< Ufunuo 1 >

1 Hizi ni habari za mambo ambayo yalifunuliwa na Yesu Kristo. Mungu alimpa Kristo ufunuo huu ili awaonyeshe watumishi wake mambo ambayo yanapaswa kutukia karibuni. Kristo alimtuma malaika wake amjulishe Yohane, mtumishi wake, mambo hayo,
The Revelation of Jesus Christ, which God gave to him, to show unto his servants the thing which it behooves speedily to come to pass; and he signified having sent by his angel to his servant John;
2 naye Yohane, ameyasema yote aliyoyaona. Na hii ndio taarifa yake kuhusu ujumbe wa Mungu na ukweli uliofunuliwa na Yesu Kristo.
who witnessed the word of God, and the testimony of Jesus Christ, as to so many things as he saw.
3 Heri yake mtu anayesoma kitabu hiki; heri yao wale wanaosikiliza maneno ya ujumbe huu wa kinabii na kushika yaliyoandikwa humu, maana wakati umekaribia ambapo mambo haya yatatukia.
Blessed is the one reading, and those hearing the word of the prophecy, and keeping the things which have been written in it: for the time is at hand.
4 Mimi Yohane nayaandikia makanisa yaliyoko mkoani Asia. Nawatakieni neema na amani kutoka kwake yeye aliyeko, aliyekuwako na anayekuja; na kutoka kwa roho saba walio mbele ya kiti chake cha enzi,
John to the seven churches which are in Asia: Grace to you, and peace, from the one who is, and who was, and who is coming; and from the seven Spirits which are before his throne;
5 na kutoka kwa Yesu Kristo, shahidi mwaminifu, wa kwanza kufufuliwa kutoka wafu, na ambaye ni mtawala wa wafalme wa dunia. Yeye anatupenda, na kwa damu yake ametufungua kutoka vifungo vya dhambi zetu,
and from Jesus Christ, who is the faithful witness, the firstbegotten of the dead, and the prince of the kings of the earth. To the one loving us with divine love, and having washed us from our sins in His own blood,
6 akatufanya sisi kuwa ufalme wa makuhani, tumtumikie Mungu, Baba yake. Kwake Yesu Kristo uwe utukufu na nguvu, milele na milele! Amina. (aiōn g165)
and He made us a kingdom, priests unto God even his Father; to him be glory and dominion unto the ages of the ages; amen. (aiōn g165)
7 Tazama! Anakuja katika mawingu! Kila mtu atamwona, hata wale waliomchoma. Makabila yote duniani yataomboleza juu yake. Naam! Amina.
Behold, he is coming with clouds; and every eye shall behold him, even those who pierced him, and all the tribes of the earth will wail at him; yes, Amen.
8 “Mimi ni Alfa na Omega,” asema Bwana Mungu Mwenye Uwezo, aliyeko, aliyekuwako na anayekuja.
I am Alpha and Omega, says the Lord God, who is and who was, and who is coming, the Almighty.
9 Mimi ni Yohane, ndugu yenu; na kwa kuungana na Kristo nashiriki pamoja nanyi katika kustahimili mateso yanayowapata wale walio wa Utawala wake. Mimi nilikuwa kisiwani Patmo kwa sababu ya kuhubiri ujumbe wa Mungu na ukweli wa Yesu.
I John, your brother, and companion in tribulation, and in the kingdom and in patience in Jesus, was in the island which is called Patmos, on account of the word of God, and on account of the testimony of Jesus.
10 Basi, wakati mmoja, siku ya Bwana, nilikumbwa na Roho, nikasikia nyuma yangu sauti kubwa kama sauti ya tarumbeta.
I was in the Spirit on the Lord's day, and I heard behind me a great voice, as of a trumpet
11 Nayo ilisema, “Andika katika kitabu yote unayoyaona, ukipeleke kwa makanisa haya saba: Efeso, Smurna, Pergamoni, Thuatira, Sarde, Filadelfia na Laodikea.”
saying, Write what you are seeing in a book, and send it to the seven churches; unto Ephesus, and unto Smyrna, and unto Pergamum, and unto Thyatira, and unto Sardis, and unto Philadelphia, and unto Laodicea.
12 Basi, nikageuka nimwone huyo aliyesema nami, nikaona vinara vya taa saba vya dhahabu,
And I turned to see the voice which was speaking with me; and having turned, I saw seven golden candlesticks;
13 na katikati yake kulikuwa na kitu kama mtu, naye alikuwa amevaa kanzu ndefu na ukanda wa dhahabu kifuani.
and in the midst of the candlesticks one like the Son of man, clothed with a garment down to his feet, and girded about the breast with a golden girdle.
14 Nywele zake zilikuwa nyeupe kama pamba safi, kama theluji; macho yake yalimetameta kama moto;
And his head and his hairs were as wool, white as snow; and his eyes were like a flame of fire;
15 miguu yake iling'aa kama shaba iliyosafishwa katika tanuru ya moto na kusuguliwa, na sauti yake ilikuwa, kama sauti ya poromoko la maji.
and his feet were like brass, as having been burned in a furnace; and his voice as the sound of many waters,
16 Katika mkono wake wa kulia, alikuwa na nyota saba, na kinywani mwake mlitoka upanga wenye makali kuwili. Uso wake uling'aa kama jua kali.
and having in his right hand seven stars: and out of his mouth is going forth a sharp two-edged sword: and his countenance like the sun shines in his strength.
17 Basi, nilipomwona tu, nilianguka mbele ya miguu yake kama maiti. Lakini yeye akaweka mkono wake wa kulia juu yangu, akasema, “Usiogope! Mimi ni wa kwanza na wa mwisho.
And when I saw him, I fell at his feet like a dead man; and he laid his right hand on me, saying, Fear not; I am the first and the last:
18 Mimi ni yeye aliye hai! Nilikuwa nimekufa, lakini, tazama, sasa ni mzima milele na milele. Ninazo funguo za kifo na Kuzimu. (aiōn g165, Hadēs g86)
the living one, and I was dead; and, behold, I am alive unto the ages of the ages, and I have the keys of death and of Hades. (aiōn g165, Hadēs g86)
19 Basi, sasa andika mambo haya unayoyaona, mambo yanayotukia sasa na yale yatakayotukia baadaye.
Therefore write the things which you have seen, and the things which are, and the things which are about to take place after these;
20 Siri ya nyota zile saba ulizoziona katika mkono wangu wa kulia, na siri ya vile vinara saba vya taa hii: zile nyota saba ni malaika wa makanisa; na vile vinara saba vya taa ni makanisa saba.
and the mystery of the seven stars which you saw in my right hand, and the seven golden candlesticks. The seven stars are the angels of the seven churches: and the seven golden candlesticks are the seven churches.

< Ufunuo 1 >