< Warumi 12 >
1 Kwa hiyo, ndugu zangu, maadam Mungu ni mwenye huruma nyingi, nawasihi kwa moyo wote: jitoleeni nafsi zenu kwa Mungu kama tambiko iliyo hai, takatifu na yenye kupendeza. Hii ndiyo njia yenu halisi ya kumwabudu.
以弟兄們! 我以天主的仁慈請你們,獻上你們的身體當作生活、聖潔和悅樂天主的祭品:這才是你們合理的敬禮。
2 Msiige mitindo ya ulimwengu huu, bali Mungu afanye mabadiliko ndani yenu kwa kuzigeuza fikira zenu. Hapo ndipo mtakapoweza kuyajua mapenzi ya Mungu, kutambua jambo lililo jema, linalompendeza na kamilifu. (aiōn )
你們不可與此世同化,反而應以新的心思變化自己,為使你們能辨別什麼是天主的旨意,什麼是善事,什麼是悅樂天主的事,什麼是全的事。 (aiōn )
3 Kutokana na neema aliyonijalia Mungu, nawaambieni ninyi nyote: msijione kuwa ni kitu zaidi kuliko mnavyopaswa kuwa. Fikira zenu na ziwe na kiasi kufuatana na kipimo cha imani Mungu aliyomgawia kila mmoja.
我因所賜給我的聖寵,告訴你們每一位:不可把自己估計得太高,而過了份;但因按天主所分與各人的信德尺度,估計得適中。
4 Mwili una viungo vingi, kila kimoja na kazi yake.
就如我們在一個身體上有許多肢體,但每個肢體,都有不同的作用;
5 Hali kadhalika ingawa sisi ni wengi, tu mwili mmoja kwa kuungana na Kristo, na kila mmoja ni kiungo cha mwenzake.
同樣,我們眾人在基督內,也都是一個身體,彼此之間,每個都是肢體。
6 Basi, tunavyo vipaji mbalimbali kufuatana na neema tuliyopewa. Mwenye kipaji cha unabii na akitumie kadiri ya imani yake.
按我們各人所受的聖寵,各有不同的恩賜:如果是說預言,就應與信德相符合;
7 Mwenye kipaji cha utumishi na atumikie. mwenye kipaji cha kufundisha na afundishe.
如果是服務,就應用在服務上;如果是教導,就應用在教導上;
8 Mwenye kipaji cha kuwafariji wengine na afanye hivyo. Mwenye kumgawia mwenzake alicho nacho na afanye hivyo kwa ukarimu. Msimamizi na asimamie kwa bidii; naye mwenye kutenda jambo la huruma na afanye hivyo kwa furaha.
如果是勸勉,就應用在勸勉上;施與的,應該大方;監督的,應該殷勤;行慈善的,應該和言悅色。
9 Mapendo yenu na yawe bila unafiki wowote. Chukieni jambo lolote ovu, zingatieni jema.
愛情不可是虛偽的。你們當厭惡惡事,附和善事。
10 Pendaneni kidugu; kila mmoja amfikirie mwenzake kwanza kwa heshima.
論兄弟之愛,要彼此相親相愛;論尊敬,要彼此爭先。
11 Msilegee katika bidii, muwe wachangamfu rohoni katika kumtumikia Bwana.
論關懷,不可疏忽;論心神,要熱切;對於主,要衷心事奉。
12 Tumaini lenu liwaweke daima wenye furaha; muwe na saburi katika shida na kusali daima.
論望德,要喜樂;在困苦中,要忍耐;在祈禱上,要恒心;
13 Wasaidieni watu wa Mungu katika mahitaji yao; wapokeeni wageni kwa ukarimu.
對聖者的急需,要分擔;對客人,要款待。
14 Watakieni baraka wote wanaowadhulumu ninyi; naam, watakieni baraka na wala msiwalaani.
迫害你們的,要祝福;只可祝福,示可詛咒。
15 Furahini pamoja na wanaofurahi, lieni pamoja na wanaolia.
應與善樂的一同善樂,與哭泣的一同哭泣。
16 Muwe na wema uleule kwa kila mtu. Msijitakie makuu, bali jishugulisheni na watu wadogo. Msijione kuwa wenye hekima sana.
彼此要同心合意,不可心高妄想,卻要俯就卑微的人。不可自作聰明。
17 Msilipe ovu kwa ovu. Zingatieni mambo mema mbele ya wote.
對人不可以惡報惡,對眾人要勉勵行善;
18 Kadiri inavyowezekana kwa upande wenu, muwe na amani na watu wote.
如若可能,應盡力與眾人和睦相處。
19 Wapenzi wangu, msilipize kisasi, bali mwachieni Mungu jambo hilo; maana Maandiko Matakatifu yasema: “Kulipiza kisasi ni shauri langu; mimi nitalipiza asema Bwana.”
諸位親愛的,你們不可為自己復仇,但應給天主的忿怒留有餘地,因為經上記載:『上主說:復仇是我的事,我必報復。』
20 Tena, Maandiko yasema: “Adui yako akiwa na njaa, mpe chakula; akiwa na kiu, mpe kinywaji. Maana kwa kufanya hivyo utamfanya apate aibu kali kama makaa ya moto juu ya kichwa chake.”
所以:『如果你的仇人餓了,你要給他飯吃;渴了,應給他水喝,因為你這樣做,是將炭火堆在他頭上。』
21 Usikubali kushindwa na ubaya, bali ushinde ubaya kwa wema.
你不可為惡所勝,反應以善勝惡。