajili yake mwenyewe, wala hakuna anayekufa kwa ajili yake mwenyewe
For none of us lives for himself, and none of us dies for himself.
8 maana tukiishi twaishi kwa ajili ya Bwana; tukifa, tunakufa kwa ajili ya Bwana. Basi, kama tukiishi au tukifa, sisi ni mali yake Bwana.
If we live, we live for the Lord; and if we die, we die for the Lord. Therefore, whether we live or die, we belong to the Lord.
9 Maana Kristo alikufa, akafufuka ili wapate kuwa Bwana wa wazima na wafu.
For this reason Christ died and then rose and lived again, so that he might be Lord over both the dead and the living.
10 Kwa nini, basi wewe wamhukumu ndugu yako? Nawe, kwa nini wamdharau ndugu yako? Sisi sote tutasimama mbele ya kiti cha hukumu cha Mungu.
Yoʋ, then, why do yoʋ judge yoʋr brother? Or yoʋ, why do yoʋ despise yoʋr brother? For we will all stand before the judgment seat of Christ.
11 Maana Maandiko yanasema: “Kama niishivyo, asema Bwana kila mtu atanipigia magoti, na kila mmoja atakiri kwamba mimi ni Mungu.”
For it is written, “As I live, says the Lord, every knee will bow before me, and every tongue will give praise to God.”
12 Kwa hiyo, kila mmoja wetu atatoa hoja yake mbele ya Mungu.
So then, each of us will give an account of himself to God.
13 Basi, tuache kuhukumiana, bali tuazimie kutokuwa kamwe kikwazo kwa ndugu yetu au kumsababisha aanguke katika dhambi.
Therefore let us no longer judge one another. Instead, resolve not to put any stumbling block or snare before your brother.
14 Katika kuungana na Bwana Yesu, nina hakika kwamba hakuna kitu chochote kilicho najisi kwa asili yake; lakini, mtu akidhani kwamba kitu fulani ni najisi, basi, kwake huwa najisi.
I know and am convinced in the Lord Jesus that nothing is unclean in and of itself, but it is unclean for anyone who considers it to be unclean.
15 Kama ukimhuzunisha ndugu yako kwa sababu ya chakula unachokula, basi mwenendo wako hauongozwi na mapendo. Usikubali hata kidogo chakula chako kiwe sababu ya kupotea kwa mtu mwingine ambaye Kristo alikufa kwa ajili yake!
If yoʋr brother is distressed by what yoʋ eat, yoʋ are no longer walking in love. Do not let what yoʋ eat destroy someone for whom Christ died.
16 Basi, msikubalie kitu mnachokiona kuwa kwenu ni kitu chema kidharauliwe.
And do not let what you consider good to be spoken of as evil.
17 Maana Utawala wa Mungu si shauri la kula na kunywa, bali unahusika na kuwa na uadilifu, amani na furaha iletwayo na Roho Mtakatifu.
For the kingdom of God is not a matter of eating and drinking, but of righteousness, peace, and joy in the Holy Spirit.
18 Anayemtumikia Kristo namna hiyo humpendeza Mungu, na kukubaliwa na watu.
Anyone who serves Christ in these things is acceptable to God and approved by men.
19 Kwa hiyo tuyazingatie daima mambo yenye kuleta amani, na yanayotusaidia kujengana.
So then, let us pursue what brings about peace and mutual edification.
20 Basi, usiiharibu kazi ya Mungu kwa sababu ya ubishi juu ya chakula. Vyakula vyote ni halali, lakini haifai kula chakula ambacho kitamfanya mtu aanguke katika dhambi.
Do not tear down the work of God for the sake of food. Everything is indeed clean, but it is wrong for a person to eat anything that causes another to stumble.
21 Afadhali kuacha kula nyama, kunywa divai, au kufanya chochote ambacho chaweza kumsababisha ndugu yako aanguke.
It is good not to eat meat or drink wine or do anything by which yoʋr brother stumbles or is offended or made weak.
22 Basi, shikilia unachoamini kati yako na Mungu wako. Heri mtu yule ambaye, katika kujiamulia la kufanya, haipingi dhamiri yake.
Do yoʋ have a firm belief about these things? Have it privately before God. Blessed is he who does not condemn himself by what he approves.
23 Lakini mtu anayeona shaka juu ya chakula anachokula, anahukumiwa kama akila, kwa sababu msimamo wa kitendo chake haumo katika imani. Na, chochote kisicho na msingi wake katika imani ni dhambi.
But whoever doubts is condemned if he eats, because his action is not based on faith; and anything that is not based on faith is sin.

< Warumi 14 >