< Ufunuo 8 >
1 Na Mwanakondoo alipouvunja mhuri wa saba, kukawa kimya mbinguni kwa muda wa nusu saa.
And when he opened the seventh seal, there followed a silence in heaven, about the space of half an hour.
2 Kisha nikawaona wale malaika saba wanaosimama mbele ya Mungu wamepewa tarumbeta saba.
And I saw the seven angels who stand before God, and seven trumpets were given them.
3 Malaika mwingine akafika, akiwa anachukua chetezo cha dhahabu, akasimama mbele ya madhabahu ya kufukizia ubani. Naye akapewa ubani mwingi autoe sadaka pamoja na sala za watu wote wa Mungu, juu ya madhabahu ya dhahabu iliyo mbele ya kiti cha enzi.
And another angel came and stood at the altar, having a golden censer, and a great quantity of incense was given him to mingle with the prayers of all the saints upon the golden altar, which was before the throne.
4 Moshi wa ubani ukapanda juu, pamoja na sala za watu wa Mungu, kutoka mikononi mwake huyo malaika aliyekuwa mbele ya Mungu.
And the smoke of the incense, with the prayers of the saints, rose up from the hand of the angel into the presence of God.
5 Kisha malaika akakichukua hicho chetezo, akakijaza moto wa madhabahuni akakitupa duniani. Kukawa na ngurumo, sauti, umeme na tetemeko la ardhi.
Then the angel took the censer, and he filled it with fire from the altar, and poured it upon the earth; and there followed thunders and voices and lightnings and an earthquake.
6 Kisha wale malaika saba wenye tarumbeta saba wakajiweka tayari kupiga mbiu ya mgambo.
And the seven angels with the seven trumpets prepared to blow their trumpets.
7 Malaika wa kwanza akapiga tarumbeta yake. Mchanganyiko wa mvua ya mawe na moto, pamoja na damu, ukamwagwa juu ya nchi. Theluthi moja ya nchi ikaungua, theluthi moja ya miti ikaungua, na majani yote mabichi yakaungua.
And the first angel blew his trumpet, and there followed hail and fire mingled with blood, and it fell upon the earth; and the third part of the earth was burned up, and the third part of the trees, and all the green grass.
8 Malaika wa pili akapiga tarumbeta yake. Na kitu kama mlima mkubwa unaowaka moto ukatupwa baharini. Theluthi moja ya bahari ikawa damu,
And the second angel blew his trumpet, and something like a great mountain burning with fire was hurled into the sea; and a third part of the sea became blood;
9 theluthi moja ya viumbe vya baharini vikafa na theluthi moja ya meli zikaharibiwa.
and a third part of the living creatures in the sea died, and the third part of the ships were destroyed.
10 Kisha malaika wa tatu akapiga tarumbeta yake. Na nyota kubwa ikiwaka kama bonge la moto, ikaanguka kutoka mbinguni, na kutua juu ya theluthi moja ya mito na chemchemi za maji.
And the third angel blew his trumpet, and there fell from heaven a great star, blazing like a torch. It fell upon a third of the rivers and upon the springs. (The name of the star is called Wormwood.)
11 (Nyota hiyo inaitwa “Uchungu.”) Basi, theluthi moja ya maji yakawa machungu; watu wengi wakafa kutokana na maji hayo, kwa sababu yaligeuka kuwa machungu.
A third part of the waters became wormwood; and many men died of the waters, because they were made bitter.
12 Kisha malaika wa nne akapiga tarumbeta yake. Ndipo theluthi moja ya jua, ya mwezi na ya nyota ikapata pigo; hata mwangaza ukapoteza theluthi moja ya mng'ao wake. Theluthi moja ya mchana ikakosa mwanga, hali kadhalika na theluthi moja ya usiku.
And the fourth angel blew his trumpet, and the third part of the sun was blasted, and a third part of the moon, and a third part of the stars; so that the third part of them should be darkened, and for a third part of the day there was no light, and at night it was the same.
13 Kisha nikatazama, nikasikia tai akiruka juu kabisa angani anasema kwa sauti kubwa, “Ole, ole, ole kwa wanaoishi duniani wakati malaika watatu waliobaki watakapopiga tarumbeta zao!”
And I looked and I heard a solitary eagle flying in mid-heaven, and crying with a loud voice, "Woe, woe, woe for all who live on the earth, Because of the rest of the trumpet-blasts That the three angels are about to blow!"