< Warumi 14 >

1 Mkaribisheni kwenu mtu aliye dhaifu, lakini msibishane naye juu ya mawazo yake binafsi.
Accept those who are still struggling to trust in God, and don't get into arguments over personal opinions.
2 Watu huhitilafiana: mmoja imani yake inamruhusu kula kila kitu; lakini mwingine ambaye imani yake ni dhaifu, hula tu mboga za majani.
One person may believe they can eat anything, while another whose trust is weak only eats vegetables.
3 Mtu ambaye hula kila kitu asimdharau yule ambaye hawezi kula kila kitu; naye ambaye hula tu mboga za majani asimhukumu anayekula kila kitu, maana Mungu amemkubali.
Those who eat anything must not look down on those who won't, and those who won't eat must not criticize those who do—for God has accepted them both.
4 Wewe ni nani hata uthubutu kumhukumu mtumishi wa mwingine? Akisimama au akianguka ni shauri la Bwana wake; naam, atasimama imara, maana Bwana anaweza kumsimamisha.
What right do you have to judge someone else's servant? It's their own master who decides whether they are right or wrong. With the Lord's help they will be able to take their stand for right.
5 Mtu anaweza kufikiria siku fulani kuwa ya maana zaidi kuliko nyingine; mtu mwingine aweza kuzifikiria siku zote kuwa sawa. Kila mmoja na afuate msimamo wa akili yake.
Some people consider some days more important than others, while others consider each day the same. Everyone should be completely convinced in their own minds.
6 Anayeadhimisha siku fulani anaadhimisha siku hiyo kwa ajili ya kumtukuza Mungu; naye anayekula chakula fulani anafanya hivyo kwa kumtukuza Bwana maana anamshukuru Mungu. Kadhalika naye anayeacha kula chakula fulani anafanya hivyo kwa ajili ya kumtukuza Bwana, naye pia anamshukuru Mungu.
Those who respect a special day do so for the Lord; and those who eat without worrying do so for the Lord since they give thanks to God; while those who avoid eating certain things do so for the Lord, and they also give thanks to God.
7 Maana hakuna mtu yeyote miongoni mwetu aishiye kwa ajili yake mwenyewe, wala hakuna anayekufa kwa ajili yake mwenyewe
None of us live for ourselves, or die for ourselves.
8 maana tukiishi twaishi kwa ajili ya Bwana; tukifa, tunakufa kwa ajili ya Bwana. Basi, kama tukiishi au tukifa, sisi ni mali yake Bwana.
If we live, we live for the Lord, or if we die, we die for the Lord—so whether we live or die, we belong to the Lord.
9 Maana Kristo alikufa, akafufuka ili wapate kuwa Bwana wa wazima na wafu.
This was the reason Christ died and came back to life—so that he could be the Lord of both the dead and the living.
10 Kwa nini, basi wewe wamhukumu ndugu yako? Nawe, kwa nini wamdharau ndugu yako? Sisi sote tutasimama mbele ya kiti cha hukumu cha Mungu.
So why do you criticize your fellow-believer? Why do you despise your fellow-believer? For all of us will stand before God's throne of judgment.
11 Maana Maandiko yanasema: “Kama niishivyo, asema Bwana kila mtu atanipigia magoti, na kila mmoja atakiri kwamba mimi ni Mungu.”
For the Scriptures say, “‘As surely as I am alive,’ the Lord says, ‘Every knee shall bow before me, and every tongue will declare that I am God.’”
12 Kwa hiyo, kila mmoja wetu atatoa hoja yake mbele ya Mungu.
So every one of us will have to explain ourselves to God.
13 Basi, tuache kuhukumiana, bali tuazimie kutokuwa kamwe kikwazo kwa ndugu yetu au kumsababisha aanguke katika dhambi.
Therefore let's not judge each other anymore, but decide to do this instead—we won't put obstacles in the way of fellow-believers, or cause them to fall.
14 Katika kuungana na Bwana Yesu, nina hakika kwamba hakuna kitu chochote kilicho najisi kwa asili yake; lakini, mtu akidhani kwamba kitu fulani ni najisi, basi, kwake huwa najisi.
I'm certain—persuaded by the Lord Jesus—that nothing in itself is ceremonially unclean. But if someone considers it to be unclean, to them it is unclean.
15 Kama ukimhuzunisha ndugu yako kwa sababu ya chakula unachokula, basi mwenendo wako hauongozwi na mapendo. Usikubali hata kidogo chakula chako kiwe sababu ya kupotea kwa mtu mwingine ambaye Kristo alikufa kwa ajili yake!
If your fellow-believer is hurt by you over matters of food, then you're no longer behaving in a loving way. Don't destroy someone for whom Christ died by the food you choose to eat.
16 Basi, msikubalie kitu mnachokiona kuwa kwenu ni kitu chema kidharauliwe.
Don't let the good things you do be misrepresented—
17 Maana Utawala wa Mungu si shauri la kula na kunywa, bali unahusika na kuwa na uadilifu, amani na furaha iletwayo na Roho Mtakatifu.
for God's kingdom is not about eating and drinking, but about living right, having peace and joy in the Holy Spirit.
18 Anayemtumikia Kristo namna hiyo humpendeza Mungu, na kukubaliwa na watu.
Anyone who serves Christ in this way pleases God, and is appreciated by others.
19 Kwa hiyo tuyazingatie daima mambo yenye kuleta amani, na yanayotusaidia kujengana.
So let's pursue the path of peace, and find ways to encourage each other.
20 Basi, usiiharibu kazi ya Mungu kwa sababu ya ubishi juu ya chakula. Vyakula vyote ni halali, lakini haifai kula chakula ambacho kitamfanya mtu aanguke katika dhambi.
Don't destroy the work of God with arguments over food. Everything is clean—but it would be wrong to eat and offend others.
21 Afadhali kuacha kula nyama, kunywa divai, au kufanya chochote ambacho chaweza kumsababisha ndugu yako aanguke.
It's better not to eat meat or drink wine or anything else that would cause your fellow-believer to stumble.
22 Basi, shikilia unachoamini kati yako na Mungu wako. Heri mtu yule ambaye, katika kujiamulia la kufanya, haipingi dhamiri yake.
What you personally believe is between you and God. Happy are those who don't condemn themselves for doing what they think is right!
23 Lakini mtu anayeona shaka juu ya chakula anachokula, anahukumiwa kama akila, kwa sababu msimamo wa kitendo chake haumo katika imani. Na, chochote kisicho na msingi wake katika imani ni dhambi.
But if you have doubts whether it's right or wrong to eat something, then you shouldn't, because you're not convinced it's right. Whatever isn't based on conviction is sin.

< Warumi 14 >