< Ufunuo 8 >

1 Na Mwanakondoo alipouvunja mhuri wa saba, kukawa kimya mbinguni kwa muda wa nusu saa.
and (when(-ever) *N(k)O*) to open the/this/who seal the/this/who seventh to be silence in/on/among the/this/who heaven as/when half an hour
2 Kisha nikawaona wale malaika saba wanaosimama mbele ya Mungu wamepewa tarumbeta saba.
and to perceive: see the/this/who seven angel which before the/this/who God to stand and to give it/s/he seven trumpet
3 Malaika mwingine akafika, akiwa anachukua chetezo cha dhahabu, akasimama mbele ya madhabahu ya kufukizia ubani. Naye akapewa ubani mwingi autoe sadaka pamoja na sala za watu wote wa Mungu, juu ya madhabahu ya dhahabu iliyo mbele ya kiti cha enzi.
and another angel to come/go and to stand upon/to/against (the/this/who altar *N(k)O*) to have/be censer golden and to give it/s/he incense much in order that/to (to give *N(k)O*) the/this/who prayer the/this/who holy: saint all upon/to/against the/this/who altar the/this/who golden the/this/who before the/this/who throne
4 Moshi wa ubani ukapanda juu, pamoja na sala za watu wa Mungu, kutoka mikononi mwake huyo malaika aliyekuwa mbele ya Mungu.
and to ascend the/this/who smoke the/this/who incense the/this/who prayer the/this/who holy: saint out from hand the/this/who angel before the/this/who God
5 Kisha malaika akakichukua hicho chetezo, akakijaza moto wa madhabahuni akakitupa duniani. Kukawa na ngurumo, sauti, umeme na tetemeko la ardhi.
and to take the/this/who angel the/this/who censer and to fill it/s/he out from the/this/who fire the/this/who altar and to throw: throw toward the/this/who earth: planet and to be thunder and voice/sound: noise and lightning and earthquake
6 Kisha wale malaika saba wenye tarumbeta saba wakajiweka tayari kupiga mbiu ya mgambo.
and the/this/who seven angel the/this/who to have/be the/this/who seven trumpet to make ready (it/s/he *N(k)O*) in order that/to to sound a trumpet
7 Malaika wa kwanza akapiga tarumbeta yake. Mchanganyiko wa mvua ya mawe na moto, pamoja na damu, ukamwagwa juu ya nchi. Theluthi moja ya nchi ikaungua, theluthi moja ya miti ikaungua, na majani yote mabichi yakaungua.
and the/this/who first (angel *K*) to sound a trumpet and to be hail and fire to mix in/on/among blood and to throw: throw toward the/this/who earth: planet (and the/this/who third the/this/who earth: planet to burn *NO*) and the/this/who third the/this/who tree to burn and all grass green to burn
8 Malaika wa pili akapiga tarumbeta yake. Na kitu kama mlima mkubwa unaowaka moto ukatupwa baharini. Theluthi moja ya bahari ikawa damu,
and the/this/who secondly angel to sound a trumpet and as/when mountain great fire to kindle/burn to throw: throw toward the/this/who sea and to be the/this/who third the/this/who sea blood
9 theluthi moja ya viumbe vya baharini vikafa na theluthi moja ya meli zikaharibiwa.
and to die the/this/who third the/this/who creature the/this/who in/on/among the/this/who sea the/this/who to have/be soul and the/this/who third the/this/who boat (to destroy *N(k)O*)
10 Kisha malaika wa tatu akapiga tarumbeta yake. Na nyota kubwa ikiwaka kama bonge la moto, ikaanguka kutoka mbinguni, na kutua juu ya theluthi moja ya mito na chemchemi za maji.
and the/this/who third angel to sound a trumpet and to collapse out from the/this/who heaven star great to kindle/burn as/when window and to collapse upon/to/against the/this/who third the/this/who river and upon/to/against the/this/who flow the/this/who water
11 (Nyota hiyo inaitwa “Uchungu.”) Basi, theluthi moja ya maji yakawa machungu; watu wengi wakafa kutokana na maji hayo, kwa sababu yaligeuka kuwa machungu.
and the/this/who name the/this/who star to say: call (the/this/who *no*) wormwood and (to be *N(k)O*) the/this/who third the/this/who water toward wormwood and much the/this/who a human to die out from the/this/who water that/since: since to embitter
12 Kisha malaika wa nne akapiga tarumbeta yake. Ndipo theluthi moja ya jua, ya mwezi na ya nyota ikapata pigo; hata mwangaza ukapoteza theluthi moja ya mng'ao wake. Theluthi moja ya mchana ikakosa mwanga, hali kadhalika na theluthi moja ya usiku.
and the/this/who fourth angel to sound a trumpet and to strike the/this/who third the/this/who sun and the/this/who third the/this/who moon and the/this/who third the/this/who star in order that/to to darken the/this/who third it/s/he and the/this/who day not (to shine/appear *N(k)O*) the/this/who third it/s/he and the/this/who night similarly
13 Kisha nikatazama, nikasikia tai akiruka juu kabisa angani anasema kwa sauti kubwa, “Ole, ole, ole kwa wanaoishi duniani wakati malaika watatu waliobaki watakapopiga tarumbeta zao!”
and to perceive: see and to hear one (eagle *N(K)O*) to fly in/on/among midair to say voice/sound: voice great woe! woe! woe! (the/this/who to dwell *N(k)O*) upon/to/against the/this/who earth: planet out from the/this/who remaining voice/sound: voice the/this/who trumpet the/this/who Three angel the/this/who to ensue to sound a trumpet

< Ufunuo 8 >