< Warumi 10 >

1 Ndugu zangu, ninataka na kutazamia kwa moyo wangu wote hao wananchi wenzangu wakombolewe. Tena nawaombea kwa Mungu daima.
Brothers, the longing of my heart and my prayer to God is for my countrymen, that they may be saved.
2 Maana naweza kuthibitisha kwa niaba yao kwamba wanayo bidii ya kumtafuta Mungu; lakini bidii hiyo haikujengwa juu ya ujuzi wa kweli.
For I bear them witness that they have a zeal for God, only it is a zeal without knowledge.
3 Maana hawakufahamu jinsi Mungu anavyowafanya watu wawe waadilifu, na wamejaribu kuanzisha mtindo wao wenyewe, na hivyo hawakuikubali njia hiyo ya Mungu ya kuwafanya wawe waadilifu.
For because they were ignorant of God’s righteousness, and sought to establish their own righteousness, they did not submit themselves to the righteousness of God.
4 Maana kwa kuja kwake Kristo, Sheria imefikia kikomo chake, ili kila mtu anayeamini akubaliwe kuwa mwadilifu.
For to every believer Christ is an end of law as a means of righteousness.
5 Kuhusu kukubaliwa kuwa mwadilifu kwa kuitii Sheria, Mose aliandika hivi: “Mtu yeyote anayetimiza matakwa ya Sheria ataishi.”
For Moses writes concerning the righteousness of the Law, saying, The man that doeth it shall live by it.
6 Lakini, kuhusu kukubaliwa kuwa mwadilifu kwa njia ya imani, yasemwa hivi: “Usiseme moyoni mwako: Nani atapanda mpaka mbinguni? (yaani, kumleta Kristo chini);
But the righteousness of faith speaks in this way. Say not in thine heart, "Who shall ascend to heaven?" - that is, to bring Christ down;
7 wala usiseme: Nani atashuka mpaka Kuzimu (yaani, kumleta Kristo kutoka kwa wafu).” (Abyssos g12)
Nor,"who shall descend into the abyss?" - that is, to bring Christ up from the dead. (Abyssos g12)
8 Maandiko Matakatifu yesema hivi, “Ujumbe huo wa Mungu uko karibu nawe, uko kinywani mwako na moyoni mwako” nao ndio ile imani tunayoihubiri.
But what does it say? The word is near thee, even in thy mouth and in thy heart. That is the very word of faith which we preach;
9 Kama ukikiri kwa kinywa chako kwamba Yesu ni Bwana na kuamini moyoni mwako kwamba Mungu alimfufua kutoka wafu, utaokoka.
Confess with your mouth "Jesus is Lord," and believe in your heart that God actually raised him from the dead, and you will be saved.
10 Maana tunaamini kwa moyo na kukubaliwa kuwa waadilifu; na tunakiri kwa midomo yetu na kuokolewa.
For with the heart man believes unto righteousness, and with the mouth confession is made unto salvation.
11 Maandiko Matakatifu yasema: “Kila amwaminiye hatakuwa na sababu ya kuaibika.”
The Scriptures say, Whoever believes in Him will not be put to shame.
12 Jambo hili ni kwa wote, kwani hakuna tofauti kati ya Wayahudi na wasio Wayahudi; Bwana wa wote ni mmoja, naye ni mkarimu sana kwao wote wamwombao.
For there is no difference between Jew and Gentile, because the same Lord Jesus is all over, and is rich unto all who call upon Him;
13 Maana Maandiko Matakatifu yasema: “Kila mtu atakayeomba kwa jina la Bwana, ataokolewa.”
for Whoever will call upon the name of the Lord will be saved.
14 Basi, watamwombaje yeye ambaye hawamwamini? Tena, watamwaminije kama hawajapata kusikia habari zake? Na watasikiaje habari zake kama hakuna mhubiri?
How then shall thy call upon Him in whom they do not believe? And how are they to believe in One of whom they have never heard? And how shall they hear without a preacher?
15 Na watu watahubirije kama hawakutumwa? Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: “Ni jambo la kupendeza mno kuja kwa wale wanaohubiri Habari Njema!”
And how can men preach unless they are sent? As it is written, How beautiful are the feet of those who bring a glad gospel.
16 Lakini wote hawakuipokea hiyo Habari Njema. Maana Isaya alisema: “Bwana, ni nani aliyeamini ujumbe wetu?”
And yet they did not all hearken to the good news; for Isaiah said, Lord, who hath believed our message?
17 Hivyo basi, imani inatokana na kuusikiliza ujumbe, na huo ujumbe unatokana na neno la Kristo.
So faith comes from a message heard, and the message comes from the teaching of Christ.
18 Lakini nauliza: je, hawakuusikia huo ujumbe? Naam, waliusikia; kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: “Sauti yao imeenea duniani kote; maneno yao yamefika mpaka kingo za ulimwengu.”
But I ask, Did they fail to hear? Yes, truly, Their sound has gone out unto all the earth, And their words unto the ends of the world.
19 Tena nauliza: je, yawezekana kwamba watu wa Israeli hawakufahamu? Mose mwenyewe ni kwa kwanza kujibu: “Nitawafanyeni mwaonee wivu watu ambao si taifa; nitawafanyeni muwe na hasira juu ya taifa la watu wapumbavu.”
But I say, Did Israel not know? First Moses says. I will provoke you to jealousy with that which is no nation; Against a Gentile nation, void of understanding, will I anger you.
20 Tena Isaya anathubutu hata kusema: “Wale ambao hawakunitafuta wamenipata; nimejionyesha kwao wasiouliza habari zangu.”
But Isaiah speaks very boldly, I was found of those who were not seeking me, I was made manifest to those who were not asking for me.
21 Lakini kuhusu Israeli anasema: “Mchana kutwa niliwanyoshea mikono yangu watu waasi na wasiotii.”
But to Israel he says, All day long I have been spreading out my hands unto a disobedient and contrary people.

< Warumi 10 >