< Warumi 10 >

1 Ndugu zangu, ninataka na kutazamia kwa moyo wangu wote hao wananchi wenzangu wakombolewe. Tena nawaombea kwa Mungu daima.
Brothers, truly my heart's desire and my supplication to God for Israel is for salvation.
2 Maana naweza kuthibitisha kwa niaba yao kwamba wanayo bidii ya kumtafuta Mungu; lakini bidii hiyo haikujengwa juu ya ujuzi wa kweli.
For I testify to them that they have a zeal of God, but not according to knowledge.
3 Maana hawakufahamu jinsi Mungu anavyowafanya watu wawe waadilifu, na wamejaribu kuanzisha mtindo wao wenyewe, na hivyo hawakuikubali njia hiyo ya Mungu ya kuwafanya wawe waadilifu.
For not understanding the righteousness of God, and seeking to establish their own righteousness, they did not submit to the righteousness of God.
4 Maana kwa kuja kwake Kristo, Sheria imefikia kikomo chake, ili kila mtu anayeamini akubaliwe kuwa mwadilifu.
For Christ is the end of law for righteousness, to every man who believes.
5 Kuhusu kukubaliwa kuwa mwadilifu kwa kuitii Sheria, Mose aliandika hivi: “Mtu yeyote anayetimiza matakwa ya Sheria ataishi.”
For Moses writes in the righteousness from the law, that the man that does them will live in them.
6 Lakini, kuhusu kukubaliwa kuwa mwadilifu kwa njia ya imani, yasemwa hivi: “Usiseme moyoni mwako: Nani atapanda mpaka mbinguni? (yaani, kumleta Kristo chini);
But the righteousness from faith says thus: Thou should not say in thy heart, Who will ascend into heaven? (that is, to bring Christ down)
7 wala usiseme: Nani atashuka mpaka Kuzimu (yaani, kumleta Kristo kutoka kwa wafu).” (Abyssos g12)
or, Who will descend into the abyss? (that is, to bring Christ up from the dead). (Abyssos g12)
8 Maandiko Matakatifu yesema hivi, “Ujumbe huo wa Mungu uko karibu nawe, uko kinywani mwako na moyoni mwako” nao ndio ile imani tunayoihubiri.
But what does it say? The word is near thee, in thy mouth and in thy heart, that is, the word of faith that we preach:
9 Kama ukikiri kwa kinywa chako kwamba Yesu ni Bwana na kuamini moyoni mwako kwamba Mungu alimfufua kutoka wafu, utaokoka.
that if thou will confess with thy mouth, the Lord Jesus, and will believe in thy heart that God raised him from the dead, thou will be saved.
10 Maana tunaamini kwa moyo na kukubaliwa kuwa waadilifu; na tunakiri kwa midomo yetu na kuokolewa.
For a man believes in the heart for righteousness, and he confesses with the mouth for salvation.
11 Maandiko Matakatifu yasema: “Kila amwaminiye hatakuwa na sababu ya kuaibika.”
For the scripture says, Every man who believes in him will not be shamed.
12 Jambo hili ni kwa wote, kwani hakuna tofauti kati ya Wayahudi na wasio Wayahudi; Bwana wa wote ni mmoja, naye ni mkarimu sana kwao wote wamwombao.
For there is no distinction of a Jew and also of a Greek, for the same Lord is of all men, being rich toward all those who call upon him.
13 Maana Maandiko Matakatifu yasema: “Kila mtu atakayeomba kwa jina la Bwana, ataokolewa.”
For every man, whoever may call upon the name of the Lord will be saved.
14 Basi, watamwombaje yeye ambaye hawamwamini? Tena, watamwaminije kama hawajapata kusikia habari zake? Na watasikiaje habari zake kama hakuna mhubiri?
How then will they call on whom they have not believed? And how will they believe of whom they have not heard? And how will they hear without preaching?
15 Na watu watahubirije kama hawakutumwa? Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: “Ni jambo la kupendeza mno kuja kwa wale wanaohubiri Habari Njema!”
And how will they preach unless they are sent? Just as it is written, How beautiful are the feet of those who proclaim good news of peace, of those who proclaim good news of good things.
16 Lakini wote hawakuipokea hiyo Habari Njema. Maana Isaya alisema: “Bwana, ni nani aliyeamini ujumbe wetu?”
But not all were obedient to the good news, for Isaiah says, Lord, who has believed our report?
17 Hivyo basi, imani inatokana na kuusikiliza ujumbe, na huo ujumbe unatokana na neno la Kristo.
So faith is from hearing, and hearing by the word of God.
18 Lakini nauliza: je, hawakuusikia huo ujumbe? Naam, waliusikia; kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: “Sauti yao imeenea duniani kote; maneno yao yamefika mpaka kingo za ulimwengu.”
But I say, did they, no, not hear? Rather, Their voice went forth into all the earth, and their sayings to the limits of the inhabited world.
19 Tena nauliza: je, yawezekana kwamba watu wa Israeli hawakufahamu? Mose mwenyewe ni kwa kwanza kujibu: “Nitawafanyeni mwaonee wivu watu ambao si taifa; nitawafanyeni muwe na hasira juu ya taifa la watu wapumbavu.”
But I say, did Israel, no, not know? First Moses says, I will provoke you to jealousy toward a non-nation. Toward a foolish nation, I will make you angry.
20 Tena Isaya anathubutu hata kusema: “Wale ambao hawakunitafuta wamenipata; nimejionyesha kwao wasiouliza habari zangu.”
And Isaiah is very bold and says, I was found by those not seeking me. I became manifest to those not asking for me.
21 Lakini kuhusu Israeli anasema: “Mchana kutwa niliwanyoshea mikono yangu watu waasi na wasiotii.”
But to Israel he says, The whole day I stretched forth my hands to a disobedient and rebellious people.

< Warumi 10 >